Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Manchester United (Red Devils) | Special Thread

dah! hii heshima ulionipa ni nzito kuliko ndevu za lionel messi.
ujio wa pochettino na faida zake kwa mtazamo wangu.
  • ana uzoefu na ni muumini wa mpira wa kisasa ambao tumekuwa tukiulilia kwa muda mrefu
  • ni muumini wa kuwapa nafasi wachezaji vijana na hili tumelishuhudia kwa wachezaji tofauti.
  • ana rekodi nzuri sana kwenye suala la kusajili wachezaji, ukiangalia wachezaji wengi aliowasajili tokea yupo southampton hadi tottenham hotspurs wameendelea kufanya vizuri na wengi wao ni wale aliyowasajili kwa fedha chache.
athari yake kubwa ninayoiona ni kurudi tena kwenye zama za kuachana na falsafa, misingi na utamaduni wa klabu iliojengwa miaka mingi iliopita, naamini kama pochettino atawasili msimu ujao hatopendelea kuchaguliwa benchi lake la ufundi hivyo basi atakuja na timu yake ya ufundi, inamaana tutaanza tena upya kama alivyofanya david moyes, LVG na jose mourinho.
halafu pia siamini kama pochettino atadumu kwa muda mrefu klabuni bila ya kuwa na fikra za kurudi tena spain kufundisha

kwa uoni wangu sioni dalili yoyote ya kuondolewa ole gunnar solskjaer mwishoni mwa msimu hata kama atashindwa kupata nafasi ya nne, kuna nguvu tatu zina mlinda kwa sasa ambazo ni legends aliocheza nao kwa mafanikio makubwa, waliyopendekeza apewe nafasi baada ya kuona jahazi linazama na nguvu ya mwisho ni ya mashabiki wale wa karne ya 20 ambao bado wanaendelea kumuona ni shujaa aliyetakasika kwa kile alichokifanya pale nou camp.

silaha yake nyengine kubwa aliyokuja nayo ni kurudisha utamaduni wa manchester united wa kucheza mpira wenye kueleweka, makocha waliopita kila mmoja alikuja na falsafa yake isiyoendana na damu ya manchester united, wakati wa jose mourinho tulishinda mechi nyingi sana chini yake kuliko mwalimu yoyote yule lakini nidhamu yetu ya ushindi ilikuwa ni ya kiwango cha chini sana.
hata ukiangalia benchi lake la ufundi ni uthibitisho tosha jinsi gani klabu imeshajiandaa kuishi na OGS kwa sababu limejaza watu wanaoendana na utamaduni wa manchester united, siamini kama ujio wa mike phelan ni kwa muda wa miezi sita tu halafu atafute mlango wa kutokea.

kama ishu ni kuwapa nafasi majina makubwa basi klabu tayari imeshapitia hatua hiyo lakini bado tuko pale pale, ukiangalia upande wa pili imemchukua miaka mitatu jurgen klopp kuifikisha liverpool hatua iliopo muda huu cha umuhimu ni kuwepo uaminifu.

Solskjaer, Phelan, Karrick na McKenna ni timu ambayo inahitaji kutafutiwa mwanadamu mwenye uelewa mkubwa wa soka la kisasa na hii ndio kazi ya kwanza anayopaswa aifanye ed woodward.
nasubiria majibu yake siku ya jumapili baada ya kupoteza alama mbili kwa mara ya kwanza tokea awe mwalimu wetu, leicester city ni kipimo chengine cha ukweli.

kuna mlevi mwenzangu ameniuliza hapa hivi ole gunnar solskjaer aliikuta manchester united ikiwa nafasi ya nne?
Shukrani sana mkuu nadhani hatutofautiani sana kimawazo, akipatikana director of football bora basi team hakika utafanya development kubwa kwa misimu mitatu ijayo tungojee tuone hatma ya suala hili la director of football inaishia wapi

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Thanks for the memories Fellaini

1. United vs Cristal Palace, May 2015
Goli la big Fella liliihakikishia Man United kucheza UCL katika msimu uliofuata

2. United vs Everton, April 2016
Goli la Big Fella liliitoa timu yake ya zamani katika nusu fainali ya FA na United walipata fursa ya kushinda kombe la kwanza tangu SAF aondoke United katika fainali ya FA mwaka huo

3. United vs Hull City, January 2017
Big Fella alifunga goli katika nusu fainali na hilo goli liliivusha United hatua ya nusu fainali na kufika fainali ambayo United alifanikiwa kuchukua kombe la Ligi ambalo lilikuwa ni kombe la pili katika zama za post SAF

4. United vs Celta Vigo, April 2017
Hii ni nusu fainali iliyodhihirisha kwamba Big Fella akifunga goli la ushindi katika Semi final lazima United achukue kombe husika. Goli muhimu lilichangia United kuchukua kombe la Europa ambalo United hawakuwahi kulibeba miaka ya nyuma.

5. United vs Arsenal, May 2018
Maruane alimuhakikishia Wenger kama kocha wa Arsenal kichapo katika mechi yake ya mwisho pale OT. Not a bad way to say goodbye to Mr. Wenger?

6. United vs Young Boys, Novemba 2018
Goli muhimu lililoivusha United kwenda hatua ya mtoano. Goli hili liliifanya United isitegemee mechi ya mwisho (ambayo United alipigwa na Valencia) ili kuvuka hatua ya makundi.

Japo aligawanya mtazamo wa mashabiki kuhusu uwepo katika club ya United, lakini naamini big Fella alikuwa ni kisu kilichookoa maisha ya komando pindi bunduki yake ilipoishiwa risasi.

THANKS BIG FELLA, BEST LUCK HUKO UENDAKO
skysports___BtWDvqvApX____.jpg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Uncle Gonzalo Higuain 65 minutes against ORDINARY BOURNEMOUTH
0 shot on target
0 dribbles
0 key Passes
20 bottles water sucked
100 misplaced passes
200 sneezing
Perfect replacement for ALVARO MORATA
 
kesho ni must win game ,


And please City shinda mechi hizo mbili (vs arsenal &Chelsea), halafu sisi tutafanya kitu Feb 24(vs Liverpool).

'Nina wasiwasi na huyu city kwenye hizi mechi mbili, Mara huyo kapigwa na arsenal.'

ANYWAY hebu tushinde mechi zetu kwanza. Let's go OLE's ARMY.
 
Back
Top Bottom