Manchester United (Red Devils) | Special Thread

“Last week, before the Crystal Palace game, I said my target was end of December to be in that position. The target changes but in the sense of let’s try to close the distance the best we can and be very close to these positions.

“I think Manchester United, in seventh place, I can agree, in spite of the investment Everton made, which was phenomenal.
“Obviously there was a great improvement in that team from last season in relation to this season, but I don’t think Everton will be in front of us at the end of the season.
“There are six teams that should stay in the first six positions. Season after season, two of these teams are staying outside the top four.


Kwahizi Kauli za Mou Kwanzaa kusema hadhani kuwa tutakuwa top four Mwisho wa December inaonesha kabisa kocha hana future plans badala yake anaweka malengo kiovyo Ovyo tu alisema week 2 zilizopita tutakuwa top 4 leo anasema hatuwezi kuwa top 4 after December....hii inaonesha mzee anafeli hajui hata target yake ni ipi....

Pili kusema kuwa hadhani Everton watakuwa juu yetu na kusema kuwa top 6 sijui na kumaliza top 6 inamaanisha target yetu kubwa ni kumaliza namba 6... hapo katumia pesa kusajili wachezaji Qatari ambao hawatumiki wanakaa benchi
.......

Hebu board itutolee huu upumbavu wa Mou yani sijawahi ona timu mbovu Kama hii huyu boys toka msimu unaanza yeye hakuwaza kuwa tutamake it to the top 4 sijui timu inawaza nini.... Hadi muda mwingine nahisi labda board inamuogopa Mou na inaogopa ikimfukuza ataisema vibaya club na board kiujumla......
 
Alafu kuna ulazima wa kuzungumzia investment za timu nyingine maana leo kahamia Everton kusifia investment yao kwani sisi tunavyotoa paun mil 75 kununua mchezaji wa everton haikuwa investment..... Anaishiwa viteteo bado kazi anayo mpaka nywele zipate rangi nyeusi
 
Ina maana hata wewe ulikuwa humjui Mourinho ?

Mourinho hajabadilika waliompa hii kazi labda walikuwa hawamjui Mourinho.I think anaweza asimalize huu msimu but kama decision makers hawajagundua tatizo cycle ya kufukuza makocha itaendelea

He has nothing to loose but still tuna miaka 6 klabu bado haijawa stable
 
Succession plan ya Man united ilifanyika kipuuzi sana ndiyo maana team imegeuka kichwa cha mwendawazimu kila mtu anajifunzia kunyoa.

Hivi vision ya Woodward kwenye hii team ni nini hasa ?
 
Succession plan ya Man united ilifanyika kipuuzi sana ndiyo maana team imegeuka kichwa cha mwendawazimu kila mtu anajifunzia kunyoa.

Hivi vision ya Woodward kwenye hii team ni nini hasa ?
Ed Woordward naye ni jipu kubwa sana..Jamaa sijui plan zao ni nini hasa..kama ni hela wanaingiza lakini as time goes mapato yataanza kudrop naamini
 
Heri David Gill angebakia angalau kwa mwaka mmoja huenda team isingekuwa hovyo namna hii.

Inaonekana kabisa tatizo la Man u liko nje ya uwanja na linakuja kuongezea na mapungufu ya mwalimu aliyepo ni shida tupu
Ed Woordward naye ni jipu kubwa sana..Jamaa sijui plan zao ni nini hasa..kama ni hela wanaingiza lakini as time goes mapato yataanza kudrop naamini
 
Heri David Gill angebakia angalau kwa mwaka mmoja huenda team isingekuwa hovyo namna hii.

Inaonekana kabisa tatizo la Man u liko nje ya uwanja na linakuja kuongezea na mapungufu ya mwalimu aliyepo ni shida tupu
Matatizo yapo mengi nje ya uwanja..Recruitment system yetu kwa miaka minne iliyopita imekuwa ni ya hovyo hovyo tu..no progression kabisa ..

