Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Hili povu...mdau yeye ana furaha tu kuwa amukukunyuga jana basi.
Hayo mengine sidhani kama alikuwa anayahitaji sana

Sent using Jamii Forums mobile app
We toka uujue mpira umewah kusikia hii timu haijafungwa? Sema jana ilikuwa ni siku ya vibonde hata aston villa na wataford walishinda huwa kwenye ligi inatokea hasa kwa timu zinazogombea kuto kushuka daraja mwenzio west ham katakata pia nne bila
 
Hapa sipingani na ww huu ni uchafu hata norwich hachez huyu hana namba mi nahisi uchaw upo ulaya fikiria lukaku anapondwa kila uchwao hii takataka ipo tu had leo kazidiwa magoli na smalling na lindelof kwa mwaka 2019
Yaani hivi vitoto vya kiingereza ni majanga.... Siunaona hata huku kwetu Willock majanga matupu na wanawaamini, halafu wanaoumia ni mashabiki.... Kama mm Jana nilivyoona tu lineup nikapata confidence... Sio muda wa kubebana huu.., kama huna kiwango,second half ndo utaingia...
 
We toka uujue mpira umewah kusikia hii timu haijafungwa? Sema jana ilikuwa ni siku ya vibonde hata aston villa na wataford walishinda huwa kwenye ligi inatokea hasa kwa timu zinazogombea kuto kushuka daraja mwenzio west ham katakata pia nne bila
Mancity na Leicester vepeee
 
Hv ulishawahi kumuona Ferguson akicheka pale United inapopoteza?Ferguson alikuwa anaonyesha hisia fulani ambazo zilikuwa zinaonyesha wazi amekasirika.Alikuwa mpaka analaumu waamuzi na kutoa lugha kali.Alishawahi kusema kwenye press conference 'nashangaa leo mwamuzi alikuwa hawezi kukimbia kwenda na kasi ya mchezo.Nadhani alikuwa ameshiba sana lunch.'

Alipigwa faini na kufungiwa mechi alipotoa hii kauli.Labda ndio maana watu wengi mpaka leo wanaamini kwamba United ilikuwa inabebwa na waamuzi lakini press conference ndiyo inatoa picha halisi ya aina gani ya kocha aliyepo kwenye timu.

Ole Gunnar Solskjaer jana kwenye press conference alionyesha wazi kwamba anaishukuru 'mizimu 'iliyompa bahati ya kuwa kocha wa timu kubwa kama United.Alisema 'pamoja na kupoteza tulicheza vizuri 'huku akitabasamu.Tena sio kwa tabasamu la kawaida kawaida tu. Tabasamu lile wazungu wanaloita 'genuine smile kama anavyoonekana kwenye picha hapo chini.

Usingeweza kuona kitu kama hiki kutoka kwa Ferguson.Siku ambayo United ingepoteza dhidi ya Arsenal ungemuona tu akiwa amefura macho mekundu 'kwa kweli tulikuwa ovyo sana leo tumeruhusu magoli rahisi sana'.Lakini asingeweza kuongea hivyo huku akiwa anatabasamu wakati ametoka kufungwa na Arsenal.United mara nyingi huifunga Arsenal iwe Emirates au Old Trafford.

Ole Gunnar Solskjaer ana bahati kubwa kuifundisha United. Ni kijana wa Carrington.Ni United 'through and through na anapokaa kwenye bench washabiki wote wanajifeel wapo na mtu mwenye damu ya United Lakini ni muhimu awe halisi na asiwe kama muigizaji mbele ya vyombo vya habari.View attachment 1309982
Halafu mbona anaanza kufanana na Mou!? Ha ha ha atatuumiza sana huyu mwalimu
 
Back
Top Bottom