kabla ya kufikia makubaliano ya kumpa mkataba jose mourinho:
- je bodi walikuwa hawafahamu ya kwamba huyu jamaa (mourinho) ni mtumiaji wa pesa sana kama alivyofanya chelsea na real madrid?
- walikuwa hawafahamu ya kwamba jose mourinho huwa hapendelei sana kuangalia umri wa mchezaji pindi anapohitaji huduma yake ( rejea usajili wa ibrahimovic, samuel etoo, michael ballack, diego millito, carvalho ricardo kuelekea real madrid)
- je! bodi ya klabu walipokuwa wanampa mkataba jose mourinho walikuwa hawafahamu ya kwamba huyu jamaa hana tabia ya kuwavumilia wachezaji wake pindi wanapokuwa ovyo au asipowahitaji (kwa mfano pendekezo la kutafutwa mchezaji wa kuziba nafasi ya mkhitaryan aliyeshuka kiwango, pia rejea usajili wa ashley cole kwenda chelsea na william gallas kwenda arsenal)
bila ya shaka walikuwa wanayafahamu yote na ndio maana walifikia makubaliano pande zote mbili ya kufanya kazi kwa pamoja.
namnukuu ed woodward
===== tuko vizuri sana kwenye eneo la kibiashara kuliko timu yoyote duniani na matokeo ya ndani ya uwanja hayaleti athari kubwa sana kwenye biashara zetu.
===== manchester united ndiyo timu pekee yenye uwezo wa kumsajili mchezaji yoyote kwenye soko la usajili bila ya kupata athari yoyote na kwa hilo namuahidi kocha nitayafanyia kazi mapendekezo yake
kwa nini manchester united walishindwa kumtimizia baadhi mahitaji yake haliyakuwa ed woodward ameshajisifu mara nyingi sana ya kwamba klabu ina uwezo wa kumsajili mchezaji yoyote anayetakiwa na mwalimu?
kuhusu kushindwa kuwatumia ipasavyo wachezaji wake aliowasajili nalo pia si geni kwa jose mourinho kwani huko nyuma alishawahi kufanya vimbwanga kama hivyo (rejea usajili wa asiel del horno,lassana diarra, shevchenko, mateja kezman) na ndio maana nikauliza hapo juu kuhusiana na utambuzi wa bodi juu ya suala hili kabla hawajampa kandarasi jose mourinho.
pia mourinho si kocha pekee mwenye tabia mbovu kama hiyo ya kushindwa kuwavumilia wachezaji wake pindi wanapocheza chini ya kiwango hata josep guardiola pia anayo tabia hiyo na bado ameendelea kuwa nayo tabia hiyo (kwa kuwa ni guardiola basi hakuna anayehoji)
- wakati guardiola anamuondoa nolito ambaye alimsajili yeye mwenyewe kwa kutokuendana na falsafa yake msimu wake wa pili alionekana malaika lakini mourinho alipomuondoa mkhitaryan kwa kushindwa kuwa kwenye kiwango msimu wake wa pili alionekana ni mwanadamu asiyekuwa na chembe ya uvumilivu.
- guardiola alimsajili claudio bravo akashindwa kufikia matarajio yake na hatimaye msimu wa pili akatumia tena fedha nyingi kwa usajili ederson (ndani ya misimu miwili josep guardiola alitumia takribani paundi millioni 70 kwa usajili wa magoal keeper)
- wakati guardiola anasajili walinzi wawili wa kushoto (benjamin mendy na laporte) huku akimuondoa mlinzi mwengine mahiri ambaye ni kolarov alionekana ni malaika lakini mourinho alipoomba apewe fungu la usajili kwa ajili ya alex sandro alionekana ni shetani asiye na uvumilivu, unabaki kujiuliza kama ni guardiola je angeliendelea kumtumia luke shaw na ashley young kama walinzi wake haliyakuwa amemuondoa alexandre kolarov na gael clichy?
- guardiola alimsajili zlatan ibrahimovic na msimu uliofuata alimuondoa na nafasi yake ilizibwa na david villa kama nitakuwa nipo sahihi.
- kama guardiola aliweza kuwandoa wachezaji kama joe hart, bacary sagna, gael clichy, zabaleta pablo, alexander kolarov, samir nasri, jesus navas, wilfried bony, mangala, martin demicheliss na kelechi iheanacho ndani ya misimu miwili je. kama angelikuwepo manchester united angeliendelea kufanya kazi na wachezaji kama smalling na phil jones kwa moyo mkunjufu.?
yaliopita si ndwele na tunapaswa tugange yajayo
twende na Ole gunnar solskjaer japo kishingo upande huenda akatufikisha kwenye safari yetu ya matumaini.
nafasi ya nne bado ipo wazi