Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Sasa mbona hiyo article yako inaonesha ni tactic ambayo Martinez aliitumia mahususi kwa ajili ya mechi ile, lakini wewe unatuambia humu kana kwamba Rom huwa anachezeshwa winger siku zote

Au mkuu umeweka source bila kusoma yote, au umewekewa?

Nakumbuka enzi za Fergie, kuna mechi tuliwafunga Arsenal goli 2 karibu timu nzima walicheza mabeki kasoro Rooney na Chicharito. Mechi hiyo Fabio alicheza winger ya kushoto na Rafael akacheza winger ya kulia, unavyoonekana wewe ulivyoiona hiyo game ukawa unasema Fabio amekuwa winger.

Mkuu tactical change za game 1 au 2 usifanye kama Ubelgiji ndio huwa wanacheza hivyo, that was exceptional case. Rom has always been played at center forward position.

Nasisitiza tu kuwa hizi zama ni ngumu sana kudanganya na uongo ukadumu
Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ubelgiji hachezi winger mkuu, usichukue mechi moja ambayo Martinez aliamua kufanya tactical twist (dhidi ya Brazil) halafu ndio utuambie kwamba hiyo ndio namba anayocheza

Hata ukisoma link uliyotuma inaonesha ilikuwa kama surprise tactic dhidi ya Brazil

Romelo Lukaku Bolingoli Ubelgiji anacheza namba tisa, mshambuliaji wa kati
belgium anacheza wapi? amehama huko nako?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu kuna vitu vingine viko wazi an so obvious sisi sote ni MAN UNITED Fans nia ya mijadala yetu mwisho wa siku ni kushuhudia timu yetu pendwa ikifanya vizuri.

Ni sahihi na ni ukweli ulio Wazi anachokisema Mdau hapo kwamba handling ya Issue ya Lukaku ilimfanya ahisi kutohitajika an of course akajikuta amekua provoked mpaka kumiss behave hadi kuvujisha stats za mazoezini akionyesha kwamba kile anachotuhumiwa si kweli kwani wawapo mazoezini ana perform far better than others (that was a stupid mistake).

Kuhusu "Kirusi" Pogba kama kilivyo itwa na Mourinho haihitaji Phd ya Falsafa ili kubaini ukweli kwamba as for now team ndio inamkumbatia zaidi but yeye Mara kadhaa performance yake, matendo yake ya kutojituma ipasavyo na matamshi ya waribu yake vyote vinathibitisha kwamba Kimwili yupo nasi ila Kimoyo yupo somewhere else.


Ile interview ya kaka yake unadhani it was just an interview? Imani yangu ni kwamba yule alikua ana reveal mazungumzo yao mengi ya kinyumbani nyumbani pia Agent wake the way anavyo tu criticise unadhani ni bure tu?


Mwisho furaha yetu ni team kufanya vizuri, turudi kwenye zama zetu za ubora wetu, tutampinga na kumkosoa yeyote tunaye dhani na kuona mbinu zake haziisaidii na kuuiimarisha team tuliyochagua kuipenda unconditionally.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
You Nailed it Mh. Kada wa Chama twawala.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Umeiweka vizuri sana, huu ndio ukweli halisi
Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hata mfumo wa ole 4-3-3 wa kulia na kushoto ni mastriker kitaalamu wanaitwa inside forward, greenwood anatokea kulia na ni striker. Hakuna tofauti yoyote na hio ya ubelgiji na ole mwenyewe amelisema kwa mdomo wake.

Hata beckham alivyoondoka kabla ya Ronaldo kuanza 1st team ole alipelekwa pembeni na kuwa support ya Rvn, so is suarez kwa sturidge, lacazete kwa Auba, etc ni jambo common sana kwenye mpira.

Na ukitaka full match ya brazil na ubelgiji pia naweza kukuekea.
 
