Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Lukaku amebulk up

Lukaku wa Everton alikuwa na KG 93 haya sasa tunaambiwa sasa amefikisha KG 104 , kajazia minyama KG 11 kabisa
 
Shida sisi mashabiki muda mwingine tunakua tunaangalia mambo juujuu tu..
 
Rudiger >>>>>>Lindelof


Lindelof kiwango bado sana
 
Toka lini Scott McTominay awe level moja na Jorginho achilia mbali Kante, Ngolo?

Kante ambae anatembea na mpira na kupita katikati ya msitu wa wachezaji unamtafutia wa kumlinganisha nae dunia hii?
 
Kweli mafanikio ya Man United ni kuwa na followers wengi
Juventus imeizidi Man United kwa wafuasi katika mtandao wa Instagram. Tangu Ronaldo atue Juventus timu hiyo imeongeza wafuasi milioni 20 hivyo kufikisha Mil 31.1 na kuiacha United yenye wafuasi Mil 31. Ronaldo mwenyewe ana wafuasi Mil 181.
 
Hahaha eti akiwa hana mpira ni hatari zaidi.....kaka jiangalie kwenye kioo halafu sema mimi ni stupid
 
..
Natamani kweli jamaa atuambie hatari ya bila kua na mpira
Kwa watazamaji tu wa mpira hii ni ngumu sana kuielewa, lakini kwa wale wapenzi wa soka wanaoangalia soka kwa jicho la 3 wanaielewa vizuri hii

Ngoja nijaribu kukuelewesha

Miaka ya nyuma mchango wa mchezaji especially mchezaji wa mbele ulikuwa unaangaliwa zaidi pale mchezaji alipokuwa na mpira (hapa tunaongelea ku dribble, kutoa pasi, kufunga na kadhalika)

Miaka ya hivi karibuni Baada ya mpira kuwa na ufundi mwingi (hapa naongelea tactics na sio technics) movement za Wachezaji bila mpira zikaonekana ni muhimu kama zilivyo movement za mchezaji akiwa na mpira

Tunaposema mchango wa mchezaji bila mpira, hapa tunaongelea movement za mchezaji, sio kusimama sehemu moja kusubiri upewe pasi, kukimbia huku na kule ili umpe options nyingi mtoa pasi (Teamate wako mwenye mpira kwa wakati huo), kukimbia huku na kule ili uwachanganye mabeki wasijue wamkabe nani maana wakikufuata wewe pasi anapewa mchezaji mwingine na wakimkaba mwingine pasi unapewa wewe unafunga. Hapa ninaongelea timu kuwa DYNAMIC na sio PREDICTABLE.

Pia movement bila mpira inahusisha kukaba/pressing kuanzia juu/kwa wapinzani ambapo hii kazi sio kila mchezaji duniani anaiweza. Lakini movement bila mpira, kama umewahi kucheza mpira wa basketi utanielewa zaidi, unakuta mchezaji anakaa Njiani kimakusudi ili beki asipite kuzuia, na hii mbinu inatumiwa sana na Barca na City kwa sasa (mfano rahisi ni kama kona zinapopigwa halafu foward anakaa mbele ya kipa, sasa hii ipo hata mchezo unapoendelea katikati ya uwanjani) .

Tukirudi kwa Jesse, changamoto aliyonayo ni kutochangia sana timu yake ikiwa na mpira na kwenye hili anapaswa kurekebisha lakini kuna kazi kubwa sana anayoifanya bila mpira

Nicheke tena na mimi Mkuu
 
Umeelezea vizuri sana. Asipo kuelewa basi achana naye, usipoteze nguvu ya kumuelewesha.
 
Sidhani kama kuna mtu atakuwa hajakuelewa hapa..itakuwa ni kiburi tu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…