Na ukiongeza na Mourinho tuliyenaye basi matatizo ndo yanazidi kuwa lukuki...

Angalia sasa saivi timu inafight ili ipate nafasi ya Europa next season..

Hii timu inanipa maumivu sana aisee...

Msimu mzima hakuna mechi tuliyocheza vizuri 90mn..
 
Siku hizi man u haichezi mpira bali inapiga mpira.
Team gani hauwezi kuona successive pass zaid ya tatu uwanjani unless wawe wanapiga mabeki tu.

Team inacheza zaidi ya dakika 20 haijapiga hata shot off target jamani.

Mtu akipoteza mpira anatembea tu badala ya kukaba na wanachrza slow kama wagonjwa actually man u inaboa sana kuangalia siku hizi kwa sisi tunaoangalizia vibandaumiza tunalipa hela kwenda kuangalia upumbavu na siyo mpira.
 
Msimu ndo ushaisha huu..sasa acha tuone Bodi ina mpango gani na hii timu..

Timu inabutuabutua tu ili eti fellaini abahatishe ashinde..No plan at all
 
Yeah japo wakishambulia wanapata magoli sijui ni nini kinacholazimisha tupaki basi hata kwa timu ndogo kama Soton tu
Msimu ndo ushaisha huu..sasa acha tuone Bodi ina mpango gani na hii timu..

Timu inabutuabutua tu ili eti fellaini abahatishe ashinde..No plan at all
 
Mourinho atafukuzwa pale itakapoonekana hakuna uwezekano wa kumaliza top 4 na mmeshashindwa kubeba UCL msimu huu. Vuteni subira.
BTW kesho kuna uwezekano wa kutunyamazisha. Historia ya Arsenal kubamizwa Old Trafford inaweza kuendelea. Na hii si kwa sababu tu ya Mourinho bali ni kwa pride ya wachezaji wenu kutotaka kufungwa na timu kubwa hasa Arsenal nyumbani.
But endapo Manchester United ikifungwa Mourinho atakuwa katika wakati mgumu zaidi hasa kwa masapota.
 
Mbivu na mbichi kujulikana Leo
 

Mimi mwenyewe Jose kwa kikosi chake dhidi ya soton sijui aliwaza nini
 
Kuelekea Katika Mchezo Wa leo Kati ya Man Utd Vs Arsenal

Nikiwa Kama Mchambuzi Wa Soka
Ngoja NiwaKumbushe Kidogo
Mara ya Mwisho Arsenal Kupata Ushindi Pale Old Traford Katika Epl ilikua Mwaka 2006 Man Utd Walifungwa Bao Moja Goal Alifunga Adebayor Pass Kutoka Kwa Fabregas
Ni miaka 12 imepita Je Arsenal Atafuta Uteja Wa miaka 12 Pale Old Traffod
 
Arsenal kuvunja mwiko wa kitambo kingi ??

Leo katika dimba la Old Trafford Manchester United wanawakaribisha Arsenal katika mechi ya ligi kuu ya soka ya Uingereza inayotarajiwa kuanza mishale ya saa 5:00 Usiku.

Arsenal wana rekodi mbaya ndani ya dimba la Old Trafford katika mechi za Ligi kuu ambapo mara ya mwisho kupata ushindi katika uwanja huo kwa mechi za Ligi kuu ya Uingereza ni Septemba 17, 2006 goli la Emmanuel Adebayor.

Na kwa kipindi chote hiko cha takribani miaka 12 Arsenal wamekuwa wanachezea kichapo au kupata sare tu .

Je unadhani vijana wa Unai Emery wanaweza kuvunja huo mwiko na kupata ushindi leo ? au United wataendelea kutunza rekodi yao ?
 
Fear factor ya Old Trafford haipo tena nategemea Arsenal kutunyanyasa sana Leo.

Na Leo hii mechi siangalii sipendi aibu za kujitakia Mimi.
 
Team inacheza utafikiri wachezaji wote wanamiaka sabini kumbe age average ya squad ni 24 years. Huu si upuuzi ?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…