Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Ujio wa Matic umem-cost Herera japo Kocha angeweza kum-accommodate km Sari alivyom-accommodate Ngoro kufuatia ujio wa joginyo.

Hererra kusimama DM kwa kweli simuamini, anafit namba nane. Matic ndio mtu poa kwenye DM pale Old Traford
 
44203684_527620547703941_4051514426904413771_n.jpg
 
Yaani timu yetu bado sana,wachezaji wanazingua sana. Goli LA rashford kama kungekuwa na mabeki wazuri asingefunga. Movement ya kwanza alopaswa kufunga akazubaa beki akafika aka clear. Ku clear kwake vibaya akawa amemsetia dogo akafunga. Kabla ya hapo yeye na lingard walikosa magoli ya wazi. Bado timu yetu ina utoto na papara nyingi. Sanchez nilimuona ni mzigo tu Leo,jamaa amezidi kupoteza concentration, mzito kidogo ktk maamuzi,mpotezaji mipira kirahisi
 
Kati ya watu hawafai kucheza ni fred
Bwana mdgo bado sana
heshima kwako rafiki.
nathubutu kusema comment yako japokuwa ni fupi sana ila kiupande wangu naichukulia ni miongoni mwa comment bora kwa siku ya leo ikifuatiwa na comment ya Darmian ambayo alikuwa anazungumzia performance isiyoridhisha ya Nemanja Matic msimu huu unaoendelea. navutiwa sana na mshabiki wa mpira mwenye tabia na mtazamo kama upepo unaovuma kwa kasi kuliko mshabiki wa mpira mwenye tabia na mtazamo usiobadilika, bahati mbaya sana humu ndani washabiki wengi hatuna tabia za upepo unaovuma kutokana na mabadiliko ya hali ya hewa.

kiupande wangu nipo tofauti sana ukilinganisha na baadhi ya wachangiaji wengine wenye msimamo mmoja tu na hata ukijaribu kuzipitia comment zangu zilizopita ndani ya thread hii utagundua ya kwamba maandishi yangu yana nafsi mbili (hupendelea kuwasilisha mawazo yangu kwa kuangalia zaidi muda uliopo). Sisi wengine mpaka muda huu hatujajiingiza kwenye starehe za ulevi, kamari, ngono zembe na hata kufuatilia video za ovyo kama za amber rutty na wajinga wengineo lakini tunapoteza muda mrefu sana kwa ajili ya kufuatilia starehe ya mpira wa miguu, sote tunafahamu machungu na madhila tunayoyapata pindi starehe unayoipendelea inapokwenda kinyume na matarajio yako uliojiwekea.

Sababu kubwa iliyonifanya ninukuu comment ya brother hapo juu ni kuhusiana na jambo moja tu ambalo kiupande wangu naliona halipo sawa kwenye klabu yetu tunayoishabikia na kadri siku zinavyosogea jambo hilo nyeti mizizi yake inazidi kwenda chini ya ardhi bila ya kutafutiwa ufumbuzi, jambo hilo si jengine isipokuwa ni sera za kutafuta wachezaji wapya (usajili)

ukweli utatuweka huru na haijalishi ukweli huo ni mchungu, jamani klabu yetu ya Manchester united tumekuwa ovyo sana kwenye soko la kutafuta wachezaji watakaoweza kuendana na misingi ya timu yetu na ugonjwa huu ulianza tokea wakati wa utawala wa Sir Alex Ferguson.
Babu yetu fergie miaka yake 4 ya mwisho alianza kuonyesha udhaifu mkubwa sana kwenye soko la usajili jambo la kushukuru zaidi soko la ushindani wa ligi kuu nyakati za fergie ilikuwa ni afadhali sana ukilinganisha na nyakati hizi. Japokuwa wachezaji hao hao wenye viwango vya kawaida walikuwa wanatupa ubingwa wa ligi kuu lakini udhaifu wao ulikuwa unaonekana kwenye michuano ya ligi ya mabingwa ambapo mara nyingi tulikuwa tunaishia kufungishwa virago na timu zilizo makini kwenye soko la usajili zaidi yetu. Sina nia ya kumdhihaki ferguson ambaye CV yake ni kubwa na nzito zaidi ya mlima wa kilimanjaro ila najaribu kuonyesha ni wapi udhaifu wa timu yetu ulipoanzia na bado mpaka sasa udhaifu huo unaendelea kututafuna.
nimebaki najiuliza maswali yafuatayo muda huu?​

