Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Yeah...
City cannot sustain this pace until May..!
What about you then..!?
 
Sasa unamlaumu lukaku wakati team imejifia iyo tatizo la Manchester United ni mourinho akicheza na team ndogo anafunguka akicheza na team kubwa anakimbilia ubarazani shenzi kabisa mwambieni kocha afanye usajili mzuri beki ya kati na pembeni maana akiumia eric baily hakuna kitu uko nyuma na uyo a young atafutiwe no huko kushoto amwachie mtu anaetumia mguu huo lukaku kafunga magoal mengi mwnzo wa league ila saiv hana watu wa kumlisha au fab yupo united?
 
Hakuna haja ya kulaumu mchezaji hata mmoja, wakulaumiwa ni kocha kwa falsafa yake anayoitumia tunapocheza na timu kubwa. Mimi naamini kwa wachezaji waliopo pale Man U wakipewa uhuru wa kucheza wanaweza kushindana na kuifunga timu yotote ile hapa duniani. Tatizo ni kwamba timu inapocheza na timu kubwa timu yetu inageuzwa underdog kwa mfumo wa ulindaji zaidi ambao kocha anawaelekeza wachezaji. Lukaku anaachwa mbele peke yake acheze na maadui wawili hadi watatu na gap kati yake na viungo linakuwa kubwa sana kwa sababu timu nzima inapaswa ikae nyuma, mwisho wa siku mipira ya kumfikia lukaku mingi ni ile ya kubutuliwa na kipa tu.
 
Kweli chifu, nyakati zingine tunasahau kwamba jamaa is only 24! Tony naye ni 22, Rashford ni 21....sioni kwanini mtu awe pessimistic!!

Na sielewi kwanini watu wanashindwa kuona game ya leo kutokuwepo kwa Pogba kumechangia sana.
 
Kwa hiyo alivyoifunga Gooners ulisema hivyo hivyo?
 

Mata katumia dakika 5 kumfanya lukaku awe na shorts on target moja binafs naiman kubwa na lukaku kukosa namba 10 kunamfanya aonekane mbaya kwa nn mata akae bench wakat city wenyewe walikuwa waoga?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…