Binafsi ningependa Harry Kane awe chaguo #1 ktk watu wanaopaswa kuja kuiweka sawa timu yetu hao wengine wawe ni fallback plan tu baada ya dili la Harry kubuma. Tunahitaji kuweka mezani Pound Sterling 100M take-it-or-leave-it Deal, baada ya hili janga la Covid-19 hakuna timu itakayo kuwa tayari kutanua bajeti kizembe zembe kama sio hitaji la msingi na timu pekee duniani yenye uhitaji wa mshambualiaji na yenye pesa ni Manchester United tu.
nakubaliana na hoja yako,
harry kane ni aina ya mchezaji ambaye pindi anapokuwepo sokoni huhitaji kujiuliza mara mbili ili ufanye uamuzi wa kumsajili, ndio maana baadhi yetu humu ndani tumekuwa tukisisitiza kwa nyakati tofauti ya kwamba halitakuwa jambo rahisi kwa klabu kufanya biashara mbili za gharama kubwa kwa dirisha moja (usajili wa harry kane na mchezaji mwengine wa kiingereza either maddison, grealish au jadon sancho).
cha kufanya ni kupiga hesabu kwa umakini zaidi ili kuweza kufahamu eneo lipi ni muhimu zaidi kulifanyia uwekezaji (mshambuliaji au winga wa kulia tatizo ambalo tunalo kwa takribani miaka 8), wengine wanashauri usajili wa gharama uelekezwe kwa mshambuliaji kama ulivyoeleza hapo juu na wengine tunashauri usajili wa gharama uelekezwe zaidi kwa winga mfano wa jadon sancho.
Pia wengine wanaamini usajili muhimu unapaswa uelekezwe kwa mchezaji atakayetupa faida zaidi ya moja atapokuwepo uwanjani (mfano jack grealish, james maddison wote wana uwezo wa kufiti nafasi na mfumo zaidi ya mmoja).
nafahamu kama tunahitaji depth squad basi uamuzi utakaofanyika hauhitaji kuangalia zaidi taathira zitakazowapata wachezaji fulani tunaopenda kuwaona wakiendelea kupewa nafasi... lakini itapendeza zaidi endapo sadaka tutakayoitoa isiwaumize na kuwavunja moyo na morali vijana wetu wenye ndoto za kuongoza jahazi la mapambano siku za mbeleni
usajili wa
jadon sancho:
usajili huu utakuja kupunguza dakika za kucheza alizokuwa akipewa
mason greenwood msimu huu., kupitia mechi za msimu huu tumeshuhudia mechi nyingi sana alizokuwa akicheza greenwood alikuwa anatokea zaidi upande wa kulia kuliko eneo la striker eneo ambalo siku za mwishoni za romelu lukaku alikuwa akichezeshwa kabla ya kuhama kwake. Kiupande wangu naendelea kuamini ya kwamba mason greenwood hapaswi kuwa mchezaji tegemezi kwenye kikosi chetu hivyo basi tunahitaji mchezaji mwengine mwenye uzoefu na kiwango kikubwa zaidi ya mason ili awe namba 7 wetu wa kudumu, namuona jadon akiwa ni mchezaji sahihi kama atakuja na kiwango kile tunachokishuhudia borussia dortmund.
Pia usajili wa mchezaji aina ya jadon utapelekea kuzibwa au kupungua kwa nafasi ya
daniel james kwenye kikosi cha kwanza, tukumbuke mechi nyingi sana za msimu huu baada ya rashford kurudishwa upande wa kushoto tulishuhudia daniel james akichezeshwa upande wa kulia...Hii ina maana ya kwamba daniel james atakwenda kugombania namba na marcus rashford upande wa kushoto (ni challenge ngumu sana kwake lakini haiepukiki)
kwa nini
Ighalo?
si mshambuliaji bora mbele ya kane, jimenez na wengineo lakini uwepo wake ndani ya kikosi utakuwa ni tofauti na hao wengineo kwa sababu tayari ameshajiandaa kuishi maisha ya kuwa mchezaji asiyehitajika mara kwa mara kwenye kikosi cha kwanza. Litakuwa ni pigo kubwa sana kiupande wetu kwa sababu tutaendelea kumtegemea goigoi anthony martial lakini itakuwa ni faida kubwa sana kwa wachezaji wengineo mfano mason greenwood.....upo utofauti mkubwa sana pindi unapogombania namba dhidi ya kane au ighalo.
pia uwepo wa Ighalo utasaidia zaidi kutuepusha na panic transfer,utatuwezesha kumonitor au kuangalia tena mwenendo wa anthony martial (tukumbuke huu ndio kwanza msimu wake wa kwanza martial kucheza eneo la striker mechi nyingi zaidi lakini takwimu zake zinaonyesha kufunga zaidi magoli kuliko washambuliaji wengine) pamoja na mason greenwood ambaye bado hatujajua ubora wake kama striker wa team kubwa,
wakati huo huo uwepo wa ighalo utasaidia katika harakati zetu za kutafuta na kuwachunguza washambuliaji wengine watakaokuja kuziba nafasi yake kama vile haaland kama ataendelea kuwepo dortmund, martinez kama atakuwepo inter milan, levit kama ataendelea kuwepo everton n.k.
sancho + bruno fernandez + pogba= martial na rashford watakuwa na uhakika wa kutupa magoli 20 kwa kila mmoja.
striker tunaovumishwa kuwahitaji msimu huu dhidi ya martial
Martial - 14 goals in 26 games (msimu wake wa kwanza kucheza eneo la ushambuliaji mechi nyingi)
Jimenez - 16 goals in 35 games
Dembele - 17 goals in 32 games (anacheza French league)
Edouard - 28 goals in 43 games (anacheza Scottish league)
Maxi Gomez - 6 goals in 22 games
Calvert Lewin - 13 goals in 23 games (everton)
===========================================