  • je wasaka vipaji wetu wamepoteza nuru kupitia jicho lao la tatu ambalo ndio muhimu zaidi pindi unapomchunguza mchezaji unayemuhitaji?
  • je inawezekana makocha wetu wamepoteza uwezo wa kuweza kumtambua ni yupi mchezaji atakayefaa kwenye falsafa zake na hatimaye wanaamua kucheza kamari la usajili?
  • je inawezekana tatizo ni wachezaji wenyewe wanaosajiliwa wakija klabuni kwetu wanacheza kwa pressure sana jambo linalopelekea kupoteza kujiamini wakiwa uwanjani?
  • je inawezekana tumeingia kwenye mkumbo wa laana tokea nyakati za mwisho za ferguson lakini hatukuweza kuligundua mapema suala hilo la kusajili wachezaji watakaofiti kwenye timu, na kama tumeingia kwenye mkumbo wa laana ina maana hata kama tutamsajili mungu wa mpira lionel messi na malaika wake wa mpira kama mbappe, neymar watakuwa ni flop ndani ya klabu yetu?
  • je inawezekana mawakala na viongozi wa timu pinzani wanatumia udhaifu wetu wa kutaka kurudisha heshima ya klabu kwa haraka hivyo basi wanatuuzia wachezaji wenye viwango vya kawaida kwa fedha nyingi sana, rejea usajili wa lindelof, lukaku, fred,pogba, sanchez, tetesi za maguire na alderweireld kwa 60 millioni pounds.
nyakati za mwisho za utawala wa sir alex ferguson biashara pekee ya maana ilikuwa ni usajili wa chicharito ambaye hata kama leo angelikuwepo kwenye klabu yetu angelistahili kupata nafasi japo dakika 30
  1. klabu ilimuuza cristiano ronaldo ambaye ana uwezo wa kufunga magoli 40 kwa msimu cha ajabu anayerithi nafasi yake alikuwa ni antonio valencia ambaye mpaka leo hii sidhani kama amefikisha angalau magoli 40 ndani ya miaka 10 hii tokea asajiliwe manchester united. Kiwango chake kisichoridhisha kimechangia kwa kiasi kikubwa arudishwe eneo la ulinzi wa kulia, hata huku kwenye nafasi yake mpya amekuwa na kiwango kisichoridhisha na ndiye chanzo kikuu cha timu yetu kupoteza makali upande wa kulia kwa miaka hii.
  2. jaribu kuangalia usajili wa chris smalling kutoka fulham: fergie alikubali kuzidiwa kete na jose mourinho kwenye dili la varane kwa sababu ya smalling ambaye thamani yake ilikuwa ni paundi 10 millioni kama ilivyo kwa varane alipotoka lens ya ufaransa. huu ni mwaka wa saba jamaa kiwango chake hakieleweki wakati varane cv yake ni nzito. media za uingereza zilimjaza ujinga mzee wetu na kama kawaida yake akaonyesha mapenzi yake tena kwa wachezaji wa kiingereza, cha ajabu mimi niliyekuwepo huku nchi za kimasikini njaa kali niliamini ya kwamba smalling aling'arishwa zaidi na mwanadamu kutoka norway ambaye sura yake ilifanana na nemanja vidic muheshimiwa brade hangeland pale fulham.Cha ajabu smalling bado ameendelea kuwa sehemu ya tatizo hata nyakati hizi wakati huo huo tunamyemelea varane kwa dau la zaidi ya 60 millioni paundi.
  3. usajili wa Ashley young kutoka aston villa:nimeanza kumfahamu ashley tokea nipo shule ya msingi kipindi hicho anachezea watford akiwa bado na pumzi za kutosha (kinda), baadae akapiga mpira mwingi sana Aston villa chini ya mwalimu martin o'neill mpaka wakafikia hatua ya kugombania top 4 msimu ulee wa federico macheda alipotuinua kwenye viti dakika za nyongeza, miaka michache mbele ashley young alipoteza muelekeo wa kisoka na alizidiwa kiuwezo hata na steward downing na gabriel agbonlahor. hivi tukiachana na mechi ile tuliyomfunga arsenal magoli 8 ni mechi ipi nyengine ambayo young alionyesha kiwango cha maana akiwa uwanjani? Ashley young ameendelea kuwa ni sehemu ya tatizo kwenye klabu yetu ila cha kustaajabisha mourinho na bosi wake ed woodward wanafanya naye mazungumzo ya kumpa mkataba mpya.
  4. bila ya kuwasahau akina buttner, bebe, anderson, gabriel obertan.
utawala wa david moyes kutoka everton

