Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Tetesi
MAN UTD WANAMTAKA SAUL


Manchester United wanataka kumsajili kiungo wa Atletico Madrid Saul Niguez, ambaye dau la euro milioni 150 litahitajika kuvunja mkataba wake, kwa mujibu wa The Sun .
Jose Mourinho anataka kuongeza ubunifu kwenye kikosi chake na anatamani kumwongeza Saul kwenye timu yake majira ya joto msimu ujao.
 
RONALDO ANATAKA KUONDOKA REAL


Cristiano Ronaldo anataka kuondoka Real Madrid, kwa mujibu wa habari za bomshell kutoka Chiringuito TV Hispania.
Mchezaji huyo wa kimataifa wa Ureno amekuwa katika kiwango kibovu miezi ya hivi karibuni, akifunga goli moja tu La Liga hadi sasa.
Inaaminika Ronaldo yupo tayari kuondoka ifikapo Juni 30, baada ya kukataa mkataba mpya Santiago Bernabeu.
 
Tetesi
ARSENAL WANAMTAKA FELLAINI


Arsenal wameugeuzia moyo wao kwa kiungo mahiri wa Manchester United Marouane Fellaini, Calciomercato limeripoti.
Mbelgiji huyo yupo kwenye mwaka wa mwisho wa mkataba wake Old Trafford, pia amekuwa akiivutia Besiktas ya Uturuki.
 
Manchester United wako tayari kumruhusu Marouane Fellaini kuondoka klabu hiyo bila malipo mwishoni mwa msimu huu kuliko kumuuza kiungo huyo wa kati mwezi Januari.
Mkataba wa Fellaini unakamilika tarehe 30 mwezi Juni na United walianza mazugumzo na Mbelgiji huyo kuhusiana na mkataba mpya msimu uliopita, hadi sasa hakujaonekana makubaliano ya aina yoyote hadi sasa.
Kiungo huyo wa miaka 29, aliikataa ofa ya karibuni zaidi kutoka kwaUnited mwezi Septemba.
Fellaini aliyejiunga na United kwa kima cha £27m mwezi Agosti alikuwa miongoni wa wachezaji bora kujiunga na United meneja David Moyes alipochukua hatamu.
Inafahamika kwamba Fellaini aliamua kuachia bonasi ya £4m ili kuhakikisha uhamisho wake unafaulu.
Thamani yake kwa klabu ya United imeshuka na pia hapendwi tena na mashabiki. Alizomwa na mashabiki wa klabu hiyo mwezi Disemba 2016 alipokuwa akipasha misuli yake moto kuingia uwanjani kama nguvu mpya walipokuwa wakikabiliana na Tottenham katika uwanja wa Old Trafford.
 
Hata hivyo, tangu hapo, Fellaini ameongeza umahiri wake.
Alifunga bao katika nusu fainali ya ligi ya Uropa dhidi ya Celta Vigo na pia kuanza waliposhinda 2-0 dhidi ya Ajax kwenye fainali.
Fellaini hapo awali alihusishwa na kutaka kuihamia Galatasaray msimu wa majira ya joto.
Lakini Meneja wa United Jose Mourinho alisema klabu ya Uturuki ilikuwa na nafasi nzuri sana ya kumsaini yeye mwenyewe kuliko Fellaini.
Fellaini alikosa kushiriki mechi nyengine msimu huu kutoka na jeraha lakini amefunga magoli manne kwenye mechi tisa alizoshiriki.
Inaaminika kwamba Fellaini amekuwa na uhusiano mwema na Mourinho, jambo ambalo huenda likawa muhimu katika kuamua mustakabali wa mchezaji huyo.
 
Mshambuliaji wa Manchester United Romelu Lukaku amekuwa mchezaji wa Ubelgiji ambaye ameweka rekodi ya ufungaji mabao mengi kwa timu ya taifa hilo.
Vijana hao wa Roberto Martinez waliifunga Japan bao 1-0 huko Brugge.
Lukaku , 24, alifunga goli la 31 kwa nchi yake pale alipomalizia krosi safi kutoka kwa Nacer Chadli aliyoiingiza wavuni kwa kutumia kichwa.
Lukaku alikuwa ametoshana na Bernard Voorhoof na Paul van Himst walipokuwa na magoli 30 kila mmoja wiki iliyopita.
Ubelgiji waliendeleza msururu wao wa kutoshindwa hadi mechi 15.
 
Marcos Rojo: "Tomorrow I am going to play a match with the reserves in a friendly match. I feel good. Up until now I have not had any problems but training is not the same as a match so I will play 45 minutes tomorrow for the reserves." [HASHTAG]#MUFC[/HASHTAG]
 
A.Martial on his relationship with Jose: “He’s hard with all of us and he is hard with me, there is no question. But I know that it’s for my benefit. But I also know that he really likes me as a person, so there’s no issue about the discipline being for the wrong reasons.” [HASHTAG]#MUFC[/HASHTAG]
 
AM: “But the objective, of course, is to have all of us in good condition, and being fit to play every match and that is what I’m hoping to do. He knows my strengths & my weaknesses, such as they are, but the outcome is that we are learning to give everything in the right way.”
 
De Gea: "I think that the players who leave Spain are not paid as much attention as those who stay in Spain. And people tend to forget about us a little. The English culture cares for and loves its players a lot." [HASHTAG]#MUFC[/HASHTAG]
 
UTD
 

Attachments

  • IMG_20171116_001955.jpg
    IMG_20171116_001955.jpg
    93.2 KB · Views: 54
  • IMG_20171116_001858.jpg
    IMG_20171116_001858.jpg
    52.6 KB · Views: 54
  • IMG_20171116_001854.jpg
    IMG_20171116_001854.jpg
    69.2 KB · Views: 55
  • IMG_20171116_001846.jpg
    IMG_20171116_001846.jpg
    48.7 KB · Views: 56
Back
Top Bottom