Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Unaposema Ed ndio aliowajri Lvg n Mou unakosea, kuhusu kuwajiri Lvg na Mou ni bodi nzima ndio inapendekeza Manager awe nani, Ed ni Makamu Mwenyekiti kwa cheo chake inamlazimu kutangaza maamuzi ya bodi

Ed ni kama Senzo wa Simba, bodi maamuzi wanayofanya na yeye akiwemo, anayatangaza maamuzi kwa press

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Na pia makocha wanalazimishwa kuwachezesha hao wachezaji waliosajiliwa na Ed au??
 
Mou alieleza wazi wachezaji walioletwa wakati yeye akiwa hawahitaji, na hata hivyo Ole hajafikia mafanikio ya Mou hapo Man u hivyo usiwe mwepesi kupuuza watangulizi wake.
Mkuu ManUtd ya sasa ipo ktk mikono salama, itasajiri hata mchezaj wa 100pounds ila typical utd player, sio kina Mou na Lvg walituletea mizigo inayofikiria hela kuliko kuvuja jasho

Sent using Jamii Forums mobile app

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Usisahau, ndani ya muda mfupi tu Mou alichukua europa na kwenye ligi akiwa wa pili pamoja na hao wachezaji wa kuunga unga, Ole mpe hata miaka 3, hachukui kombe lolote.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu umesema vizuri sana, Mou hakupata sapoti ya kutosha, aliletewa wachezaji asiowahitaji na bado alifanya vizuri, wachezaji aliowahitaji akina Maguire wamesajiliwa baada ya yeye kuondoka, wachezaji aliokuwa anawaweka bench hawakupata namba hata baada ya yeye kuondoka, tena wengine wameondoka klabuni, ila hata vijana aliowaamini kwa kuwapa namba ndio tegemeo kwa sasa. Ila unafiki mwingine ni kuwa wakati wa Mou focus ya club ilikuwa kuchukua makombe, huku wachezaji wastaafu wa man walikuwa wamejazana kwenye TV stations wakikosoa kila kinachofanywa, ila baada ya mwenzao kupewa timu focus imebadilika na sasa wanazungumzia kujenga culture ya Man U! Unafiki mkubwa!
Sent using Jamii Forums mobile app
 
Maguire alikuwa choice ya Mourinho, Bissaka kafanya vizur so far, ila pia usisahau hata Lukaku mliyemuuza huko aliko ni moto wa hatari.
Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu seems bado hata huelewi structure ya Man u inavyo operate.

Ed ndio CEO wetu ndio mtu mkubwa zaidi kiutendaji. Yeye ndio mwenye last say na ndio ameajiriwa na wamiliki wa timu ku over see kila kitu.

Juu ya Ed kuna Joel na Avram glazzer tu unaweza kuiangalia Bodi ya Man U hapa
Board of Directors

Vision ya Ed ndio vision ya man utd na anaajiri kutokana na muono wake ulivyo. Ndio maana watu walio chini yake wote ni kama yeye ambao hawajui lolote kuhusu mpira wengi ni bankers mfano mzuri ni huyo Matt judge ambae yupo responsible kunegotiate mishahara ( na sio kocha wa timu kama ulivyochapia huko juu)

Soma vizuri hao top executive wote then niambie nani mtu wa mpira? Then kaangalie timu kama Bayern ama ajax ama barcelona ama juve ndio utajua tatizo la Man U ni nini.

Na uingereza ni timu mbili tu so far ambazo hazina dof Man U na Newcastle na wote wanafanana Tabia zao.
 
kabla ya kufikia makubaliano ya kumpa mkataba jose mourinho:
  • je bodi walikuwa hawafahamu ya kwamba huyu jamaa (mourinho) ni mtumiaji wa pesa sana kama alivyofanya chelsea na real madrid?
  • walikuwa hawafahamu ya kwamba jose mourinho huwa hapendelei sana kuangalia umri wa mchezaji pindi anapohitaji huduma yake ( rejea usajili wa ibrahimovic, samuel etoo, michael ballack, diego millito, carvalho ricardo kuelekea real madrid)
  • je! bodi ya klabu walipokuwa wanampa mkataba jose mourinho walikuwa hawafahamu ya kwamba huyu jamaa hana tabia ya kuwavumilia wachezaji wake pindi wanapokuwa ovyo au asipowahitaji (kwa mfano pendekezo la kutafutwa mchezaji wa kuziba nafasi ya mkhitaryan aliyeshuka kiwango, pia rejea usajili wa ashley cole kwenda chelsea na william gallas kwenda arsenal)
bila ya shaka walikuwa wanayafahamu yote na ndio maana walifikia makubaliano pande zote mbili ya kufanya kazi kwa pamoja.