  • mpaka leo najiuliza ina maana huyu moyes alikuwa haangalii rekodi za mechi za manchester united kabla hajaanza kibarua chake na kwa nini akatumia 30 millioni paundi kwa ajili ya marouanne fellaini, alipokuja manchester david tulikuwa na washambuliaji watatu lakini bwana yule akamleta fellaini awe namba 10 wetu. Fellaini ameendelea kuwa ni sehemu ya tatizo kwenye timu yetu hadi leo hii na hakuna kiongozi yeyote anayejali uchovu wa fellaini.Kocha na mtendaji mkuu anayekwenda na wakati hawezi kumpa mkataba mpya fellaini na hutomuona mchezaji mwenye uwezo kama wa fellaini kwenye timu kubwa isipokuwa manchester united
utawala wa van gaal

  1. huyu mzee ndio kazidisha majanga miaka yake miwili ya kazi, kamleta matteo darmian kwa 15 millioni ambaye hana cha maana alichokileta kwenye klabu yetu.
  2. kamleta morgan schneiderlin kwa 26 millioni paund na yeye amefeli, kamleta blind amefeli, depay pressure kubwa amefeli, di maria pressure kubwa amefeli.
  3. luke shaw baada ya miaka minne kupita kidogo ameanza kuonyesha mwanga wa kuonyesha thamani yake.
utawala wa jose mourinho

hizi zimekuwa ni nyakati za mawakala na viongozi wa timu kujikusanyia fedha nyingi kutokana na mauzo ya wachezaji wenye viwango vya kawaida wanapokuja manchester united. Leo hii tumekuwa hatuna tofauti kubwa sana na madada poa (makahaba) ambao huuza miili yao kwa ajili ya kupata pesa ya mkate na sabuni.
  • makahaba wanawapa wateja wao huduma kwa fedha kidogo japokuwa inasemekana huduma ya amber rutty (sijawahi kuona video yake) inakuwa na dau kubwa wakati manchester united tunatoa fedha nyingi kwa ajili ya kupewa huduma ya mchezaji aisiyetabirika.hawa mawakala akiwemo mino raiola, mendez wanatufanyia uhuni sana kipindi hiki.
usajili wa Fred
Inaumiza sana pale unapo endelea kushuhudia klabu ikiendelea kufanya makosa yenye kujirudia kila panapo funguliwa dirisha la usajili, tumefanya makosa kwa sanchez, lindelof, pogba (105 million pounds), dimaria n.k

Hivi kweli Fred huyu anayezidiwa kimpira na moussa dembele ana thamani ya paundi millioni 55 ?​
United tumepoteza muelekeo kiasi ambacho tunalipa hela ndefu kwa mchezaji ambaye hana uwezo wa kuingia kikosi cha kwanza nyakati hizi, sasa kwa nini tukamsajili au uvumi wa kutaka kuwapokonya tonge manchester city una ukweli ndani yake?

kule klabuni shakhtar donetsk,mchezaji Taras stepanenko alikuwa anacheza kiungo wa chini na fred akawa anacheza nafasi ya kiunganishi cha timu(box to box) wakati huku kwetu anayecheza nafasi hiyo ni paul pogba, kivyovyote fred hawezi kumweka nje paul pogba na vile vile hawezi kumweka nje nemanja matic ili awe kiungo mkabaji.
kocha akiwapanga wote watatu kwa pamoja tunakuwa wazito sana kuwasogelea maadui, ina maana benchi la ufundi walikuwa hawayajui haya?


fedha ya usajili wa fred ilipaswa itumike kwanza kwa ajili ya kumsajili mchezaji atakayetupa faida papo kwa papo hata kama ni mlinzi na si kumsajili mchezaji wa kusubiri mchezaji fulani apate majeruhi ndio apewe nafasi. Tuwatazame manchester city wamelipa paundi millioni 50 kwa ajili ya ryad mahrez ambaye tayari ana uwezo wa kuendana na kasi ya ligi kuu ya uingereza pamoja na mechi kubwa, kiukweli klabu imefanya tena biashara ya kijinga sana na viongozi wa shakhtar wana haki ya kutukejeli kwa kuwapa hela nyingi.

