fuentte
JF-Expert Member
- Jul 30, 2015
- 3,210
- 9,206
Mwanzo nilianza kumuamini Ogs kuwa anajaribu kuijenga manchester mpya kwa kuwaamini vijana wadogo wenye vipaji. Lakini cha kushangaza targets zake unamkuta mtu kama Dier ambaye bench la spurs linajua rangi ya boxer yake.Hapa ndiyo ninapoleta mjadala kuhusu nani wa kulaumiwa kwenye usajili! Je ni Ed? au Ole?
Nakumbuka Liverpool tukiwa na Matajiri hawahawa (FSG) tulionao Makocha waliopita Hodgson, Dalglish na Rodgers walikuwa wskitusainia wachezaji aina ya Henderson, Downing, Allen, Spearing, Charlie Adams, Lallana, Kolo Toure, Lovren na Wapumbavu wengi tu wa Calibre ya hao ambao ni average na wa bei za kununua Nyanya.
Lakini tukiwa na Matajiri hawahawa FSG chini ya Kocha Klopp tunasaini wachezaji wa aina ya Mane, Salah, Allison, Fabinho na VVD ambao ni talented bei zao zinaendana na Soko.
Sasa hapo je tatizo ni Tajiri, CEO, Makocha au Scout teams zinakuwa na udhaifu katika kuidentify Targets sahihi?
Ni wazi kuwa Scout team pamoja na Kocha hawapo vizuri ndiyo sababu ya kusajili failure signings.
Nadhani kuna namna hawa walimu wanaoomba ajira huwa wanaahidi kufanya makubwa kwa bajeti ndogo.