Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Msimu utakua mgumu sana na wakuvutia sana. Usajili utakaofanyika ndio itakua pona ya timu.
Je unaamini katika usajiri tu ndiyo mkombozi?! Vipi kwa timu kama Tottenham ikiwa na vijana hodari na machachali na msimu uliopita walianza tengeneza chemestry na ilionekana ambayo mimi naiona ndiyo bora je wasipo ingia katika soko la usajiri wataweza teteleka msimu huu? Ikiwa bado ilikuwa na mtaji wa vijana wao ambapo kwangu kama yasingekuwa majeraha nilianza kumuona MARCELO wa EPL yaani Dany Rose pamoja LAMELA je unaweza iweka nafasi ipi timu kama hii.?
 
Naijua Man Utd haiwezi kurudi level itachukua miaka hata kumi au zaidi. Kwani nyota kusajiliwa ni tatizo. Kama ni biashara hata arsenal wanafanya hawana loss wamejaza pesa tu jiulize nini kinafanyika. Itabaki story tu.
 

Bila ya kuongeza nguvu Totenham haitoweza kuchukua ubingwa,lazima wasajili lakini sidhani kama watasajili mchezaji wa gharama kwasababu wanamalizia uwanja wao.
Labda wakimuuza Walker watapata pesa ya kusajili.
Kwenye kuchukua ubingwa,hilo sahau. Hawana kikosi cha kuchukua ubingwa,wao wataendelea kuleta presha kama misimu mingine tu.
 
Hivi ni soko limebadirika ama uwezo maana dah SANCHEZ anamjambisha Wenger anataka 400 kwa wiki. Lemar uhamisho wake wanataka 80 dah.!
Hali ya Soko limebadilika sana siku za hivi karibuni,hii ni kutokana na uwepo wa Mawakala wa Michezo ambao wao huang alia Zaidi pesa kuliko uwezo wa Mchezaji,lakini vile vile hali hii huakisiwa na ongezeko la Mapato yanayopatikana kutokana na mchezo wa Mpira wa Miguu,mara nyingi timu hufaidika Zaidi kuliko mchezaji ndio mana hawa akina CR7 na Mwenzake Messi wamelibadilisha sana soko la Ulaya la Mpira wa Miguu kwa kulifanya kuwa la biashara Zaidi kwa kila wanachokifanya na hii kupelekea mawakala nao kuanza kuzipiga timu kupitia kwa wachezaji wao.

Let's imagine kwenye dunia ya sasa unadhani Zidane angeuzwa kwa kiasi gani?Ronaldinho?

Leo hii Lukaku anapatikana sokoni kwa 75,hazard 85,Morrata 80 na e.t.c

Gareth Bale alinunuliwa sijui kwa 80+ aaaah na hawa Marais wa Vilabu pia wanachangia kuharibu soko la Ulaya.

Soon nadhani UEFA na FIFA watapitia upya hili soko na kuunda chombo kwa ajili ya kuregulate soko la wachezaji Ulaya ili kubalance timu mana ni wababe na vilabu vyenye uwezo ndio wanaoweza kununua world class players pekee timu nyingine zitachemka so kunaweza kutengenezwa kizazi cha timu 5 au 4 Ulaya ambao ndio watakaoweza kutwaa makombe.

Na hii now tunaiona kwenye League za Spanish,Ufaransa,Ujerumaini na Italy ambazo ni mbili au moja ndio zinazoshinda makombe.

England ni kwa sababu ya timu nyingi kuwa na pesa ndio zinazosababisha ubingwa kutokutulia mahala pamoja.

Wachezaji wamekuwa wakilipwa mishahara mikubwa na kuwa na mikataba yenye thamani kubwa,hizi pesa kwemye Mpira saa nyingine ni kufuru.

Leo Mess analipwa mshahara wa us Dollar 400 kwa wiki,Ronaldo 350,Rooney 300 bila mapato yao binafsi.

Huu Mshahara wa Mess unaweza kuwalipa wachezaji wote wa Bantley pale England au au Betis kwao Spain.
 
Rooney first touch was and is still awful but that deficiency never fetters him from becoming Manutd legend.

Why?

His goals made him a legend and so will Lukaku be if he scores 25+ a season for Manutd
 
Mashabiki hela siyo sheda bali kufungwa hutuachia simanzi nzito
 
Naijua Man Utd haiwezi kurudi level itachukua miaka hata kumi au zaidi. Kwani nyota kusajiliwa ni tatizo. Kama ni biashara hata arsenal wanafanya hawana loss wamejaza pesa tu jiulize nini kinafanyika. Itabaki story tu.
Bro unaongea kama shabiki wa Mpira anayeujuwa mpira au unataka tujaze Sever tu hapa,any way kwa faida yako na wengine acha tuendelee na mjadala na hivi leo ni sabasaba so we're free.

