Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Lukaku anafit kwenye hii timu kweli??...why tusimwamini hata sanchez upfront??

Binafsi siioni nafasi yake,lakini ngoja tuone kocha akimpa nafasi atafanya nini??
Jana amempa nafasi Matic, I hope umekubaliana na uamuzi wake

Mimi naamini hata Lukaku ni striker mzuri, amedhihirisha hivyo akiwa timu nyingine
 
Swali la kizushi: Wadau Hii vice versa ya Man U sijui ilikuwaje. Ole alikuwa mwanafunzi Wa Ferguson na Phelani sasa hivi wamempa Ole jukumu la kuwa Mwalimu Mkuu na msaidizi wake ni phelan. Kwa nini Phelan asingepewa nafasi ya Ole halafu nafasi ya Phelan akapewa Ole?
Mkuu umewahi kuona kwenye nchi, mtu aliyekuwa Naibu Waziri wizara flani,moja kwa moja akapandishwa akiwa PM, na wale waliokuwa mawaziri kamili wengine wakabaki kuwa wabunge tu au kuwa mawaziri wa kawaida?

Au Mwalimu baadae akawa chini ya Afisa Elimu ambaye aliwa kufundishwa naye?

Hilo ndio jibu fikirishi
 
Smalling akiwa Mkuu na de gea msaidizi siyo mbaya. Shida ya De gea na Valencia naona siyo waongeaji ni wapole sana
Captain materials

1. Ander Herrera, ana hamasa, ana uchungu na timu na mfia timu

2. Ashley Young, ni short term solution

3. Chriss Smalling, ni mpambanaji, anaijua United tangu na tangu. Tatizo mbele ya safari anaweza asiwe first teamer

4. Paul Pogba is just a mescenary, hafai, mbinafsi

5. Valencia, nadhani hata kuongea kingereza kwake ni tatizo

6. Degea, fantastic player, fantastic goal keeper, lakini sio kila fantastic player can be a fantastic leader
 
Yaani Leo hadi lindelof alikuwa anapanda na kutoa assist kama kiungo mchezeshaji. Phil Jones alipiga shuti ndani ya 18 kipa akadaka duu!
Ball playing defender, makocha wengi wanaopenda mpira wa kushambulia wanawahusudu sana ma ball playing defenders na ball playing goal keepers

Inaonekana dogo amepewa ruhusa ya kupanda kwa kuwa ana uwezo wa kuufanyia mpira jambo kwa maslahi ya timu

Lakini kwa uchezaji huu, clean sheet zitakuwa chache, lakini yote heri cha msingi ushindi
 
Chelsea, Arsenal, Liverpool na Baadhi ya Washabiki Wa Man United (Pro-Mourinho) tulishirikiana kueka Kambi hapa.

Sasa Ni Muda Wa Kushirikiana kivyengine kuhamishia Maturubali Darajani kule London kwa Mr. Masigara.

😀😀😀
Hahaha hahahaha






Ndio maana presha ilikuwa kubwa Mou abaki kumbe ilikuwa combination ya hatari.
 
Mkuu umewahi kuona kwenye nchi, mtu aliyekuwa Naibu Waziri wizara flani,moja kwa moja akapandishwa akiwa PM, na wale waliokuwa mawaziri kamili wengine wakabaki kuwa wabunge tu au kuwa mawaziri wa kawaida?

Au Mwalimu baadae akawa chini ya Afisa Elimu ambaye aliwa kufundishwa naye?

Hilo ndio jibu fikirishi
Nadhani Majaliwa alitoka kuwa naibu Waziri, na moja kwa moja kuwa PM.
 
Ball playing defender, makocha wengi wanaopenda mpira wa kushambulia wanawahusudu sana ma ball playing defenders na ball playing goal keepers

Inaonekana dogo amepewa ruhusa ya kupanda kwa kuwa ana uwezo wa kuufanyia mpira jambo kwa maslahi ya timu

Lakini kwa uchezaji huu, clean sheet zitakuwa chache, lakini yote heri cha msingi ushindi
clean sheets sio tatizo kwa sababu hakuna kombe la clean sheet its like an individual prize

ila goli nyingi zinafanya ukachukue kombe
1st game 0-0
2nd game 0-0
3rd game 0-0
three matches three points three clean sheets

1st game 5-1
2nd game 3-1
3rd game 4-2
three matches nine points

bila shaka umeona utofauti hapo
 
Kubadilishwa mwl aliyekosa matokeo mazuri huwa kunabadilisha saikolojia na morali ya wachezaji. Bila hata kocha wanaweza kuonekana wameimprove in short term but in long term, things may turn as usual. Kwa hiyo hutegemea analysis ya wataalam kuona km kocha anaweza kuwa na consistency in longterm
Umeneno vizuri sana mkuu
 
Mimi Ni mmoja ambaye Nimeumia Sana Kufukuzwa Mourinho! Musinishangae ila Kumbukeni kuwa "Adui Muombee Njaa"..

Na Njaa kubwa niliyokuwa nikiwaombea nikuwa Mourinho aogezewe Mkataba ili muzidi kupata Maumivu 😀😀😀

Kwa Upande Wa Wa Pili Nimefurahi Sana Kuteuliwa Mshabiki Nguli, Mshabiki lialia, Mshabiki Kindakindaki, Mshabiki Mkereketwa, Mshabiki Halisi Wa LIVERPOOL FC kamanda Ole Gunnar Solskjaer Kuwa Manager Wa Man United.

