Hata wachezaji ambao tunawaona ni bora duniani (Messi na Ronaldo) wakienda kucheza Everton wanaweza kuwa na wakati mgumu kutoa msaada pale timu itakapozidiwa. Why? Kwa sababu kuna tofauti kubwa sana ya strength ya vikosi wanavyochezea wachezaji hawa.
Madrid wana uwezo mkubwa wa kikosi kuliko Everton, hivyo wanaweza kubadilisha mchezo kirahisi kuliko Everton.
Binafsi sijawahi kuona mechi ambayo Madrid amezidiwa halafu Morata ndo akawa msaada kwa team.
So, Lukaku akija kwetu (until it's official), nyuma yake atakua na viungo tofauti na wale wa Everton, atakua na viungo hatari zaidi ya alipotoka hivyo hata tema ikizidiwa, still hao viungo ndo watakaofanya yeye aonekane msaada.
Kumbuka mchezaji mmoja tu hawezi kufanya kila kitu uwanjani, lazima chemistry ya team nzima ifanye kazi.