mbona manchester city wamelipa pesa nyingi kwa bernard silva, gundogan, danilo, mendy, jesus na bado wanakaa nje?
ukweli mwengine tusioupenda mashabiki wa manchester united ni kuhusiana na viwango vya wachezaji wetu ukiwalinganisha na wachezaji wa manchester city.
Tumekuwa tukijidanganya na kujiaminisha ya kwamba wachezaji wetu wana viwango sawa na wachezaji na timu nyengine ila tunakosa mwalimu mzuri wa kutengeneza wachezaji wetu wachezae vizuri.
Baada ya kuangalia mechi za msimu huu napingana na wale wanaoamini ya kwamba tuna wachezaji bora kama mancheter city, chelsea,liverpool na timu nyengine kubwa barani ulaya, nusu na robo ya wachezaji wetu wana majina maarufu sana lakini wakiwa uwanjani wapo ovyo kuliko soda aliokunywa bwana harusi wa UDSM.
Wenzetu bado wanaendelea na steji ya kujenga timu ya ushindani ukilinganisha na upande wetu sisi ambao bado tumeendelea kulala usingizi huku tukiringia historia.

bernard silva, gundogan, danilo, mendy wote hao wanapopewa nafasi kikosi cha kwanza wanacheza vizuri sana ukilinganisha na wachezaji wetu tuliowasajili kwa gharama kama vile lukaku, bailly, lindelof.
kwa hali tukiofikia hatuna haki ya kujilinganisha na miamba ya soka la bara la ulaya kama juventus, barcelona, madrid, atletico madrid, man city na hata liverpool.

siku ambayo fred atacheza vizuri nitakuja kumsifia humu ndani ila naogopa kusema iyo siku iko mbali sana.
1541283440788.png
 
Inatakiwa tuanze kufunga magoli mengi sasa, hii gd inaweza kumkosesha MTU uefa.
Kweli. Jamaa inabidi waanze kufanyia mazoea mpira wa kasi. Toka enzi United huwa hatu-possess bali huwa ni kasi na kushambulia kwa presha. Tulikuwa almost na utamaduni sawa na Liver. Tukiurejea huu, tunaweza fanya wizuri, japo hatuna winga tuna wachezaji wenye pace.

Liver anatisha lakini ha-possess sana mpira.
 
Mourinho: “He's (Herrera) a player of balance, he's not an incredible creator, not an incredible scorer, he has a little bit of everything but I think he's a player of balance, knowledge, his tactical knowledge is big, he understands what I want, what the team needs.” #mufc [MEN]
 
heshima kwako rafiki.
nathubutu kusema comment yako japokuwa ni fupi sana ila kiupande wangu naichukulia ni miongoni mwa comment bora kwa siku ya leo ikifuatiwa na comment ya Darmian ambayo alikuwa anazungumzia performance isiyoridhisha ya Nemanja Matic msimu huu unaoendelea. navutiwa sana na mshabiki wa mpira mwenye tabia na mtazamo kama upepo unaovuma kwa kasi kuliko mshabiki wa mpira mwenye tabia na mtazamo usiobadilika, bahati mbaya sana humu ndani washabiki wengi hatuna tabia za upepo unaovuma kutokana na mabadiliko ya hali ya hewa.

kiupande wangu nipo tofauti sana ukilinganisha na baadhi ya wachangiaji wengine wenye msimamo mmoja tu na hata ukijaribu kuzipitia comment zangu zilizopita ndani ya thread hii utagundua ya kwamba maandishi yangu yana nafsi mbili (hupendelea kuwasilisha mawazo yangu kwa kuangalia zaidi muda uliopo). Sisi wengine mpaka muda huu hatujajiingiza kwenye starehe za ulevi, kamari, ngono zembe na hata kufuatilia video za ovyo kama za amber rutty na wajinga wengineo lakini tunapoteza muda mrefu sana kwa ajili ya kufuatilia starehe ya mpira wa miguu, sote tunafahamu machungu na madhila tunayoyapata pindi starehe unayoipendelea inapokwenda kinyume na matarajio yako uliojiwekea.

