Niliitazama mechi ya jana kwa jicho la mtazamaji Neutral.
Baada ya first half nilibaki nikijiuliza je Man united walikosa mbinu sahihi kupambana na Liverpool au walikosa watu sahihi wa kupambana na Liverpool?
Ukiangalia kimbinu Man united hawakuzidiwa sana ndiyo maana walifanikiwa kuuzima ubora wa Trent Alexander Anorld na Andy Robertson.
Walifanikiwa kumfanya Sadio Mane na Firimino pamoja na Moh Salah kwa dakika zote 90 wawe wa kawaida ukiachilia mbali dakika 15 za first half na 15 za second half.
Kimsingi Liverpool siyo bora sana kwenye eneo Lao la kati ukilinganisha na maeneo mengine yote ya uwanja hivyo threat pekee za Liverpool zinatengenezwa pembeni na dead ballls.
Hatari nyingine ambayo unapaswa kuwapa Liverpool heshima ya kiwango cha juu ni kwenye second balls hapa United walifanikiwa kwa kiwango walau 58% ila kujisahau kwao kuliwafanya waadhibiwe goal la pili.
Kwa kujibu swali langu la kwanza ni kwamba United walifanikiwa kujilinda kupunguza magoli ila walishindwa kuwazuia Liverpool kufunga magoli kibaya zaidi walikosa pia maarifa ya kupata walau goal.
Kwenye hoja yangu ya pili juu ya watu sahihi wa kupambana na Liverpool hapa ndiyo ulikuwa ugonjwa mkubwa sana wa United.
United hawatishi katika eneo lolote lile la uwanja ukiondoa counter attacks za hapa na pale.
1 kiulinzi united wanakosa mengi sana kuanzia goal kipa na safu yake yote ya ulinzi.
2 kwenye kiungo cha ukabaji kuna mapungufu mengi sana ya kiufundi yanayoifanya timu ijikabe yenyewe hasa unapomkosa Mc Tominay na Pogba transition ya timu inakuwa mbovu na yakubahatisha tu.
3 safu ya ushambuliaji ya united ilikuwa haina watu sahihi wa kuifunga Liverpool na wala haikuwa threat kwa Liverpool kivyovyote vile.
Itoshe kusema kwamba mechi ya jana Man united walibebwa na bahati ya kutofungwa magoli mengi tu hasa dakika 15 za kipindi cha pili ambacho Liverpool walikuwa hatari sana na waliweza kuwashika United kila mahali.
Hivyo basi United kwa kiasi fulani walikosa mbinu sahihi za kuifunga Liverpool na pia kiasi kikubwa walikosa watu sahihi wa kuweza kuifunga Liverpool.
Sent using
Jamii Forums mobile app