hahahahaaaaa humu ndani kila member ana haki ya kutoa maoni yake muda wowote ule anaojisikia utayari wa kufanya hivyo, wala usijisikie tabu kutoa mawazo yako brother.
unajua mwanadamu kadri unapokutana na changamoto kwenye mfumo wako mzima wa maisha kitu kikubwa kitakachotawala nafsi yako ni mawazo,fikra na maswali yasiokwisha.
hii hali ndio imeikumba klabu ya manchester united nyakati hizi ambapo kwa sasa kila anayehusika na man utd kuanzia sisi wapiga kelele ambao wengi wetu hatujawahi hata kufika old trafford hata kwa njia ya ndoto mpaka yule mfagiaji wa uwanja anauwazia huu mkwamo ulioikumba man utd ndani ya uwanja, hivyo basi hata kama utamfanyia mahojiano ili uweze kukusanya maoni juu ya kinachochangia mkwamo uliopo na yeye atatoa sababu zake bila ya shinikizo lolote kama unavyopaswa na wewe kufanya humu ndani.
Hoja yako ulioiwasilisha kwa maoni yangu nahisi pia ina ukweli kwa asilimia kubwa sana na ndio iliosababisha kuwepo sintofahamu kati ya jose mourinho na ed woodward kwenye biashara ya usajili msimu huu japokuwa ed woodward hajawahi kutamka hadharani sababu zilizopelekea kushindwa kufanya usajili wa baadhi ya demand za kocha.
wachezaji wote aliowasajili jose mourinho huko walikotokea walikuwa ni muhimu kwenye vikosi vyao hivyo basi kwa kuwatumia wale wachezaji aliowaacha LVG na david moyes tulipaswa angalau msimu huu tuwe tayari tumeshajenga timu yenye kueleweka kimfumo wa uchezaji na hicho ndicho anachokiamini ed woodward na mashabiki wake nikiwemo na mimi kwa asilimia 50.
umekuja kwenye klabu umemkuta marcos rojo, degea, valencia, young, mata, rashford, martial,herrera n.k.
Haijatosha nimekuongezea pogba, ibrahimovic,mkhitaryan, bailly ukafanikiwa kutupa makombe mawili msimu wako wa kwanza.
nikaona haitoshi nikamuongeza lukaku,matic, lindelof na ukafanikiwa kutupa nafasi ya pili huku tukicheza zaidi ya mechi 20 msimu mzima bila ya kuruhusu goli kwa defence hii iliopo. Msimu wa tatu nimekupa fred, dalot na wachezaji wote muhimu waliokuwepo msimu uliopita wameendelea kuwepo, haitoingia akilini eti timu ile ile iliyocheza mechi takribani 20 bila ya kuruhusu goli leo hii iruhusu magoli 20 kwenye mechi 12 kwa sababu ya kutokukupa hela ya kumsajili mlinzi mwengine wa kati.
Unajua msimu uliopita kwa defence hii iliopo hatukufikisha mechi 10 tulizoruhusu zaidi ya goli 2 kama sikosei?
unajua msimu uliopita kwa wachezaji hawa wa mbele tulikuwa na takwimu zenye kuridhisha kwenye ufungaji wa magoli tukizidiwa na man city na labda liverpool.
sasa mbona liverpool defence yao ndio ile ile lakini bado wamezidi kuwa imara?
mbona chelsea timu yao ndio ile ile aliyoiwacha conte antonio wakiwa nafasi ya 5 lakini wapo vizuri.
- je inawezekana kutosikilizwa kwake kimawazo kumemfanya mourinho awe na hasira hivyo basi ameamua kutufanya tuonekane dhaifu kwenye ulinzi ili aonekane madai yake yana ukweli na aonekane nabii msema ukweli kama anavyodhani radika kupitia coment yake moja hapo juu?
lakini tukiangalia upande mwengine wa shilingi hata madai ya jose mourinho na washabiki wake yana ukweli ndani yake nikiwemo na mimi kwa 40%, biashara ya usajili nayo pia ni biashara isiyotabirika kwa asilimia 100, unaweza ukawa na matumaini ya kwamba mchezaji fulani atakuja kukupa kitu kikubwa utakapomsajili lakini ikawa ni kinyume chake hivyo basi itakulazimu umvumilie japo kwa miezi 6 au ukiona improvement yake ni kinyume na matarajio utafute mbadala wake.
jana kwenye mawazo yangu nilizungumzia jinsi gani mzee alex ferguson alivyokuwa anajenga timu yake, lakini kwa hali hii iliofikia si vibaya kama tutaendeleza mfumo huu wa kutumia fedha ovyo kwa dhumuni la kurudisha heshima yetu kwanza halafu baadae tutarudisha falsafa zetu za zamani kwa kumtumia mwalimu mwengine na hii ni kwa sababu jose mourinho tokea aifahamu harufu ya fedha ya kupitia mikono ya bilionea Roman Abramovich hajawahi kuwa muumini wa kujenga timu kwa kutumia mfumo wa academy au kununua wachezaji kwa bei rahisi baadae akawatengeneza.
ina maana bodi walikuwa hawalifahamu hili walipokuwa wanampa ajira?
bila shaka walikuwa wanafahamu ila waliamua kumpa timu kwa dhumuni lile lile la kuhitaji aturudishie heshima yetu japo kwa njia ya kinyume na falsafa za uendeshaji wa timu ya man utd, why wanamgeuka kwa hoja dhaifu eti tulishakupa paundi millioni 60 za usajili wa bailly na lindeloff?
mbona majirani zetu walishawahi kulipa paundi millioni 40 kwa ajili ya mangala ambaye ni flop?
mbona majirani walishalipa paundi millioni 50 kwa ajili ya torres?
mbona majirani walishalipa paundi millioni 30 kwa ajili ya wilfred bony ambaye ni flop?
mbona guardiola alilipa fedha nyingi kwa ajili ya bravo na msimu uliofuata akatafuta kipa mwengine?
mbona josep guardiola licha ya kuwa mpaka januari msimu uliopita alishatuongoza kwa pointi 12 na alifanya usajili wa mlinzi anayeitwa laporte sasa kwa nini mourinho aliyeachwa kwa pointi 20 baada ya ligi kumalizika awekewe kizingiti anapotaka kumsajili mlinzi mwengine wa kati?
mbona alex ferguson alimsajili juan sebastian veron na diego forlan akawa flop na bado aliendeleza kutumia hela.
imani yangu inanifanya niamini ya kwamba bodi ina matatizo na mourinho ana matatizo sasa je ujio wa mkurugenzi wa ufundi ndio utaondoa tatizo la pande mbili hizi?
mimi sijui la muhimu tuombe uhai ili tumshuhudie bosi mpya atakayewatuliza jose na ed woodward.
nimesikia ivan campos anapigiwa upatu kuja man utd na anatokea lille ya ufaransa.
wenye kufahamu mafanikio ya ivan campos tokea akiwa real madrid naomba atuwekee kwa faida ya wote.