Sababu kubwa iliyonifanya ninukuu comment ya brother hapo juu ni kuhusiana na jambo moja tu ambalo kiupande wangu naliona halipo sawa kwenye klabu yetu tunayoishabikia na kadri siku zinavyosogea jambo hilo nyeti mizizi yake inazidi kwenda chini ya ardhi bila ya kutafutiwa ufumbuzi, jambo hilo si jengine isipokuwa ni sera za kutafuta wachezaji wapya (usajili)

ukweli utatuweka huru na haijalishi ukweli huo ni mchungu, jamani klabu yetu ya Manchester united tumekuwa ovyo sana kwenye soko la kutafuta wachezaji watakaoweza kuendana na misingi ya timu yetu na ugonjwa huu ulianza tokea wakati wa utawala wa Sir Alex Ferguson.
Babu yetu fergie miaka yake 4 ya mwisho alianza kuonyesha udhaifu mkubwa sana kwenye soko la usajili jambo la kushukuru zaidi soko la ushindani wa ligi kuu nyakati za fergie ilikuwa ni afadhali sana ukilinganisha na nyakati hizi. Japokuwa wachezaji hao hao wenye viwango vya kawaida walikuwa wanatupa ubingwa wa ligi kuu lakini udhaifu wao ulikuwa unaonekana kwenye michuano ya ligi ya mabingwa ambapo mara nyingi tulikuwa tunaishia kufungishwa virago na timu zilizo makini kwenye soko la usajili zaidi yetu. Sina nia ya kumdhihaki ferguson ambaye CV yake ni kubwa na nzito zaidi ya mlima wa kilimanjaro ila najaribu kuonyesha ni wapi udhaifu wa timu yetu ulipoanzia na bado mpaka sasa udhaifu huo unaendelea kututafuna.
nimebaki najiuliza maswali yafuatayo muda huu?​

  • je wasaka vipaji wetu wamepoteza nuru kupitia jicho lao la tatu ambalo ndio muhimu zaidi pindi unapomchunguza mchezaji unayemuhitaji?
  • je inawezekana makocha wetu wamepoteza uwezo wa kuweza kumtambua ni yupi mchezaji atakayefaa kwenye falsafa zake na hatimaye wanaamua kucheza kamari la usajili?
  • je inawezekana tatizo ni wachezaji wenyewe wanaosajiliwa wakija klabuni kwetu wanacheza kwa pressure sana jambo linalopelekea kupoteza kujiamini wakiwa uwanjani?
  • je inawezekana tumeingia kwenye mkumbo wa laana tokea nyakati za mwisho za ferguson lakini hatukuweza kuligundua mapema suala hilo la kusajili wachezaji watakaofiti kwenye timu, na kama tumeingia kwenye mkumbo wa laana ina maana hata kama tutamsajili mungu wa mpira lionel messi na malaika wake wa mpira kama mbappe, neymar watakuwa ni flop ndani ya klabu yetu?
  • je inawezekana mawakala na viongozi wa timu pinzani wanatumia udhaifu wetu wa kutaka kurudisha heshima ya klabu kwa haraka hivyo basi wanatuuzia wachezaji wenye viwango vya kawaida kwa fedha nyingi sana, rejea usajili wa lindelof, lukaku, fred,pogba, sanchez, tetesi za maguire na alderweireld kwa 60 millioni pounds.
nyakati za mwisho za utawala wa sir alex ferguson biashara pekee ya maana ilikuwa ni usajili wa chicharito ambaye hata kama leo angelikuwepo kwenye klabu yetu angelistahili kupata nafasi japo dakika 30
  1. klabu ilimuuza cristiano ronaldo ambaye ana uwezo wa kufunga magoli 40 kwa msimu cha ajabu anayerithi nafasi yake alikuwa ni antonio valencia ambaye mpaka leo hii sidhani kama amefikisha angalau magoli 40 ndani ya miaka 10 hii tokea asajiliwe manchester united. Kiwango chake kisichoridhisha kimechangia kwa kiasi kikubwa arudishwe eneo la ulinzi wa kulia, hata huku kwenye nafasi yake mpya amekuwa na kiwango kisichoridhisha na ndiye chanzo kikuu cha timu yetu kupoteza makali upande wa kulia kwa miaka hii.
  2. jaribu kuangalia usajili wa chris smalling kutoka fulham: fergie alikubali kuzidiwa kete na jose mourinho kwenye dili la varane kwa sababu ya smalling ambaye thamani yake ilikuwa ni paundi 10 millioni kama ilivyo kwa varane alipotoka lens ya ufaransa. huu ni mwaka wa saba jamaa kiwango chake hakieleweki wakati varane cv yake ni nzito. media za uingereza zilimjaza ujinga mzee wetu na kama kawaida yake akaonyesha mapenzi yake tena kwa wachezaji wa kiingereza, cha ajabu mimi niliyekuwepo huku nchi za kimasikini njaa kali niliamini ya kwamba smalling aling'arishwa zaidi na mwanadamu kutoka norway ambaye sura yake ilifanana na nemanja vidic muheshimiwa brade hangeland pale fulham.Cha ajabu smalling bado ameendelea kuwa sehemu ya tatizo hata nyakati hizi wakati huo huo tunamyemelea varane kwa dau la zaidi ya 60 millioni paundi.
  3. usajili wa Ashley young kutoka aston villa:nimeanza kumfahamu ashley tokea nipo shule ya msingi kipindi hicho anachezea watford akiwa bado na pumzi za kutosha (kinda), baadae akapiga mpira mwingi sana Aston villa chini ya mwalimu martin o'neill mpaka wakafikia hatua ya kugombania top 4 msimu ulee wa federico macheda alipotuinua kwenye viti dakika za nyongeza, miaka michache mbele ashley young alipoteza muelekeo wa kisoka na alizidiwa kiuwezo hata na steward downing na gabriel agbonlahor. hivi tukiachana na mechi ile tuliyomfunga arsenal magoli 8 ni mechi ipi nyengine ambayo young alionyesha kiwango cha maana akiwa uwanjani? Ashley young ameendelea kuwa ni sehemu ya tatizo kwenye klabu yetu ila cha kustaajabisha mourinho na bosi wake ed woodward wanafanya naye mazungumzo ya kumpa mkataba mpya.
  4. bila ya kuwasahau akina buttner, bebe, anderson, gabriel obertan.
utawala wa david moyes kutoka everton

