Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Happy Independence Day
  1. uhuru kwa andreas perreira kutoka namba 6 hadi namba 11 japokuwa alichezeshwa kwa dakika 7, ni matumaini yangu benchi la ufundi litaendelea kumtumia kama kiungo mshambuliaji.
  2. uhuru kwa walinzi wetu wa kati angalau jana walifanikiwa kupumzika, unapolinda kwa njia ya kushambulia hata kama beki wako wa kati ni Damushin basi ataonekana hodari kuliko thiago silva wa AC MILAN.
  3. uhuru kwa benchi la ufundi, inaonekana dhahiri michael carrick na mwenzake mckenna walikuwa hawafurahishwi na kitendo cha jose mourinho kumchezesha andreas perreira kiungo mkabaji, ni ngumu kuamini kama yale mabadiliko aliyafanya solskjaer haliyakuwa mechi za manchester united alikuwa hazifuatilii kwa kiwango cha standard gauge.
  4. kwa mara ya kwanza nimeshuhudia kocha wetu akiingia uwanjani kuwapongeza wachezaji wake na kwa mara ya kwanza nimeshuhudia kocha akiwasifia wachezaji na si kujibebesha sifa yeye kwa asilimia kubwa.
  5. ngoja nicheke kwanza : kwa mara ya kwanza muheshimiwa radika na timu yake wanazungumza lugha moja na muheshimiwa Daud1990 na timu yake
  6. nilishazoea kuangalia mechi ya manchester united tukicheza dakika 30 bila ya kupiga shuti goli la wapinzani lakini jana ilikuwa ni tofauti, tumepiga mashuti 17 na mashuti 9 yalilenga goli.
  7. kuna tofauti kubwa kati ya kumiliki mpira bila ya kufanya chochote na kumiliki mpira huku timu ikionyesha harakati za kutafuta magoli, nyakati za van gaal tulikuwa tunamiliki mpira kuliko AJAX lakini baada ya dakika 90 tunapata suluhu. Jana timu ilimiliki mpira 74% na timu ilionyesha harakati za kutafuta magoli.
  8. dah! namuonea huruma sana fred, kwa mpira huu wa kugusa mara moja unamfaa sana lakini wapinzani wake nao pia ni wabaya sana, ni matumaini yangu uhuru wa jana utaturudishia rotation kama ilivyokuwa nyakati za fergie

ni mjinga peke yake ndiye atakayekuwa na matumaini ya kwamba tutashinda kila siku, kwangu mimi haiwezekani kwa sababu mpira una matokeo matatu. Tulichokuwa tunakitaka mashabiki wa manchester united chini ya jose mourinho ni mpira wenye kueleweka ambao utatoa uhuru kwa wachezaji kujisikia furaha kufanya kazi walioichagua maishani mwao, na hata kama itatokezea tupo nyuma kwa magoli dhidi ya wapinzani wetu basi ionekane morali ya kutafuta ushindi na si kudhalililishwa na wapinzani wetu kama walivyotufanyia liverpool na manchester city.

wanasema tumewafunga cardiff FC, ok wapo sahihi na tunawashukuru wapinzani kwa kutukumbusha ya kwamba tumeifunga timu iliyo nafasi ya nne kutoka chini na ni matumaini yangu familia ya manchester united haitabweteka na ushindi tulioupata jana bali itakuwa ni chanzo cha kuendeleza wimbi la ushindi dhidi ya huddlesfield town siku ya jumatano.
Kinachonikera ni kwamba jose mourinho ameiacha timu tukiwa nyuma kwa pointi 11 dhidi ya wapinzani wetu watatu ambao wanawania nafasi 4 za juu kama sisi, kama tungeliweza kumfukuza jose mourinho mechi dhidi ya west ham united basi muda huu tungelikuwa tunawania nafasi ya 3, cha ajabu jose mourinho ameondoka na fedha zetu na pia anaelekea kuondoka na nafasi yetu ya 4.
1545524590905.png

wapinzani wetu muda huu baada ya ole gunnar solskjaer kuingizwa dakika za majeruhi, cha ajabu wametupita kwa point nyingi lakini wameanza kuweweseka kama mzee wa ujasiriamali, sijui kwa kiingilishi linatamkwa vipi kiutani.
 
