Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Kane ni complete package, endapo akitua OT ni fire, ebu angalia hapo chini tu
Bruno+Pogba+Rashford+Kane=CORONA

Tatizo naloliona club sidhani kama itaweza fanya usajiri mbili kubwa dirisha moja, hapa itategemea na kipaumbele cha OGS either #7 au striker

Sent using Jamii Forums mobile app
 

Mkuu umejuaje kama anaipenda Manchester United


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kiufundi kitu pekee kinachoweza kuzuia Harry kujiunga nasi ni hofu ya Ole kum-drop mshambuliaji mmoja wapo kati ya Marcus or Anthony (most likely). Kichwani kwake namuona kama anaamini sana wanaweza kumtoa.

Kiukweli tunapaswa kum-drop Anthony kwa sasa tubaki na Marcus pamoja na Mason ili tumu-accommodate Harry. Anthony tumempa nafasi sana sioni chochote kwake kwa misimu mitano mpaka sasa tokea 2015/2016 amecheza mechi 136 na kufunga goli 45 tu.

Kwa timu kubwa kama Manchester United mshambuliaji ambaye ni tegemeo mwenye takwimu kama za Anthony ni mbovu sana, kwa wastani anafunga goli 9 kwa msimu. It's time to let that boy go.
 
PTER hawa Inter milan ni kweli wana dhamira ya dhati ya kupambana na Juventus kwa muda mrefu?

target zao za usajili sizielewi...
Nadhani Intermilan wanatafuta quickfix solution kwanza ndiyo waanze kutafuta mwelekeo mpya.

Wamepotea muda mrefu sana toka kizazi chao cha kina Cambiasso, Christian Chivu, Pandev, Sneider, Milito, Lucio na wengineo kilipowapa mafanikio hawajarudi tena katika ushindani ndani ya Italy na Ulaya kwa ujumla.

Katika kipindi hicho wamejitahidi kutengeneza kikosi cha vijana na wachezaji wazoefu lakini wameshindwa kupambana na Juventus na walau hata AS Roma na SS Napoli wamegeuka kuwa wababe kuliko Inter.

Sasa kwa sasa wanachokifanya nikutafuta njia fupi itakayowarudisha juu ndiyo waanze kusafiri kutaka kupambana na Juventus.

Jambo jingine Inter Milan hawana financial muscles kama aliyonayo Juventus hivyo wanalazimika kufanya kila linalowezekana kudhibiti matumizi makubwa ya fedha ambayo hawana wakati huo huo wakiupa muda nafasi ya kuamua hatima yao.

Nafikiri kwa hali waliopo bado wako kwenye mwelekeo sahihi itategemea na bahati yao na ubora wa mpango wao utakavyoweza kutoa matokeo chanya.

Tuupe nafasi muda utasema.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
sasa mkuu tufanyaje?..tuvunje mkataba?
Kusema kweli Sanchez ni liability kubwa sana kwa Man United kwa sasa.

Kule Italy kavamiwa na majeraha na hajacheza mechi nyingi.

Akirejea Old Trafford sijui atakuwa anafanya kazi gani.

Bora wambadilishie majukumu awe Usher pale Stretford end.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
kwa hivyo na wao wameamua kutumia njia ile ile waliyoitumia juventus ya kusajili wachezaji waliokwisha thibitisha ubora wao huko wanakotoka, wasi wasi wangu upo kwenye umri wa wachezaji husika wanaosajiliwa na wanaovumishiwa kuwahitaji kama vile olivier giroud, sidhani kama watadumu kwa muda mrefu kwenye soka la ushindani kwa kuangalia viwango vyao (ashley young, victor moses, diego godin, asamoah).

Jambo jingine Inter Milan hawana financial muscles kama aliyonayo Juventus hivyo wanalazimika kufanya kila linalowezekana kudhibiti matumizi makubwa ya fedha ambayo hawana wakati huo huo wakiupa muda nafasi ya kuamua hatima yao.
hapo pana ukweli ndani yake kwa sababu kabla hata ya Calciopoli (kashfa ya kupanga matokeo msimu wa 2005/2006) tayari juventus walishakuwa vinara wa ligi ya Italy, kutoka mwaka 1995/96 walifanikiwa kubeba ubingwa mara 6, milan mara 3 na lazio mara 1.

ina maana kurudi kwao kwenye ligi ya serie A baada ya kushushwa daraja walikuja tu kuendeleza moto wao uliozoeleka tokea zamani.

Kama Inter Milan wanahitaji kupambana na Juventus basi njia pekee itakayowasaidia ni kujikusanyia pato kubwa litakalotokana na operation zinazofanyika ndani ya klabu (mapato ya uwanja, jezi, mikataba ya kibiashara, haki za televisheni n.k) lakini kama watategemea nguvu ya fedha ya mwenyekiti wa klabu basi watarudi tena nyuma kama ilivyokuwa kwa AC Milan au kama ilivyokuwa chini ya moratti (baada ya kuondoka mourinho).

nadhani conte pekee hatoshi kuiokoa Inter Milan, bali pia wanahitaji vichwa vyengine vyenye mipango madhubuti ya kuongoza mpira wa kisasa kama ilivyo kwa juventus iliojengwa na Blanc, Marotta, Paratici, Nedvěd.

nawaombea wapate mafanikio yatakayodumu kwa muda mrefu ili warudishe heshima ya SERIE A
 
Beppe Marotta now yupo Inter Milan baada ya Juventus kurudi serie A combination ya Conte+Marotta,Nedved & Paratici ndio wali-engineer mafanikio yao currently hao 2 wako Inter,ligi ya Italy haiitaji sana young players ndio ufanikiwe ndio maana mpaka leo still backbone ya Juve inawategemea Chielini,Bonucci,CR7,Matuidi,Cuadrado,Khedira ,CR7 while young players like Bernadeshi,De Legt,Emre Can,Rabiot bado wana-struggle miaka ya karibuni Inter walikuwa na many good young players (Icardi,Brozovic,Skirniar,Lautaro,De Vrij) na majority hawajawahi kushinda chochote na recently hawajawahi kuwa na winner manager like Conte unlike Juventus ambao wanasajili winners (Matuidi,CR7,Costa,Rabiot,Ramsey) na ukiangalia tofauti ya benchi la Juventus na Inter ni kubwa currently Inter target at least kupata nafasi ya kucheza champions league ambapo since Mourinho era walipotea kabisa
 
Manchester United mko mbioni kupoteza wapenzi wenu watakaohamia Newcastle United. Wale mliokuwa mnavaa jezi za Shearer, Faustino Asprilla miaka ya 90 tunawajua.
Man u, Liverpool na Arsenal kibongo bongo ndio team zenye mashabiki loyal si kama chelsea na Man city wengi ni Glory hunters.
Tegemea hao kuhama iwapo Newcastle atakuwa vizuri.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…