  • mpaka leo najiuliza ina maana huyu moyes alikuwa haangalii rekodi za mechi za manchester united kabla hajaanza kibarua chake na kwa nini akatumia 30 millioni paundi kwa ajili ya marouanne fellaini, alipokuja manchester david tulikuwa na washambuliaji watatu lakini bwana yule akamleta fellaini awe namba 10 wetu. Fellaini ameendelea kuwa ni sehemu ya tatizo kwenye timu yetu hadi leo hii na hakuna kiongozi yeyote anayejali uchovu wa fellaini.Kocha na mtendaji mkuu anayekwenda na wakati hawezi kumpa mkataba mpya fellaini na hutomuona mchezaji mwenye uwezo kama wa fellaini kwenye timu kubwa isipokuwa manchester united
utawala wa van gaal

  1. huyu mzee ndio kazidisha majanga miaka yake miwili ya kazi, kamleta matteo darmian kwa 15 millioni ambaye hana cha maana alichokileta kwenye klabu yetu.
  2. kamleta morgan schneiderlin kwa 26 millioni paund na yeye amefeli, kamleta blind amefeli, depay pressure kubwa amefeli, di maria pressure kubwa amefeli.
  3. luke shaw baada ya miaka minne kupita kidogo ameanza kuonyesha mwanga wa kuonyesha thamani yake.
utawala wa jose mourinho

hizi zimekuwa ni nyakati za mawakala na viongozi wa timu kujikusanyia fedha nyingi kutokana na mauzo ya wachezaji wenye viwango vya kawaida wanapokuja manchester united. Leo hii tumekuwa hatuna tofauti kubwa sana na madada poa (makahaba) ambao huuza miili yao kwa ajili ya kupata pesa ya mkate na sabuni.
  • makahaba wanawapa wateja wao huduma kwa fedha kidogo japokuwa inasemekana huduma ya amber rutty (sijawahi kuona video yake) inakuwa na dau kubwa wakati manchester united tunatoa fedha nyingi kwa ajili ya kupewa huduma ya mchezaji aisiyetabirika.hawa mawakala akiwemo mino raiola, mendez wanatufanyia uhuni sana kipindi hiki.
usajili wa Fred
Inaumiza sana pale unapo endelea kushuhudia klabu ikiendelea kufanya makosa yenye kujirudia kila panapo funguliwa dirisha la usajili, tumefanya makosa kwa sanchez, lindelof, pogba (105 million pounds), dimaria n.k