namnukuu ed woodward
===== tuko vizuri sana kwenye eneo la kibiashara kuliko timu yoyote duniani na matokeo ya ndani ya uwanja hayaleti athari kubwa sana kwenye biashara zetu.
===== manchester united ndiyo timu pekee yenye uwezo wa kumsajili mchezaji yoyote kwenye soko la usajili bila ya kupata athari yoyote na kwa hilo namuahidi kocha nitayafanyia kazi mapendekezo yake

kwa nini manchester united walishindwa kumtimizia baadhi mahitaji yake haliyakuwa ed woodward ameshajisifu mara nyingi sana ya kwamba klabu ina uwezo wa kumsajili mchezaji yoyote anayetakiwa na mwalimu?

kuhusu kushindwa kuwatumia ipasavyo wachezaji wake aliowasajili nalo pia si geni kwa jose mourinho kwani huko nyuma alishawahi kufanya vimbwanga kama hivyo (rejea usajili wa asiel del horno,lassana diarra, shevchenko, mateja kezman) na ndio maana nikauliza hapo juu kuhusiana na utambuzi wa bodi juu ya suala hili kabla hawajampa kandarasi jose mourinho.

pia mourinho si kocha pekee mwenye tabia mbovu kama hiyo ya kushindwa kuwavumilia wachezaji wake pindi wanapocheza chini ya kiwango hata josep guardiola pia anayo tabia hiyo na bado ameendelea kuwa nayo tabia hiyo (kwa kuwa ni guardiola basi hakuna anayehoji)
  • wakati guardiola anamuondoa nolito ambaye alimsajili yeye mwenyewe kwa kutokuendana na falsafa yake msimu wake wa pili alionekana malaika lakini mourinho alipomuondoa mkhitaryan kwa kushindwa kuwa kwenye kiwango msimu wake wa pili alionekana ni mwanadamu asiyekuwa na chembe ya uvumilivu.
  • guardiola alimsajili claudio bravo akashindwa kufikia matarajio yake na hatimaye msimu wa pili akatumia tena fedha nyingi kwa usajili ederson (ndani ya misimu miwili josep guardiola alitumia takribani paundi millioni 70 kwa usajili wa magoal keeper)
  • wakati guardiola anasajili walinzi wawili wa kushoto (benjamin mendy na laporte) huku akimuondoa mlinzi mwengine mahiri ambaye ni kolarov alionekana ni malaika lakini mourinho alipoomba apewe fungu la usajili kwa ajili ya alex sandro alionekana ni shetani asiye na uvumilivu, unabaki kujiuliza kama ni guardiola je angeliendelea kumtumia luke shaw na ashley young kama walinzi wake haliyakuwa amemuondoa alexandre kolarov na gael clichy?
  • guardiola alimsajili zlatan ibrahimovic na msimu uliofuata alimuondoa na nafasi yake ilizibwa na david villa kama nitakuwa nipo sahihi.
  • kama guardiola aliweza kuwandoa wachezaji kama joe hart, bacary sagna, gael clichy, zabaleta pablo, alexander kolarov, samir nasri, jesus navas, wilfried bony, mangala, martin demicheliss na kelechi iheanacho ndani ya misimu miwili je. kama angelikuwepo manchester united angeliendelea kufanya kazi na wachezaji kama smalling na phil jones kwa moyo mkunjufu.?
yaliopita si ndwele na tunapaswa tugange yajayo
twende na Ole gunnar solskjaer japo kishingo upande huenda akatufikisha kwenye safari yetu ya matumaini.
nafasi ya nne bado ipo wazi
 
Vita nafasi ya 4

Wapinzani wanaofuata kwa Man Utd na Chelsea

Man Utd VS Everton, Watford, Newcastle & Burnley

Chelsea Vs Tottenham, Southampton, Arsenal & Brightom

Kaugonjwa ka mechi ndogo kasiturudie

Sent using Jamii Forums mobile app
hizi team ndogo tunapaswa tuzifunze adabu ili zikome kutuzowea..
dalili zinaonyesha dhahiri ya kwamba chelsea atapoteza alama nne ndani ya mechi nne zijazo
 
Sanchez at Treatre of dreams was a Joke
swadakta brother
tulitegemea makubwa sana kutoka kwake kupitia miguu yake ila ikawa kinyume chake, hata huko inter milan hana nafasi na sidhani kama watakuwa tayari kumpa mkataba wa kudumu.

Tuombe matajiri wa kichina, japan au waarabu wahitaji huduma yake ili tuondokane na mzimu wake.

habari njema ni kwamba hata usajili wa henrikh mkhitaryan umeshindwa kuwafaidisha arsenal.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…