Mkuu ukiona mtu analalamika clean sheet na hata kumponda Paul kuwa useless basi ujue upro mourinho unamsumbua na haamini kuwa mourinho katimuliwa
Hayo ni mawazo yako, na ninayaheshimu

Timu zote zinapata mafanikio ya kubeba ndoo, defensively lazima wawe solid

Angalia Leicester iliyochukua kombe 2016

Angalia Manchester City iliyochukua kombe 2017/2018

Angalia Liverpool ya msimu uliopita ilifunga sana lakini ikaruhusu sana kufungwa, na ikaishia kuwa msindikizaji

Angalia Liverpool ya mwaka huu, ina clean sheet zakutosha na angalia ilipo kwenye msimamo wa ligi

Wewe endelea kukariri tu kuwa Mourinho ndio alikuwa anapenda ulinzi imara, kila kocha mwenye kutaka makombe anataka ulinzi imara
 
Happy Independence Day
  1. uhuru kwa andreas perreira kutoka namba 6 hadi namba 11 japokuwa alichezeshwa kwa dakika 7, ni matumaini yangu benchi la ufundi litaendelea kumtumia kama kiungo mshambuliaji.
  2. uhuru kwa walinzi wetu wa kati angalau jana walifanikiwa kupumzika, unapolinda kwa njia ya kushambulia hata kama beki wako wa kati ni Damushin basi ataonekana hodari kuliko thiago silva wa AC MILAN.
  3. uhuru kwa benchi la ufundi, inaonekana dhahiri michael carrick na mwenzake mckenna walikuwa hawafurahishwi na kitendo cha jose mourinho kumchezesha andreas perreira kiungo mkabaji, ni ngumu kuamini kama yale mabadiliko aliyafanya solskjaer haliyakuwa mechi za manchester united alikuwa hazifuatilii kwa kiwango cha standard gauge.
  4. kwa mara ya kwanza nimeshuhudia kocha wetu akiingia uwanjani kuwapongeza wachezaji wake na kwa mara ya kwanza nimeshuhudia kocha akiwasifia wachezaji na si kujibebesha sifa yeye kwa asilimia kubwa.
  5. ngoja nicheke kwanza : kwa mara ya kwanza muheshimiwa radika na timu yake wanazungumza lugha moja na muheshimiwa Daud1990 na timu yake
  6. nilishazoea kuangalia mechi ya manchester united tukicheza dakika 30 bila ya kupiga shuti goli la wapinzani lakini jana ilikuwa ni tofauti, tumepiga mashuti 17 na mashuti 9 yalilenga goli.
  7. kuna tofauti kubwa kati ya kumiliki mpira bila ya kufanya chochote na kumiliki mpira huku timu ikionyesha harakati za kutafuta magoli, nyakati za van gaal tulikuwa tunamiliki mpira kuliko AJAX lakini baada ya dakika 90 tunapata suluhu. Jana timu ilimiliki mpira 74% na timu ilionyesha harakati za kutafuta magoli.
  8. dah! namuonea huruma sana fred, kwa mpira huu wa kugusa mara moja unamfaa sana lakini wapinzani wake nao pia ni wabaya sana, ni matumaini yangu uhuru wa jana utaturudishia rotation kama ilivyokuwa nyakati za fergie

ni mjinga peke yake ndiye atakayekuwa na matumaini ya kwamba tutashinda kila siku, kwangu mimi haiwezekani kwa sababu mpira una matokeo matatu. Tulichokuwa tunakitaka mashabiki wa manchester united chini ya jose mourinho ni mpira wenye kueleweka ambao utatoa uhuru kwa wachezaji kujisikia furaha kufanya kazi walioichagua maishani mwao, na hata kama itatokezea tupo nyuma kwa magoli dhidi ya wapinzani wetu basi ionekane morali ya kutafuta ushindi na si kudhalililishwa na wapinzani wetu kama walivyotufanyia liverpool na manchester city.