Hivi kweli Fred huyu anayezidiwa kimpira na moussa dembele ana thamani ya paundi millioni 55 ?​
United tumepoteza muelekeo kiasi ambacho tunalipa hela ndefu kwa mchezaji ambaye hana uwezo wa kuingia kikosi cha kwanza nyakati hizi, sasa kwa nini tukamsajili au uvumi wa kutaka kuwapokonya tonge manchester city una ukweli ndani yake?

kule klabuni shakhtar donetsk,mchezaji Taras stepanenko alikuwa anacheza kiungo wa chini na fred akawa anacheza nafasi ya kiunganishi cha timu(box to box) wakati huku kwetu anayecheza nafasi hiyo ni paul pogba, kivyovyote fred hawezi kumweka nje paul pogba na vile vile hawezi kumweka nje nemanja matic ili awe kiungo mkabaji.
kocha akiwapanga wote watatu kwa pamoja tunakuwa wazito sana kuwasogelea maadui, ina maana benchi la ufundi walikuwa hawayajui haya?


fedha ya usajili wa fred ilipaswa itumike kwanza kwa ajili ya kumsajili mchezaji atakayetupa faida papo kwa papo hata kama ni mlinzi na si kumsajili mchezaji wa kusubiri mchezaji fulani apate majeruhi ndio apewe nafasi. Tuwatazame manchester city wamelipa paundi millioni 50 kwa ajili ya ryad mahrez ambaye tayari ana uwezo wa kuendana na kasi ya ligi kuu ya uingereza pamoja na mechi kubwa, kiukweli klabu imefanya tena biashara ya kijinga sana na viongozi wa shakhtar wana haki ya kutukejeli kwa kuwapa hela nyingi.

mbona manchester city wamelipa pesa nyingi kwa bernard silva, gundogan, danilo, mendy, jesus na bado wanakaa nje?
ukweli mwengine tusioupenda mashabiki wa manchester united ni kuhusiana na viwango vya wachezaji wetu ukiwalinganisha na wachezaji wa manchester city.
Tumekuwa tukijidanganya na kujiaminisha ya kwamba wachezaji wetu wana viwango sawa na wachezaji na timu nyengine ila tunakosa mwalimu mzuri wa kutengeneza wachezaji wetu wachezae vizuri.
Baada ya kuangalia mechi za msimu huu napingana na wale wanaoamini ya kwamba tuna wachezaji bora kama mancheter city, chelsea,liverpool na timu nyengine kubwa barani ulaya, nusu na robo ya wachezaji wetu wana majina maarufu sana lakini wakiwa uwanjani wapo ovyo kuliko soda aliokunywa bwana harusi wa UDSM.
Wenzetu bado wanaendelea na steji ya kujenga timu ya ushindani ukilinganisha na upande wetu sisi ambao bado tumeendelea kulala usingizi huku tukiringia historia.

bernard silva, gundogan, danilo, mendy wote hao wanapopewa nafasi kikosi cha kwanza wanacheza vizuri sana ukilinganisha na wachezaji wetu tuliowasajili kwa gharama kama vile lukaku, bailly, lindelof.
kwa hali tukiofikia hatuna haki ya kujilinganisha na miamba ya soka la bara la ulaya kama juventus, barcelona, madrid, atletico madrid, man city na hata liverpool.

siku ambayo fred atacheza vizuri nitakuja kumsifia humu ndani ila naogopa kusema iyo siku iko mbali sana.
View attachment 920544
Nilichokuwa nafikir mata akiwepo na fred hamna kinachofanyika lazima mmoja akae bench
 
Mourinho: “He's (Herrera) a player of balance, he's not an incredible creator, not an incredible scorer, he has a little bit of everything but I think he's a player of balance, knowledge, his tactical knowledge is big, he understands what I want, what the team needs.” #mufc [MEN]
kitatokezea kitu gani kama tukiamua kumrudisha eneo la ulinzi wa kati nemanja matic halafu herrera na perreira wakawa wanabadilisha nafasi ya namba 6.
kuna baadhi ya timu si lazima uziwekee walinzi wa nne wa asili
matic amekuwa mzito sana msimu huu kwa kila kitu.
 
Back
Top Bottom