Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Point ila soko liliharibiwa sana na psg na man city chelsea hawakuwa wakitoa mpunga sana watafuta vipaji wao wa chelsea walikuwa vizur sana

Usajili wa robinho na lucas moura ulianza kutungisha soko.
utani kidogo
  1. usajili wa rio ferdinand kwa paundi millioni 31 kutoka leeds haukuharibu soko la usajili miaka 17 iliopita?
  2. usajili wa wayne rooney kwa paundi millioni 25 akiwa na miaka 18 kutoka everton haukuharibu soko la usajili.?
  3. usajili wa juan sebastian veron kwa paundi 26 million haukuharibu soko la usajili?
tatizo sio kutumia fedha nyingi bali tatizo ni kutumia fedha nyingi na hatimaye matarajio yakawa madogo kama yanayotukuta sisi nyakati hizi.
hahahahahaaaa ferguson alizowea kumuonea masikini professor wenger.
 
United ili-spend fedha ambazo zilitokana na mapato ya klabu unlike City/Chelsea ambao fedha zilitoka Kwa wamiliki wa klabu directly ndio maana UEFA waliamua kuanzia Financial Fair Play ingawa nayo imefeli
 
Asiekuelewa hapa hakika hatakuelewa kamwe nafikir hii ndo post the best ktk majukwaa yote ya mpira hapa jf kwa upande wangu uchambuzi na namna ulivyoziangalia timu nyingine.
 
Mkuu kwanza inabidi uelewe tu hiyo advantage ya kufundisha miaka yote hiyo 26, ni yeye ndio ameitengeneza ..... Kwa hiyo haikushushwa tu kutoka Mbinguni.

Yeye amekuwa kocha kwa miaka 26 pale United consecutively, he hao wengine (kama Lipi) kwanini hawakuwa makocha mfululizo, je walikosa timu na kama walikosa timu kwanini, kocha bora huwa anakosa timu kwa muda mrefu? Kama sio bora kwa kiwango hicho, basi sio bora, waache waendelee kuwa nyuma ya SAF kwenye mafanikio ambaye ni bora.

Hao wengine hawakuweza kukaa timu moja kwa sababu mbalimbali, lakini kubwa ikiwa hawakuwa na consistence kwenye mafanikio kwa miaka mingi na mwisho wa siku kutimuliwa. SAF alikuwa ana consistence ya mafanikio na hata yeye angekuwa hapati mafanikio pale United angetimuliwa mapema na asingedumu kwa hiyo miaka 26.

Jambo lingine naona wewe umeweka standards kubwa sana (KIPIMO CHAKO CHA MAFANIKIO NI KIKUBWA SANA). Yaani ili kocha ahesabike amefanikiwa UCL inabidi awe angalau amefika fainali, knock out stage, robo fainali na nusu fainali unaona kwamba hayo sio mafanikio.

Embu tufanye Kipimo chako cha mafanikio ni kuingia fainali ((ambacho mimi naona si kipimo sahihi). Yeye kwa miaka 26, amefika fainali mara 4, embu nitajie makocha waliowahi kufika fainali angalau mara 5 (maana mara 4 si mafanikio). Tuanzie hapo ili tujue kuna makocha wangapi wenye mafanikio katika UCL. Baada ya hapo tukubaliane kama idadi hiyo tu ndio makocha wenye mafanikio UCL.
 
Mkuu hiyo bei ilikuwa inaweza kutolewa na timu zenye daraja la juu

Hata ulikuwa ukiangalia uwezo wao kisoka ulikuwa sawa na bei mfano hao wote walifika nusu fainali ligi ya mabingwa kwa kipindi kile ulikuwa unaona viwango halisi kabisa

Sasa kwa mfano lucas moura anatoka brazil moja kwa moja kwa paund million 35 ilikuwa halali? Hiyo psg walilipa wakat uhalisia wake alikuwa na thamani ya 25 hizo ndo mmevutana na mawakala ikafika 25
 
Mimi mkuu sikuelewi kwanini unaona kama SAF kukaa timu moja ni privilege aliyopata, hiyo sio privilege bali matokeo ya uwezo wake. Wewe unadhani Mourinho hapendi kukaa timu moja muda mrefu, au Pep au Ancelot au Zidane? Mimi nadhani unapaswa kumsifu kwanza ameweza kukaa muda mrefu timu moja.

Pep na Zidane ni mifano mizuri sana. Wewe unadhani Pep kwanini alikimbia Barca, alijua within 3 to 5 years hatakuwa na Xavier, Iniesta, Puyol, Messi, Bosquet and co. (Na hata wakiwepo hawatakuwa wa kiwango hicho sababu ya umri) ( Hii ilikuwa CORE ya Barca)

Unadhani Zidane hakupenda kufundisha Madrid miaka 20+, alisoma upepo, aliona wachezaji wake tegemeo kama akina CR 7, Ramos, Modrick, Pepe, walikuwa mwishoni, (Pepe alishaondoka) Bale (Zidane angebaki, yeye angeondoka n.k), Alikimbia fedhea (Hawa ni CORE ya timu ya Madrid)

Nadhani wewe tu ndio utakuwa una wasiwasi na uwezo wa SAF katika UCL, lakini dunia nzima wapo tofauti na wewe.
 
Usisahau na kuweka orodha ya tuliowafunga/kuwatoa kwenye miachuano ya UCL

Naona umefumbia macho statistics nyingine
 
hahahahahahahahaaaa usajili wa lucas moura umenikumbusha mbali sana.
sir alex ferguson alichukia sana baada ya waarabu wa PSG kumpokonya tonge mdommoni.
nayafahamu yote hayo brother ila tunavuta muda wa kuangalia timu yetu hivyo basi mijadala kama hii inapendeza ikiwepo.
I find it quite amazing that a club can pay 45million euros for a 19-year-old boy," said the Scot.
Lucas Moura PSG deal angers Sir Alex Ferguson


kuna dalili yoyote ya diogo dalot kupewa nafasi leo?
 
