kusema kweli kwa wapenzi wa mpira wa mguu ambao hawaongozwi na ushabiki wa kinafiki, MAN UTD wanachosha na kuondoa utamu wa mpira pindi wanapocheza. Mimi sijapata kujua kama viwango vya wachezaji ndo umeshuka au kocha ndo ufundishaji wake umekosa ubunifu.
Mchezaji anapata mpira unaona kabisa hajui aipeleke wapi, kwakweli imefika wakati MU waanze uwekezaji upya wenda kwa kumchukua kocha mzaliwa wa United (mfano akina Giggs and Company), wachezaji akina Rashford (amelewa sifa kwa kuaminiwa akiwa bado kijana mdogo), Lukaku, Smalling,Jones, Matic wote waondolewe United.
United ilianza kuangaika kipindi cha Van Gaal kwa mfungaji akatafutwa Ibra na Falcao bado shida ikabaki vile vile, akaja akina Lukaku na Alex mambo yanazidi kua mabaya. Ni maajabu timu imeshafungwa magoli 22 na wao wamefunga magoli 21 ndani ya mechi chini ya 11 ya Ligi kuu. Sisi wapenzi wa mpira itatupendeza zaidi Man U wakianza uwekezaji upya, hakuna cha majina makubwa kwa upande wa ukocha na wachezaji wameshindwa tayari.
Sisi wenzenu bado tunaangaika wa mfungaji asiyetupa pressure mpaka sasa tokea enzi za Torres>Demba Ba> Etto>Falcao>Costa>Drogba>Morata>Mitchuy>Gerou......Bado tunaangaika tu.
Timu nyingi bado wanamwona na kumwacha Zaha wakati anaitaji kufundishwa kitu kimoja tu kulenga goli na wakati gani wa kutoa mpira mguuni wake.