wanasema tumewafunga cardiff FC, ok wapo sahihi na tunawashukuru wapinzani kwa kutukumbusha ya kwamba tumeifunga timu iliyo nafasi ya nne kutoka chini na ni matumaini yangu familia ya manchester united haitabweteka na ushindi tulioupata jana bali itakuwa ni chanzo cha kuendeleza wimbi la ushindi dhidi ya huddlesfield town siku ya jumatano.
Kinachonikera ni kwamba jose mourinho ameiacha timu tukiwa nyuma kwa pointi 11 dhidi ya wapinzani wetu watatu ambao wanawania nafasi 4 za juu kama sisi, kama tungeliweza kumfukuza jose mourinho mechi dhidi ya west ham united basi muda huu tungelikuwa tunawania nafasi ya 3, cha ajabu jose mourinho ameondoka na fedha zetu na pia anaelekea kuondoka na nafasi yetu ya 4.
View attachment 975482
wapinzani wetu muda huu baada ya ole gunnar solskjaer kuingizwa dakika za majeruhi, cha ajabu wametupita kwa point nyingi lakini wameanza kuweweseka kama mzee wa ujasiriamali, sijui kwa kiingilishi linatamkwa vipi kiutani.
Chief hapo kwa Fred sijakuelewa kabisa ulikuwa unamaanisha nini hasa?
 
Sijui kuhusu united fans wengine ila wengi wetu humu tumefurahishwa na aina ya uchezaji wa timu zaidi kuliko idadi ya magoli. Mpira saffi ukisindikizwa na matokeo mwanana,hapo lazima usahau shida zako kwa muda kidogo ufurahie maisha.
Tulitamani kuona uchezaji wa aina hii ambapo wachezaji wanatembea lakini wanauamrisha mpira kutii uelekeo tofauti tofauti nao unatii. We fikiria Jana nimeshuhudia Ashley young anapiga no look pass tena kwa kisigino!
Thanks ogs,you brought the united we once lost!!!!
Kwa upande wangu uko sahihi asilimia zote
 
Sina Shaka na Lukaku, ni goal Score mzuri Mno ingawa ana mapungufu yake hasa Katika umilikaji wa Mpira.

Lukaku ni mmaliziaji wa Kazi kubwa inayofanywa na viungo.

Man United ya Mourihno ilikosa Ubunifu Katika eneo la kiungo cha Juu kutokana na mifumo na Maelekezo ya Kocha.

Ni imani yangu kutokana na Mabadiliko ya Kocha na Benchi la Ufundi Lukaku atarudi Katika zama zake, anahitaji kuaminiwa na kupewa Nafasi.

Kwa United Tatizo halikuwa wachezaji, Tatizo lilikuwa Kocha.

Mourihno alishindwa kufaidika na wachezaji ama alishindwa kuwatumia wachezaji alionao Katika kupata Matokeo chanya.

Mifumo yake haikuwafanya wachezaji kuwa huru, alilazimisha wachezaji wote kuwa na uwezo wa kukaba Muda wote.

Ndio mana hata alipokuja Sanchez baada ya michezo kadhaa alianza kulalamika Mbinu za Kocha na Majukumu tofauti na uwezo wake anayopewa uwanajani.

Nadhani Kazi kubwa ya Ole Sasa Ni kuwarudisha wachezaji mchezoni na kila Mmoja kujituma Katika eneo lake.
Jana amempa nafasi Matic, I hope umekubaliana na uamuzi wake

Mimi naamini hata Lukaku ni striker mzuri, amedhihirisha hivyo akiwa timu nyingine
 
Nakubaliana nawe, Kama tunakubaliana kucheza soka la kushambulia tunatakiwa kuwa na Beki Nzuri mno, Kikosi Chetu tuna Tatizo Katika Beki.

2. Young/Valencia umri umeshawakimbia
3. Shaw sio wa kumtegemea sana kutokana na majeruhi yake ya Mar a kwa Mara ingawa nakiri ni moja ya wachezaji wa Kiingereza wenye vipaji

Tuna Tatizo hasa Katika Beki namba 4 na 5, Lendlof ni mzuri hasa timu inaposhambulia lakini anakosa umakini timu inaposhambuliwa anahitaji kujenngwa zaidi.