Ipo mkuu mourinho aliongea juzi kwamba majeruhi aliyokuja nayo sasa yamepotea pia kuna kitu nimegundua bailly anamsubir rojo arudi vizur mourinho nimeona ni mjanja bailly anacheza vizur sana rojo

Kwa hiyo leo dalot atacheza.
 
Ipo mkuu mourinho aliongea juzi kwamba majeruhi aliyokuja nayo sasa yamepotea pia kuna kitu nimegundua bailly anamsubir rojo arudi vizur mourinho nimeona ni mjanja bailly anacheza vizur sana rojo

Kwa hiyo leo dalot atacheza.
tuombe hivyo hususan kwa eric bailly.
hii dunia imeshaharibika na itapotokezea eric bailly akatingisha kibiriti itakuwa ni mtihani kiupande wetu.
fikiria tetesi zote za usajili wa mabeki wanavuka 50 millioni.
 
tuombe hivyo hususan kwa eric bailly.
hii dunia imeshaharibika na itapotokezea eric bailly akatingisha kibiriti itakuwa ni mtihani kiupande wetu.
fikiria tetesi zote za usajili wa mabeki wanavuka 50 millioni.
Kweli mkuu huyu kumpoteza ni hasara bado mdogo sana miaka 23 naona kocha kaamua kumtengeneza kiakili maana zile goli mbili harakaharaka za newcastle zilimpoteza kabisa
 
natamani atokee mwanadamu amshitue mourinho atufanyie biashara zifuatazo.
julian draxler / marco reus
douglas costa
thiago alcantara.
tutakuwa na uwezo wa kusimama na timu yoyote ile barani ulaya.
Mkuu hapo mm namuona douglas costa timu yetu inamhitaj sana mtu kama huyo kiungo kama cha kante tupate na mtu kama tobby aisee ntakuwa mjanja sana
 
Mkuu nimekuelewa Sanaaa. Umechambua vizuri Sanaa.

Japo hapo mwishoni daah!! naomba nikanushe kabisaaa. SIJATUMWA NA MOU. Hahahahaaa.

Pia ningependa kusikia maoni yako juu ya heshima anayo pewa Fergie kulinganisha na mafanikio yake nje ya mipaka ya uingereza
 
Mkuu Damushin kwanza nikupongeze kwa uchambuzi wako makini usiochosha kusoma

Mkuu itabidi tu umtelekeze Johnmweusi na uhamie upande wetu, kwani inaonekana bwana Johnmweusi anajisahaulisha kuwa UCL ndio mashindano yanayokutanisha cream ya wachezaji bora ulimwenguni. Anajisahaulisha kwamba yale ndio mashindano bora kwa ngazi ya vilabu ulimwenguni yanayokutanisha timu bora 32 kabisa kutoka barani Ulaya (Ushahidi karibu kila Klabu bingwa dunia huwa inachukuliwa na bingwa wa UCL). Hivyo hayo si mashindano ya timu ama kocha kushinda kila mwaka.

Nirudi kwenye hoja, ukirejea takwimu zako utagundua kuwa kwa takribani hiyo miaka 21 ambayo SAF alipambana Ulaya ni wastani wa kila baada ya miaka 3 aliweza kuifikisha nusu fainali Man Utd. Na katika miaka hiyo ni wastani wa kila baaada ya miaka 5 SAF aliweza kuifikisha United fainali. Na hiyo inaonesha kuwa SAF aliweza kuchukua kombe la UCL kila baada ya miaka 10. Je hayo si mafanikio? Ni makocha wangapi wameweza kufanya hivyo? (Japo Johnmweusi hataki tufananishe na makocha wengine, lakini unapoongelea ubora wa kitu/mtu lazima utumie ufafanisho, kama mzani vile huku jiwe, upande wa pili sukari)

Kwa vigezo vya mkuu Johnmweusi tunaweza tusiwe na kocha bora/mwenye mafanikio katika mashindano ya UCL.

Lakini pia niwakumbushe tu wadau kwamba unapoongelea tuzo barani Ulaya, kuna mashindano zaidi ya Kombe la UCL. Kiujumla SAF ana tuzo 7 za Ulaya alizoshinda kutokana na mashindano mbalimbali ya Ulaya. Yeye na Waitaliano wawili Trapaton na Anceloti ndio wanaongoza kwa kushinda tournaments za Ulaya (mara 7).
 
Ukiacha sir alex

Basi kocha wa pili nimpendae ni huyu frenk RijkaadView attachment 952138

Messi, Iniesta, Gerrard Pique, Xhavi (I'm not sure), Etoo na Yaya Toure wasipompa heshima Huyu aliyewatoa Mashimoni basi Wametukosea sote Wadau Wa Soka.

Lakini Cha Ajabu Wanampa Heshima PEP (exclude Eto'o na Yaya) aliyekuja Kuwatumia tu akaondoka...

Ni ubaguzi kwasababu Ni Mspain na Mlatini mwenzao.
 
Wengi hawatambui hilo huyo jamaa kaisimamisha barca wanampaga sifa pep ambae kaikuta misingi imewekwa na huyo mholanzi.
 
United wame-activate one year extension kwenye mkataba wa De Gea na mazungumzo ya kuongeza mkataba yanaendelea (De Gea will not be free agent next summer)
Bado naona 2020 anaweza kusepa huo mkataba nnawasiwasi nao sana sanchez na pogba kimshahara wameongeza ugumu de gea anataka 300 kwa wiki
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…