Mafanikio ya Timu Yeyote yanategemea Vitu Vinne, Moja historia au ukubwa wa timu kiasili sifa hii nadhani timu hizi zote mbili zinazo Liverpool ndio wanaongoza kuchukua UEFA champion Zaidi ya Man U lakini wakifatiwa na Man United lakini katika historia Man United ndio mbabe kwa kuchukua makombe pale EPL,mbili uwezo wa kocha kwa misimu Zaidi ya mitatu tulikosa World class kocha,Moyes hakuwa top cocher duniani wakati anasajiliwa kuja kufundisha Man United,uwezo wa wachezaji binafsi,baada ya Ufalme wa Sir Fegurson ambaye aliweza kuwatengeneza wachazaji wa kuwa kuja kuwa World Class top player,aliopondoka waliomfatia walishindwa kuwa na uwezo huu na kufanya kuona vipaji halisi vya wachezaji wetu, na thamani ya timu katika kuvutia Wawekezaji, kulipa na kununua wachezaji wapya Wenye uwezo,Moyes na Van Gaal hakujuwa ukubwa wa Man United hawajuijuwa thamani halisi ya Man United na ndio mana uliona usajili wa kwanza wa Mou na Wenye thamani ni kumchukua Fellain ambaye hakuwa mchezaji Mkubwa Ulaya.

Van Gaal yeye katika utawala wake aliuza wachezaji wengi wazuri kama Chicharito na kutuletea wapaka Poda wake.

Any way tulikuwa ni kipindi cha Mapito na Mabadiliko now timu ipo kwa kocha mwenye kujuwa Vyote hivi na nzuri Zaidi anajuwa Kiu ya Mashabiki wake.

Bodi ya Man United inakiri kuwa ilifanya makosa makubwa sana kukubali timu kuachiwa Moyes na ndio tulipoanza kuyumba,Van gaal ni top class kocha alitusaidia kutengeneza barabara lakini alipishana na Falsafa ya timu.

Sasa Mou ni mtu sahihi pale Man United anaendana na Falsafa ya timu,ni kocha Mkubwa hivyo anahitaji na timu iwe kubwa na ndio mana aliweza fanya usajili wa uhakika na Mkubwa kurudisha hadhi ya Club Yetu.

Asernal wanakosa baadhi ya Sifa hapo kaka,Asernal sio timu kubwa Ulaya ni timu kubwa England so sio vizuri kuifananisha na Man United,Yes wanafanya vizuri sokoni lakini sio timu yenye kulipa wachezaji mishahara mikubwa sio Wenye kutoa pesa ndefu kwenye usajili.

Asernal imesajili nadhani ni wachezaji wawili top class players kwa misimu miwili ya hivi karibuni lakini sio timu kubwa kuifananisha na Man United na ndio mana wanakosa mbinu za kuchukua makombe.

Nimekwambia tumerudi katika ukubwa wetu au Level Yetu, Man United ni Mabingwa wa Uropa Legue,Kombe kubwa la pili bara ni Ulaya sasa hiyo miaka kumi ipi unayosema.

Kutwaa EPL msimu wa 2017/2018 tusubiri sina shaka na hili,mana hata msimu uliopita zile droo zingebadilika tungeongea mengine.
 
Haiko hivyo
Kupanda kwa dau la TV rights ni ubora wa EPL siyo gharama za uendeshaji kupanda

Ila gharama za uendeshaji zimepanda kutokana na mapato ya TV rights kupanda na kupaaisha matarajio ya wauzaji wachezaji ya kuwa timu za EPL wanazo....they can afford to pay those crazy fees

Ila ubora wa ligi ya EPL ukishuka basi na TV rights zitashuka na madau ya usajili, mishahara ya wachezaji kuporomoka

Madau pia yanapanda kwa sababu makocha hawataki kuwaamini wachezaji mahiri nje ya European ligi wakati Africa na South America kuna vipaji vingi lakini EPL hawawataki kwa madai hawana European experience

Timu ndogo za EPL nazo hukosea kuhangaika na kusaili wa kwao kwa madau makubwa mwishowe hufilisika kumbuka LEEDS UNITED wako wapi leo

Nionavyo, umiliki wa hizi timu utachukuliwa na mabilionea vinginevyo uendeshaji wake tuendako hata hizo TV rights, udhamini, mapato ya milangoni n.k hazitafua dafu na mishahara na tozo za usajili zitaendelea kuwa juu ya bei stahiki za soko
 
Ni kweli lakini angalia ni kwenye mechi zipi kapata magoli mengi...yeye sio day to day scorer...akiwakuta vibonde anawanywa goli za kutosha...mechi za maana haonekani kabisa
Mind you still tuna UCL ambako ni league ya wakali tu wa ulaya
Musimu uliopita tulipoteza pointi nyingi na timu ndogo na Lukaku ni mahiri wa kucheka na nyavu zao na hilo Mourhnio kalipa uzito stahili
 
Weka haya maneno rehani khalafu musimu utakapokwisha jipime mwezi wa tano mwakani
 
Rashford ni msimu wake wa pili.

Msimu wa kwanza (2015/16) kacheza mechi 11 kafunga goli 5.

Msimu wa pili (2016/17) kacheza mechi 32 (16 sub) kafunga tena goli 5.

Lukaku kuanzia 2012 yuko juu ya goli 15 kutoa 2014/15 alikuwa na goli 10.
Hizi ndizo takwimu za kuzingatia
 
Subiri hizo droo zibadilike muone mengine maana umeandika kama unapiga ramli. Mambo mengi ni ya kufikirika.
Umejaza maneno mengi ya kufikirika huyo kocha kafukuzwa alikotoka subiri mtamfukuza muda si mrefu.
 

Mkuu kama nakumbuka vizuri, msimu ulioisha timu zote kuanzia Chelsea hadi Sunderland walilipwa Pound Million 98 kama TV rights.
Sasa hapa sijaelewa Sunderland ilikuwaje wakapata mgao sawa na Man Utd wakati wao wana Defoe tu (At least)
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…