Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Kwa Mara ya iwanza ndani ya Miaka 7 tunafanya usajili ambao ndio right selection...... Bruno na dybala next......
 
Ukweli ni kwamba pamoja na uzuri wao hawamfikii Chris Smalling unless tuwe na chuki binafsi dhidi Smalling.
Kuna aina mbili za mabeki wa kati. Kuna beki kiongozi na Beki mpambanaji (Dog Fighter). Ili timu iwe vizuri inahitaji kuwa na mabeki wenye hizo sifa. Beki mpambanaji ana kazi ya kuhakikisha anashiriki katika kukaba hatari zote za mwanzo na beki kiongozi kazi yake ni kuziba pengo litakapojitokeza na kupanga timu. Rojo, Baily, Johns hawa ni mabeki wapambanaji hivyo ukiwapanga pamoja tegemea maumivu kwa kuwa wote watakimbilia kukaba na hakuna wa kuziba nafasi. Smalling ni beki kiongozi role yake ni tofauti kabisa na hao wengine.

Kwa sasa nafasi ya Beki mkabaji naona sio shida sana, msimu uliopita Victor Lind. amenesha kuimudu hiyo nafasi kwa sasa tunahitaji sana beki kiongozi. Kuja kwa Maguire kutasaidia kuimarisha ulinzi. Kinachohitajika zaidi ni kuwa na namba 6 mwenye uwezo wa kukaba kwa kutumia nguvu na akili. Kule mbele sio shida kuna hitaji kocha kuwa mkali watu wasilete utoto golini
 
Dalot kasajiliwa kama Beki 2 lakini yule dogo naona kama ana uwezo wa kucheza position nyingi ikiwemo winga kwa kuwa ana uwezo wa kumiliki mpira. Kwa kuwa yupo AWB beki 2 ni vyema kocha aangalie nafasi nyingi ya kumtumia Dalot kwa baadhi ya mechi dogo ana potential kubwa sana
 
Dalot kasajiliwa kama Beki 2 lakini yule dogo naona kama ana uwezo wa kucheza position nyingi ikiwemo winga kwa kuwa ana uwezo wa kumiliki mpira. Kwa kuwa yupo AWB beki 2 ni vyema kocha aangalie nafasi nyingi ya kumtumia Dalot kwa baadhi ya mechi dogo ana potential kubwa sana
Ameshalisema hili kuwa Dalot atapewa majukumu mengine uwanjani ukizingatia his versatility.
 
Rashford akiacha utoto na Martial akaacha ubishoo ni madogo hatari sana wana uwezo mkubwa sana wa kucheza kama wings au washambuliaji wa kati. Inabidi kocha awe mkali sana na wapatiwe ushauri
 
Back
Top Bottom