Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Ole tumpe mkataba wa kudumu mkuu.

Kila la kheri Chelsea
 
Kabla ya kuwauza kina Sanchez na Lukaku angeanza na kina Lingard, Rashford.

James ni mahututi kati ya marehemu. Kuchukua mchezaji bora ni kwamba hakuna kitu tena kwenye hiyo timu.

Ole sio mkali kama unavyosema manake kuna mediocre players anazidi kuwapa nafasi na bado hawana wanafanya uwanjani. Makocha wakali ni kina Pep, ukifanya makosa unakaa benchi mechi inayofuata. Huo ukali wa Ole ni upi kama unauza Lukaku unaacha Rashford anayekupa goli 5 msimu mzima? Unaona anachofanya Pogba? Uchafu wa Lingard unauona? Uozo wa Pereira hauonekani? Nioneshe ukali wa Ole.

Unaanza msimu na wachezaji kama Chong, Greenwood, kweli? Na upo comfortable kabisa?

Ole anatumia formation mbovu, haimpi matokeo na bado anaendelea kuitumia kila siku. Huyo ni kocha kweli?
 
Dirisha lilikuwa wazi. Hizo nafasi zilikuwa ni za kuziba.
 
Ndio maana nakwambia Ole asiondoke mpaka 2021.

Tutakapokuwa relegation zone ndo Glezers watapata akili.
 
Hapo kwa Lingard usiondoke kwanza.

Nioneshe umuhimu wa Lingard kiufundi.

Kumbuka ni no. 10 ambaye hana assist wala goli msimu huu.

Mlinganishe na Bruno mwenye goli 9 na assists 5. Ambaye Ole amemkataa akasema anapoteza mipira hovyo mara kwao kuna Obesity.
 
How do we impeach Ed Woodward?

He is a cancer and disaster pale United.
 
Mkuu Rashford ana miaka 21 Sasa bado Ni mtoto Sana then Unataka auzwe Rashford abaki Sanchez?

Rashford kafunga magoli 10 msimu uliopita na Sanchez kafunga 3 msimu mmoja na nusu Ila auzwe Rashford abaki Sanchez?

Hebu mkuu niambie Sanchez amefanya Nini man U kinachofanya kuondoka kwake kuwe Ni pigo kwetu? Maana nashangaa Sana Mashabiki wanaomponda Ole kwa kuondoka Sanchez. Mara Mia ya Lukaku angalau ana Good moments zake Ila sio Sanchez.

Na kusema James Ni mahututi mkuu kwa kutumia vigezo vipi?

Huyo pep anakuja Msimu wa kwanza alikuwa na magarasa yake vile vile kina Otamendi, bravo etc na alikuwa akiwapanga hivyo hivyo mpaka aliponunua wachezaji wake, unachofanya wewe Ni kumcompare kocha mwenye wachezaji zaidi ya 20 kikosi wenye sifa ya kucheza first 11 na Kocha ambae hata Hana wachezaji 11 wenye sifa ya first eleven.

Na ole anatengeneza mfumo wake sababu hakuna result mechi mbili tatu haimaanishi kwamba eti ni mfumo mbovu auache.
 
Misimu minne kama sio mitano kwa Rashford pale United. Uwezo wake ndio umefika mwisho, hana la ziada anaweza kukupa kamwe. Kama kina Tom Cleverley. Miaka 21 sio mtoto tena kwenye mpira wa miguu. Mchezaji anayepata chance kila mechi na bado anavurunda ni tatizo pia. Rashford sio standard ya United tena, hana quality tena. Angeuzwa wakati Barca wanamtaka.

Nimesema James ni bora kulinganisha na hao hohehae. Kama DeGea alivyokuwa mchezaji bora wa msimu for 2 or 3 years. Manake timu haina quality tena.

Ole alikuja katikati ya msimu, alishakuwa anayaona mapungufu ya timu mapema. Alikuwa na uwezo mkubwa sana wa kuuza wachezaji wabovu wote na kuleta wapya wa kufit kwenye kikosi chake.