Johnes Naye si Beki wa uhakika kutokana na majeruhi na Kiwango Chake kuwa cha kupanda na kushuka na si Beki mzuri kwa timu inayopenda kushambulia Muda wote.

Baily kuna Shida either ni Mou alishindwa kumtumia ama Mfumo ule wa kukaba Muda wote umemchosha mapema, Ana tatizo la kuzuia Mipira ya juu kutokana na kimo Chake.

Huwa nafikiria Baily aanze kuandaliwa kucheza Beki namba 2 Kama Mbadala wa Valencia/Young timu ikiwa inatafuta Beki namba 2 wa uhakika.

Kwenye eneo la Kiungo sina Shida hata Kidogo, Man United ni moja ya timu yenye viungo wazuri duniani hasa kiungo cha Chini.

Herera + Matic Kama timu tunatakiwa kuizoea Hii combination mapema sana, Mou alituchelewesha sana.

Juu ya Matic na Hererra anacheza Pogba.

Herera+Matic+Pogba wanakupa vitu vingi zaidi Katika eneo la Kiungo, timu inaposhambuliwa Herera na Matic wanashuka kuzuia na timu inaposhambulia Herrera na Pogba wanapanda kushambulia na kutengeneza pasi za mwisho Kama si kufunga kabisa.

Kwangu namba Tisa tuendelee kumuamini Lukaku/Rashford inategemea na Match.

Namba 10 tuendelee kumpa nafasi Martial ambaye huwa mzuri zaidi anapokuwa nyuma ya mshambuliaji.

Wings Lingard+ Sanchez.

Kuanza kwa Lingard na Rashford kutategemea na aina ya match.

Ila tunahitaji mshambuliaji Mmoja zaidi wa katikati kupatA Magoli Mengi zaidi.
Ball playing defender, makocha wengi wanaopenda mpira wa kushambulia wanawahusudu sana ma ball playing defenders na ball playing goal keepers

Inaonekana dogo amepewa ruhusa ya kupanda kwa kuwa ana uwezo wa kuufanyia mpira jambo kwa maslahi ya timu

Lakini kwa uchezaji huu, clean sheet zitakuwa chache, lakini yote heri cha msingi ushindi
 
Hayo ni mawazo yako, na ninayaheshimu

Timu zote zinapata mafanikio ya kubeba ndoo, defensively lazima wawe solid

Angalia Leicester iliyochukua kombe 2016

Angalia Manchester City iliyochukua kombe 2017/2018

Angalia Liverpool ya msimu uliopita ilifunga sana lakini ikaruhusu sana kufungwa, na ikaishia kuwa msindikizaji

Angalia Liverpool ya mwaka huu, ina clean sheet zakutosha na angalia ilipo kwenye msimamo wa ligi

Wewe endelea kukariri tu kuwa Mourinho ndio alikuwa anapenda ulinzi imara, kila kocha mwenye kutaka makombe anataka ulinzi imara
huu ni msimu wa tatu kipa wa tiko tiko ndo anakuwa kipa mwenye klin shit nyingi kuanzia la liga mpaka ulaya nzima kwa msimu anaondok na klin shit 23+ lakini makombe wanachukua Barca

