Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Tutapata hata penalt kweli leo?
aahhaaa! Kwa uchezaji wa DJ, Martial na Rashford hakuna mechi inayoweza kuisha bila possible penalty. Sema marefa huwa wanaamua kubana zingine. Sheffield wapo aggressive sana, hawataepuka makosa ndani ya box.

Muhimu defence iwe vizuri na chances zitumie vizuri, maana Sheffield wanapiga mpira mkali.

Naamini ushindi upo.
 
Sheffield VS Man Utd

Sheffield atakuwa nyumbani dhidi ya United wa Manchester

Katika mechi 5 za mwisho Sheffield hajapoteza game hata 1, game 3 ame draw na 2 kashinda zote akiwa nyumbani

Tangu SAF astaafu, katika mechi 19 ugenini dhidi ya timu za wapanda daraja, United ameshinda mechi 11, ame draw mechi 2 na kufungwa mechi 6

Katika mechi 7 za mwisho, the Blades (Sheffield) dhidi ya United, the Blades amepigwa mechi zote kwa jumla ya magoli 14 kwa 1.

Wachezaji muhimu ambao hawatakuwepo. United watamkosa Tominay, Pogba, pengine na Matic, Tuanzebe na Shaw kwa kukosa match fitness

Wakati huo huo the Blades watawakosa wachezaji 2 mmoja amepata majeraha kwenye National Team na namba 1 wao Dean Henderson ambaye ni golikipa wa United anayekipiga pale Bramal Lane kwa mkopo

Wachezaji chipukizi wanaoweza kupata nafasi kwa United kutokana na majeraha ya first teamers ni James Garner na Dylan Levit (midfielders) na Brandon Williams (left back)

Mechi itapigwa saa 1:30 usiku pale Bramal Lane
 
Back
Top Bottom