Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Sifa ya mwisho;
Wana dozi mirembe kama wewe.
Mnaoshangilia uuzwaji wa jezi na historia wakati wengine wanashangilia makombe na mataji.
Kama ni historia ya makombe milan kawaacha kusikojulikana.
Sidhani kama kuna ambaye anamwogopa milan sasa.

MASHABIKI WA MAN U NIMECHONGA MIKOKOTENI
MUHINDI AKIWAFILISI MKUJE MSUKUME MPATE MUMUPELEKEE TENA ALIPIE MISHAHARA
 
jinsia yako please
halafu hapo mwisho unaposema hatuwezi kupambana na city wew ndio unaweza kupambana nao
Mbona unaanza matusi
Mbona mijishipa inaanza kukutoka shingoni na kama unataka kulia hivi
Huo ndo ukweli na utabaki kuwa ukweli
Ukimind njoo unipige nipo zangu hapa mtongani kituoni nakungoja
 
Ndugu punguza hasira, kwani wewe ni shabiki wa timu gani,?
 
Yule mzungu aliyekuwa kocha wa Azam aliwahi sema kuwa, kwa Tanzania hata mkata maua anaweza kukosoa mbinu ya mwalimu wa soka anayoitumia uwanjani.
 
Manchester United imekwaa kisiki kupata saini ya mchezaji nyota wa Chelsea Willian katika usajili wa dirisha dogo Januari, mwakani.

Mchezaji huyo wa kimataifa wa Brazil, alisema kuwa hana mpango wa kutimka Chelsea na amewataka mashabiki wa klabu hiyo kumuunga mkono.

Man United ilikuwa na matumaini ya kupata saini ya mchezaji huyo ili kwenda kuimarisha kikosi hicho.

Jose Mourinho alirusha ndoano akidai Willian ni mchezaji bora mwenye sifa za kucheza Man United.

William anayetamba katika kikosi cha kwanza kwa Mtaliano Antonio Conte, alisema hana mpango wa kuhama Chelsea na amewataka mashabiki wa klabu hiku kumsapoti.

Awali, ziliibuka tetesi kuwa mchezaji huyo amekubali kutua Old Trafford katika dirisha dogo kabla ya kujitokeza hadharani kukana taarifa hiyo.

“Siku zote nimekuwa na furaha Chelsea. Naipenda sana klabu hii kwa roho moja, siwezi kuondoka naomba mashabiki watulie wanipe ushirikiano,” alisema Willian.

Willian mwenye miaka 29, alifunga bao la kwanza katika mchezo wa Ligi Kuu England walioshinda mabao 3-1 dhidi ya Huddersfield.
 
Kocha wa Manchester United, Jose Mouriho ameingia hofu ya kumpoteza libero wake Eric Bailly mwenye maumivu ya kifundo cha mguu.

Mourinho alidokeza Bailly anatakiwa kufanyiwa uchunguzi wa kina kubaini ukubwa wa jeraha hilo ambalo linaweza kupunguza kasi ya Man United.

Man United inachuana vikali kuwania ubingwa wa Ligi Kuu England msimu huu dhidi ya mahasimu wake Manchester City inayoongoza kwa pointi 46.

Mourinho alisema kuwa endapo beki huyo wa kimataifa wa Ivory Coast hatapata matibabu ya kina, anaweza kupata matatizo makubwa siku za usoni.

Bailly aliyeumia wakati akiitumikia timu ya taifa ya Ivory Coast katika mashindano ya kimataifa, amekosa mechi nane za Man United kutokana na jeraha.

“Nadhani ana tatizo kubwa. Tunapambana ili apate matibabu ya kina, lakini tunaangalia kama anaweza kufanyiwa upasuaji baada ya kupata taarifa ya daktari,” alisema Mourinho.

Mourinho alisema hawezi kutabiri kama beki huyo anaweza kukosa mechi zote zilizobaki na ametoa nafasi kwa daktari kuendelea na uchunguzi.

Man United inaendelea kuwatumia mabeki wa kati Chris Smalling, Phil Jones au Victor Linderlof aliyesajiliwa na klabu hiyo majira ya kiangazi msimu uliopita.
 
Mbona unaanza matusi
Mbona mijishipa inaanza kukutoka shingoni na kama unataka kulia hivi
Huo ndo ukweli na utabaki kuwa ukweli
Ukimind njoo unipige nipo zangu hapa mtongani kituoni nakungoja
Unaweza kuniambia ni wapi alipoandia matusi?? Jiangalie bwana mdogo, Usikurupuke.
 


Mkuu Jose wa Chelsea, Real ....... ni yule yule wa kupaki bus.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…