Kumuuza Herera ni kosa kama kumuuza Lukaku. Kumuacha Young, Jones na Lingard ni makosa pia.

Kumbuka EPL ni ligi ngumu na kubwa kama Man Utd ilivyo timu kubwa. Muda wa majaribio akafanye akiwa Modle huko.

Kufanya majaribio ya formation mpya na haikupi matokeo ni matatizo pia. Hatuna huo muda wa kuendelea kusubiri.

Ni bora tuwe na formation ya kueleweka iwe identity ya United na sio kocha aje na majaribio ya formation yake.
 
Bruno Fernandez sio no 10 Ila Dybala ndio no 10, Bruno Ni kiungo wa kati Kama vile Mc tominay, Fred ama pogba. Hata angekuja Man U asingechukua no ya Lingard.

Kuhusu lingard mkuu tumeshaongea Sana comments zilizopita huko nitajaribu tu kupoint kiufupi kwa heshima yako.

-Lingard ndio top scorer wetu Wembley na makombe mawili ya Fa na Efl chini ya LVG na Mou yote tumeyapata kwa goli la ushindi la Huyu jamaa, sio hivyo tu hata nusu zake za Wembley kafunga.

-kama sijakosea Ni 2Nd top scorer wetu kwenye big matches against top 6 wenzetu.

Kwa hizo point mbili Hapo juu jamaa anahandle pressure vizuri kuliko wachezaji wetu wengi masuper star wanaopotea mechi kubwa.

Nilimfananisha Lingard na ji sung park, role yake kubwa Ni kutia pressure na kukaba juu kabla timu pinzani hawajafikia midfield yetu, park hakuwa akijulikana kwa assist Wala magoli, msimu mzima anaweza funga goli 4 tu. Tofauti ya kipindi kile Ni kwamba tuna Nani, park, Giggs etc wote wanaweza cheza eneo moja na wanapokezana kutokana na mechi inavyohitaji Ila Sasa tuna Lingard na Mata tu pamoja na Gomez ambaye bado haja blend 1st team.

Hivyo unapoangalia uchezaji wa lingard uziangalie tu magoli na assist angalia vitu Kama Hivi toka adebut man UTD

Kwa kazi anayopewa anaifanya vizuri ndio maana wote kina Mou, lvg, Moyes, Fergie, ole wanamkubali. Na sio kosa la lingard kutokuwa na mbadala wake, timu itafute no 10 mzuri acheze, yeye atatumika pale anapohitajika.
 
Hahahaaaaaa KAMA UNAJUA ,UNAJUA TU,
hata kama huna mpira unakuwa hatari thana....
Mapenzi tu

Ana hatari sana akiwa hana mpira kwa kukaba au? Lingard huyu huyu ambae mechi inaisha ana completed tackles sifuri

Labda wanamaanisha kujiposition
 
Mwenyewe binafsi huwa sielewi kwanini utd tunashindwa kutafuta no 10 wa uhakika.
Kuhusu swala la Jesse mi nakubaliana na ww kidogo kwamba jamaa japokuwa sio mzuri sana lakin ana moment zake na umuhimu wake hawa pale mwalimu anapotaka timu ikabie juu.
Baadae ya game ya Arsenal RVP alisema wachezaji wetu wa mbele mtu ambaye at least alikuwa anaji position sehemu sahihi ni J Lingz.
 
Mourinho alishindwa akatimuliwa huyo Conte mwenyewe attitude yake inaweza kuleta shida tu kwenye team.
Mourinho hakushindwa kinachomtokea sosha ndicho kilichowatokea moyes na van gaal dirisha la usajili lilikuwa waz miez mitatu unashindwa hata kufanya mbadala wa herrera maana yake timu inatafuta dili za kibiashara na mikataba minono uwanjani hawajali kama mkurugenz wa hii timu angekuwa makini basi leo timu ingekuwa mbali
 
Nakuelewa sana mkuu
 
Mkuu mbona mbishi sana ,mtu ambaye hana mpira anaassist vipi?ushaambiwa ni "HATARI AKIWA HANA MPIRA" labda hiyo sentensi hapo ulikuwa hujaielewa vema..
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…