Mkuu mimi ni mmoja wa wadau humu wakati watu wanatake side ya pogba na kumponda mourinho nilikuwa upande wa kocha, na nilitaka kipindi kile kile wakiondoka waondoke wote, kama ole hamtaki pogba ataondoka, kama pogba hataki man U ataondoka vile vile, ila mambo mengi ambayo yanasemwa juu ya huyu jamaa ni uzushi, mchezaji pia kaka yake kusema ana dream ya kucheza spain ni jambo baya? As long as ana mkataba na ni proffesional akautii huo mkataba kuna ubaya gani?

Pogba huyu huyu december amecheza mechi mbili sijui tatu hali ya kuwa ni majeruhi na maumivu, pogba huyu huyu halalamiki akichezeshwa out of position, jamaa muda wote amekuwa proffesional.

Na kuhusu huyo lukaku mkuu ame submit official kwa wahusika kwamba anataka kuondoka mwezi wa 3 na amekubaliwa as a proffesional alitakiwa kutii mkataba wake, lakini kitendo cha kujibizana na man u na kutoa siri za mazoezini kinaonyesha jinsi alivyo insecure, na according to luke shaw ole aliwaambia wakimbie taratibu hivyo hata zile data alizovujisha amedanganya kwamba yeye ni fast player.

Hii mada ya lukaku iishe hapa mkuu ila naomba hii comment iwe reference tuone inter itaishia vipi
 
Kama Sanchez,Di Maria hahah

Sent using Jamii Forums mobile app
Kwa kweli walifurahia single digit lkn inakuwa ngumu sana babae.

Sanchez sijui, di maria hana nyota, kwa sasa ukimuuliza hata mtoto anaweza akasema di maria ni mchezaji wa Yanga. Yaani hasikiki kabisa. Tofauti na wakati flan akiwa Madrid, alikuwa nyota sijui nani kaizima babae.
 
Hata ole siku aliomchezesha lukaku pembeni(dhidi ya Arsenal) ilikuwa ni tactical twist, si kwamba siku zote alikuwa akimchezesha pembeni. Mfano mechi ya psg lukaku alikuwa mbele.
 
Ukienda ufaransa unadowngrade mkuu hata neymar kapotea.
 
Kwa Kua umependekeza mada hiyo iishie hapo nami naungana na wewe kwa afya yetu sote as MAN UNITED Fans ni vizuri kufunga mjadala huo.

Nisahihi kabisa nakumbuka kweli kwamba ulikua upande wa Kocha that time.

Luka is no more Man United player so tumuache nasi tujadili tulivyo navyo, shortage ya mfungaji mwenye njaa iliyokithiri ambaye yuko tayari hata kuvunjika pua ili timu ifunge, Management mbovu inayojali faida za kiuchumi na isiyofahamu mahitaji halisi ya soka (hapa namzungumzia ED Na Wamiliki Glazers family), team kukosa consistence Leo inacheza hivi kesho vile, mbinu za hovyo katika kusajili mchezaji unamkosa kwa hela ndogo then unalazimika kumchukua January kwa hela zaid (rejea tukio la Bruno Fernandez).


Naunga mkono kila ghasia anazofanyiwa Ed angalau yeye binafsi na Glazers family wataheshimu position yetu fans katika team, perhaps watafeel maumivu yetu yakufungwa na team ambazo zinataka kushuka daraja wamepafanya Old Trafford kua ni Uwanja wa kawaida kawaida tu kwamba yeyote anaweza pata matokea.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Una maana gani?

Sent using Jamii Forums mobile app
Kuna comment nyingine unazisoma halafu kama joto la mwili linakupanda hivi,maana zinakuwa tofauti kabisa na unachokitaka au unachokiamini..That's football though

I Love Fred,workrate yake ni kubwa sana,na nilikuwa nime-write off,lakini msimu huu ulivyochanganya ameni-prove wrong..Kuna talent pale

Ni swala la Kocha kutafuta combination ambayo wachezaji wata-complement each other..Mfano Fred unamchezesha na mtu kama Matic(kwenye ubora wake),atakachosaidia Matic ni kucontrol game kwenye high pressure,then unamwongeza Fernandes anakuwa anatoa pass laana za magoli na kufunga..

Shida ni kuwa,kuna watu wanataka hadi Fred awe anafunga..sasa nauliza How many Goals did Carrick scored for us??
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…