nadhani wewe ndo umekariri
 
Happy Independence Day
  1. uhuru kwa andreas perreira kutoka namba 6 hadi namba 11 japokuwa alichezeshwa kwa dakika 7, ni matumaini yangu benchi la ufundi litaendelea kumtumia kama kiungo mshambuliaji.
  2. uhuru kwa walinzi wetu wa kati angalau jana walifanikiwa kupumzika, unapolinda kwa njia ya kushambulia hata kama beki wako wa kati ni Damushin basi ataonekana hodari kuliko thiago silva wa AC MILAN.
  3. uhuru kwa benchi la ufundi, inaonekana dhahiri michael carrick na mwenzake mckenna walikuwa hawafurahishwi na kitendo cha jose mourinho kumchezesha andreas perreira kiungo mkabaji, ni ngumu kuamini kama yale mabadiliko aliyafanya solskjaer haliyakuwa mechi za manchester united alikuwa hazifuatilii kwa kiwango cha standard gauge.
  4. kwa mara ya kwanza nimeshuhudia kocha wetu akiingia uwanjani kuwapongeza wachezaji wake na kwa mara ya kwanza nimeshuhudia kocha akiwasifia wachezaji na si kujibebesha sifa yeye kwa asilimia kubwa.
  5. ngoja nicheke kwanza : kwa mara ya kwanza muheshimiwa radika na timu yake wanazungumza lugha moja na muheshimiwa Daud1990 na timu yake
  6. nilishazoea kuangalia mechi ya manchester united tukicheza dakika 30 bila ya kupiga shuti goli la wapinzani lakini jana ilikuwa ni tofauti, tumepiga mashuti 17 na mashuti 9 yalilenga goli.
  7. kuna tofauti kubwa kati ya kumiliki mpira bila ya kufanya chochote na kumiliki mpira huku timu ikionyesha harakati za kutafuta magoli, nyakati za van gaal tulikuwa tunamiliki mpira kuliko AJAX lakini baada ya dakika 90 tunapata suluhu. Jana timu ilimiliki mpira 74% na timu ilionyesha harakati za kutafuta magoli.
  8. dah! namuonea huruma sana fred, kwa mpira huu wa kugusa mara moja unamfaa sana lakini wapinzani wake nao pia ni wabaya sana, ni matumaini yangu uhuru wa jana utaturudishia rotation kama ilivyokuwa nyakati za fergie

ni mjinga peke yake ndiye atakayekuwa na matumaini ya kwamba tutashinda kila siku, kwangu mimi haiwezekani kwa sababu mpira una matokeo matatu. Tulichokuwa tunakitaka mashabiki wa manchester united chini ya jose mourinho ni mpira wenye kueleweka ambao utatoa uhuru kwa wachezaji kujisikia furaha kufanya kazi walioichagua maishani mwao, na hata kama itatokezea tupo nyuma kwa magoli dhidi ya wapinzani wetu basi ionekane morali ya kutafuta ushindi na si kudhalililishwa na wapinzani wetu kama walivyotufanyia liverpool na manchester city.

wanasema tumewafunga cardiff FC, ok wapo sahihi na tunawashukuru wapinzani kwa kutukumbusha ya kwamba tumeifunga timu iliyo nafasi ya nne kutoka chini na ni matumaini yangu familia ya manchester united haitabweteka na ushindi tulioupata jana bali itakuwa ni chanzo cha kuendeleza wimbi la ushindi dhidi ya huddlesfield town siku ya jumatano.
Kinachonikera ni kwamba jose mourinho ameiacha timu tukiwa nyuma kwa pointi 11 dhidi ya wapinzani wetu watatu ambao wanawania nafasi 4 za juu kama sisi, kama tungeliweza kumfukuza jose mourinho mechi dhidi ya west ham united basi muda huu tungelikuwa tunawania nafasi ya 3, cha ajabu jose mourinho ameondoka na fedha zetu na pia anaelekea kuondoka na nafasi yetu ya 4.
View attachment 975482
wapinzani wetu muda huu baada ya ole gunnar solskjaer kuingizwa dakika za majeruhi, cha ajabu wametupita kwa point nyingi lakini wameanza kuweweseka kama mzee wa ujasiriamali, sijui kwa kiingilishi linatamkwa vipi kiutani.



Mkuu hongera Sana kwa Uzi murua. Umemaliza kila kitu.


GGMU
 
Nitajie mechi ambayo Mourinho aliongoza team kushinda magoli matano.

Ukinitajia hiyo mechi naihama Manchester nakuwa shabiki mnazi wa Burnley
Man U 5 na 2 Dortmund under Mourinho's coaching, download afu ole wako usijitekenye afu nisikukute hapa Jamii Forum kumbe umebadili tu ID ya kale na kutumia nyingine mpya.

Download kwenye youtube afu uje na majibu na kuhama jumla jumla Man U
 
Back
Top Bottom