OGS Ni Boyhood Fan Wa Liverpool
Mkuu mtu anaweza kuwa boyhood fan, lakini baadae akabadilika baada ya kucheza timu flani kwa muda mrefu

Mfano hata OGS juzi ame declare he is United fan
 
IMG_3066.JPG


Tupate maneno ya wadhamini wetu
 
Najua hilo! Angelikuwa yupo Simba au Yanga ningelihesabu vyengine
Ulimboka Mwakingwe alikuwa mshabiki wa Yanga akiishi pale Mzumbe, akichezea timu ya Chui alijulikana hivyo kwa sasa sina uhakika bado ni Yanga damu
 
clean sheets sio tatizo kwa sababu hakuna kombe la clean sheet its like an individual prize

ila goli nyingi zinafanya ukachukue kombe
1st game 0-0
2nd game 0-0
3rd game 0-0
three matches three points three clean sheets

1st game 5-1
2nd game 3-1
3rd game 4-2
three matches nine points

bila shaka umeona utofauti hapo
Ninafahamu, rejea sentence yangu ya mwisho

Lakini ushindi wa clean sheet unanoga kuliko ushindi wa "dirt sheet"
 
clean sheets sio tatizo kwa sababu hakuna kombe la clean sheet its like an individual prize

ila goli nyingi zinafanya ukachukue kombe
1st game 0-0
2nd game 0-0
3rd game 0-0
three matches three points three clean sheets

1st game 5-1
2nd game 3-1
3rd game 4-2
three matches nine points

bila shaka umeona utofauti hapo
Mkuu ukiona mtu analalamika clean sheet na hata kumponda Paul kuwa useless basi ujue upro mourinho unamsumbua na haamini kuwa mourinho katimuliwa
 
Mkuu mtu anaweza kuwa boyhood fan, lakini baadae akabadilika baada ya kucheza timu flani kwa muda mrefu

Mfano hata OGS juzi ame declare he is United fan

Tofautisha Kati ya Boyhood Fan na Plastic Fan

Boyhood Fan hawezi kuhama timu, Bali plastic Fan anaweza kuhama timu muda wowote hule kwa njia yoyote ile.

Au wewe unaweza kuhama Man United?

• Rio na OGS Ni boyhood Fans Wa Liverpool mpaka watakufa... Ila wanaheshimu Ulegend wao kwa Man United.
Kuchezea Man United hakuondoshi mapenzi ya timu nyingine.

• Ni sawa na Carragher aliwakamia Everton kwenye game lakini Ni Shabiki Lialia kindakindaki Wa Everton.

• Au De Bruyne anacheza Man City na anatukamia kwelikweli lakini Ni Shabiki lialia Wa Liverpool.

• John Terry Ni Legend Wa Chelsea lakini Ni Shabiki lialia Wa Man United.

• Henderson Ni Captain Wa Liverpool lakini Ni Shabiki lialia Wa Man United.

• Theo Walcot alipokuwa Arsenal alikuwa Akitufunga lakini Ni Shabiki lialia Wa Liverpool.

• Thiery Henry Ni Legend Wa Arsenal lakini Ni Shabiki lialia Wa Liverpool.

• Paul Merson Ni Legend Wa Arsenal lakini Ni Shabiki lialia Wa Chelsea.

• Luke Shaw Ni mchezaji Wa Man United lakini Ni Shabiki lialia Wa Chelsea.

• Lallana yupo Liverpool lakini Ni Shabiki lialia Wa Everton

• Milner yupo Liverpool lakini Shabiki lialia Wa Man United.

Kwahiyo Kupenda timu usiyoichezea kupo Mkuu wala hakubadiliki.
 
View attachment 975315

Tupate maneno ya wadhamini wetu

Sijui kuhusu united fans wengine ila wengi wetu humu tumefurahishwa na aina ya uchezaji wa timu zaidi kuliko idadi ya magoli. Mpira saffi ukisindikizwa na matokeo mwanana,hapo lazima usahau shida zako kwa muda kidogo ufurahie maisha.
Tulitamani kuona uchezaji wa aina hii ambapo wachezaji wanatembea lakini wanauamrisha mpira kutii uelekeo tofauti tofauti nao unatii. We fikiria Jana nimeshuhudia Ashley young anapiga no look pass tena kwa kisigino!
Thanks ogs,you brought the united we once lost!!!!
 
huyu Di MAteo alichukua UEFA na bado akafungashwa virago, why?
swali la 1 ulilouliza humu ndani ni hili:
hivi hawa ma interim coaches hata wakichukua ubingwa huwa hawapewi timu kwa sababu gani?

nikajibu kwa kumtaja roberto di matteo alipokuwa chelsea alirithi kibarua cha andreas villas boas na kufanikiwa kuwapa chelsea ubingwa wa FA na champions league dhidi ya bayern munich ndipo baadae akapewa mkataba wa miaka 2.

huyu Di MAteo alichukua UEFA na bado akafungashwa virago, why?

huu ni mjadala mwengine ambao umeamua kuuanzisha kupitia mgongo wangu dhaifu usiokuwa na uwezo wa kubeba hata gunia la usufi.
Roberto di matteo alifukuzwa msimu wake wa kwanza akitumikia mkataba wa miaka 2 na si kweli ya kwamba alifukuzwa wakati akiwa bado ni kocha wa muda.
  1. alifukuzwa November 2012 baada ya kufungwa na juventus magoli 3 na kupelekea chelsea watolewe hatua ya makundi.
  2. wakati anafukuzwa chelsea walikuwa nafasi ya 3 kwenye msimamo wa ligi kuu huku wakiwa nyuma kwa alama 3 dhidi ya man city ambao ndio waliokuwa wakiongoza ligi.
  3. kwa maswali zaidi tembelea thread ya chelsea naamini maswali yako yatajibiwa kwa ufasaha zaidi japokuwa kwa nyakati hizi wanaugulia maumivu ya kukosa mshambuliaji na si maumivu ya kufungwa na leicester city.
1545515739994.png
 
Back
Top Bottom