Mi nakubaliana na mashabiki wenzangu wengi kuwa tatizo Pogba analaumiwa sana kwa makosa ambayo siyo yake, Pogba wa Juve na France sio Pogba huyu wa Man Utd.
Akiwa Juve alikuwa anacheza akiwa na Attacking mind hata kwenye midfield anakuwa free sana huku kazi ya kudefend na kuchukua mipira katikati anamuachia Vidal afanye kazi hyo, ndo maana tulikuwa tunamuona anashowcase uwezo wake na skills lakini chini ya Mourinho hicho kitu kimekuwa limited.
Mfumo wa 4-2-3-1 hatakiwi kuwekwa kwenye holding au kudefend position rather anapaswa kuwekwa kwenye front attacking players labda in btwn Martial and Rashford au pembeni kushoto anapopapenda zaidi na anapokuwa free.
Kama mtakumbuka game na Everton tulicheza 4-3-3 mlimuona Pogba alivyokuwa free kwa sababu aliacha kazi ya kudefend akawa anasaidia kupeleka mpira mbele na kushambulia yule ndio Pogba ambaye alikuwa Juve na ndio anakuwa very comfortable kucheza kitu ambacho kwa sasa anashindwa kufanya.
Na hii trend ndo inayofanya wachezaji wazuri Mourinho anagombana nao the like of Ronaldo akati akiwa Madrid, Salah ambaye sasa tunaona alivyo on form, KDB, Casilas na wengine wengi. Mourinho kama kocha anatakiwa abadilike aache kuendekeza mabifu na wachezaji wake hii haisaidii vijana, sisi tumemuuza Depay lakini mnaona moto anaouwasha huko Lyon. Last season Herrera alikuwa mhimili wa Midfield lakini mwaka huu mchizi kamuweka Benchi bila sababu yoyote tusipoangalia na yeye tunaweza kumpoteza.
View attachment 696546