likizo yangu imekwisha
- phil jones
- jesse lingard
- andreas perreira
- marcos rojo
operation safisha taka taka inapaswa iendelee kwa kuwaondoa watumishi hao wanne (nitamheshimu sana OGS kama atatimiza mpango huu)
kama tutawaondoa hao walinzi wawili hakutakuwa na ulazima wa kutafuta mlinzi mwengine wa kati kwa bei ya gharama kwa sababu
chris smalling tunaweza kumrudisha kikosini, vile vile upo uwezekano wa kumtumia luke shaw kama mlinzi wa kati hata kwenye mfumo wa kutumia walinzi wa nne ikitokezea harry maguire anahitaji mapumziko (hakuna lisilowezekana kwa mchezaji professional kubadilishwa nafasi pia references zipo nyingi kama vile david alaba, joshua kimmich, philip lahm na sergio ramos),
ukiachana na ole gunnar solskjaer na benchi lake la ufundi , kiukweli
jesse lingard na
andreas perreira wameturudisha nyuma sana msimu huu kwenye kampeni yetu ya kurudisha ubora wa timu yetu (ole aliweka matumaini makubwa sana kwa hawa vijana kabla ya ligi kuanza, bahati mbaya wameshindwa kumtihibitishia mwalimu na mashabiki juu ya umuhimu wao wa kuendelea kuaminiwa kikosini)......
kuna kila dalili mmoja wao kati ya hao wawili nafasi yake ikazibwa na mchezaji wa kiengereza japokuwa wapo wageni wenye viwango vizuri kama
van der beek na
martin ordegaard, kwa sasa ni wachezaji wawili tu ndio wamekuwa kwenye rada (james maddison na jack grealish), sidhani kama tuna uwezo wa kuwasajili wachezaji wote wawili kwa pamoja.
yupi ni bora kati yao msimu huu?
kiukweli sifahamu kwa sababu kwanza sijawahi kungalia mechi za aston villa hata mara moja (labda tumuulize ujugu kuhusiana na grealish) , pia nikiangalia takwimu za maddison nahisi kama kiwango cha utoaji huduma kimepungua sana msimu huu pengine ni mabadiliko ya kimajukumu aliopewa na mwalimu ndio chanzo (sina uhakika)... wanavyosema wadau ni kwamba faida ya jack grealish ana uwezo wa kucheza nafasi tofauti kwa kiwango cha juu.
andreas perreira ana miaka 24 ya kuzaliwa, naweza kusema ndiye mchezaji wetu aliyetumika kwenye nafasi nyingi tofauti bila ya kulalamikia maamuzi ya walimu, alipokuwa spain (granada na valencia) kwa nyakati tofauti kama nitakuwa sahihi alitumika kama winga, aliporudi klabuni chini ya jose alitumika kama double pivot midfield, alipokuja ole amekuwa akipendelea sana kumtumia kwenye mfumo 4-3-3 na pia kama namba 10.
andreas amejaaliwa bidii ya kupambana, solid mentality lakini amenyimwa ubora (quality), hana sifa za kuwa winga bora, hana sifa za kuwa kiungo bora wa ulinzi kama makelele, hana sifa za kuwa kiungo mshambuliaji bora hususani anapokuwa na mpira ndio maana si ajabu kumkuta akiwa na takwimu zisizoridhisha akiwa kama ni kiungo mshambuliaji.
ukiniuliza ni eneo gani bora ambalo
andreas anacheza vizuri, jibu litakuwa sijui na sitaki kujua..
ni muda muafaka kwake yeye kutafuta timu isiyokuwa na presha ili apate kujijenga zaidi kwenye career yake ya soka na pia kulitambua zaidi eneo lake sahihi la kiuchezaji, hata kama atabaki msimu ujao nahofia atakuwa na msimu mgumu sana kiuchezaji.
habari njema kwa wote ni kwamba
fred ameanza kutoka usingizini japokuwa ana ugonjwa wa kuanguka ovyo kama wilder..
tuliowahi kumtukana
fred tukutane hapa tupate kuandaa waraka wa kuunga mkono juhudi za muheshimiwa manywele.