Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Ishu sio Mchezaji wa kumfikia Pogba kiwango..ishu ni kuwa na midfield wanaofanya kazi yao ipasavyo,kuanzia kukaba kucreate magoli na kuipa timu balance..kwani timu zote zinazocheza vizuri zina Pogba kwenye middle zao??
Swali zuri sana. Na ni timu ngapi zenye viungo Wa kawaida na bado zinatu outshine na Pogba wetu?
 
dogo kaipandisha daraja Sheffield na ataibakisha this season uzoefu tu ndo anaohitaji.
 
halafu soko la jezi la United halipo Europe lipo Asia, mimi na wewe tutavaa jezi za mchezaji mwenye kiwango ila wao kuvaa jezi yenye jina la mtu fulani ni fahari kwao......Asia na mpira wapi na wapi???
Sasa ili mchezaji awe maarufu na watu kuwa na tension nae si lazima awe na uwezo Mkubwa na kuipa mafanikio timu yake? Mf. Juve walicheza na timu ya south Korea. Mashabiki wakajaa uwanjani kwa sababu waliambia CR7 atacheza kwa dk 45 na mwisho Wa siku jamaa hakucheza kabisa. Mashabiki wakaja juu sana kwa hasira na kuanza kuimba jina la Messi. So na wao wanajua kilicho bora kwenye mpira
 
Hivi bado jezi yake inanunuliwa kwa wingi? Basi wazungu nao ni machizi. Uwezo haonyeshi,anaicost timu,watu washaanza kumchukia sasa jezi hizo anauzaje ktk kiwango cha kuwa icon ya timu?
% kubwa ya mashabiki wa Utd wapo Asia, Africana North America.

Pogba lazima auze jezi kwasababu anapendwa bado.
 
Tumchukue Oblack.

Tumuuze DeGea Madrid.
 

Miongoni mwa wachezaji waliokuwa na uwezo mkubwa wa kudrible na kufunga tela mabeki wawili mpaka watatu katika Ubora wao ni Marc Overmarce, Zola, Giggs na kuna Kipara flani ivi akiitwa Paulo De Canio akichezea West Ham lakini hawakuwahi kuangaliwa kama ni wachezaji hatari zaidi katika ulimwengu wa Soka wa Wakati huo.
Kwahiyo dribbling ni added advantage tu lakini si kigezo cha ubora.
 
Manchester ilikuwaje bila De gea?

Walikuwa na Van Dar Sar mtu ambaye huwezi kujutia kuwa naye golini! Lakini leo ukiondosha De Gea basi makipa wa kuchezea Timu kama Manchester United ni 4 tu, waliobakia wote ni Vipurepure:-
1) Alisson
2) Ter Steven
3) Oblak
4) Ederson

Je kati ya hao 4 ni nani hapo unayewezea kumng'oa kiboyaboya? Jibu ni Mmoja tu kwa Njia moja tu! Naye ni Kuactivate release clause ya €100m ya Oblak.
 
Katika hao makipa uliowataja King

Binafsi naamini Terstegen & ederson ubora wa timu zao unawaongezea advantages kuwafanya wawe makipa bora .
 
Donaduma Gianlugi ni mzuri pia kwa kumuendeleza,anaweza kuja kuwa kipa bora sana.
 
Donaduma Gianlugi ni mzuri pia kwa kumuendeleza,anaweza kuja kuwa kipa bora sana.
Huyu dogo bado ni type ya kina kepa arizabalaga , Alipigiwa promo sana za kutaka kuuzwa bei kubwa na Wakala wake mino raiola ,
 
Upo sawa Mkuu, wapo akina Quaresma & Co.

Kuna tofauti kati wachezaji hatari, na wachezaji machachari
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…