Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Teh teh tukizungumzia ushindi kwenye mpira MAN U kaeni pembeni. THE BLUES KWANZA
 
Unaweza kuwa ni mapema mno kusema! Lakini Mou have to go, ameharibu timu kabisa, mbinu zake za kizee za kulinda goli na sub ya Fellaini mcheza foul mkubwa zimetukosesha ushindi. Sitaki Mou, aende zake.
Nani aje
 
Mr akiwa hana uwezo wa kukupa mimba na hana tiba chepuka ukipata mtoto bambikiza tu utafanyaje? Njoo huku hutaki on a sasa
 
Arsenal walipotoa draw vs Man Utd, Mourinho alisema alitamani angekuwa na a tall player on the bench hasa Fellaini angesaidia kulinda ushindi. Leo Fellaini aliletwa kulinda ushindi badala yake ameua ushindi.
Mpaka Leo umeshindwa kumuelewa huyu jamaa ni MTU wa chai
 
Kaka sio kabila hiyo
 
Nashindwa hata namna ya kuelezea game ya jana zaidi ya hasira juu ya hasira.Mipango ya Jose kipindi cha pili ilikuwa mibovu labda tungesema kosa lake kubwa lilikuwa ukosefu wa uzoefu lakini hapana Jose ana uzoefu mkubwa katika soka kafundisha clubs nyingi kubwa.

Tatizo la Man ni kumtegemea sana Zlatan kupita kiasi,unaweza kusifu bao lake la jana lakini ukitazama dakika 90 alikuwa akifanya nini uwanjani unabaki kushangaa,hana uwezo wa kukaa na mpira,hana uwezo wa kupunguza mabeki,hana uwezo wa kukimbizana labda angeenda Seria A angefanya maajabu lakini si EPL.Man inajengwa around Zlatan nadhani ni kosa kubwa sana tena kubwa sana kwasababu huyu ni mchezaji mwenye umri mkubwa sana 36 anakwenda 37 muda si mrefu.Nashangaa Jose anamhitaji msimu ujao huu ni upimbi wa kupitiliza.

Sijui kwanini Mata hakuwemo katika kikosi cha jana,nasema sijui kama yupo mnazi wa Man tafadhali anisaidie maelezo mazuri yaliyo nyooka na si vinginevyo.Mechi ya jana Rooney alikuwa anatumikia adhabu yake Mata alitakiwa sana hii tabia ya Jose kupenda michezaji mirefu imepitwa na wakati kabisa na sioni akibadilika hata kiduchu sana sana namwona akizidi kuishiwa mipang kadri siku zinavyosonga mbele.

Gap baina yetu na top 4 inazidi kupanuka siku hadi siku.Mipango ya kucheza mipira ya kuzuia hata kwa timu kama Evaton inazidi kunichosha kabisa.Sub za jana zilituangusha sana kati ya michezo sita au saba mechi ya jana ilikubwa mbovu sana hasa kipindi cha pili.

Ifike wakati Jose atengeneze timu ya miaka 3 hadi 5 ijayo lazima umri wa wachezaji anaotaka kusajili wafit katika mipango ya MAN na si mipango yake ya muda mfupi.
 

1.Goli la Ibra, narudia kuwa sija discredit goli lake ila nasema, goli lilitokana na Keepers error zaidi rather than ufundi binafsi wa mchezaji. Najua wewe ni muangaliaj mpira mzuri lakini unavo yachambua magoli ujue kuna vitu kama
Individual error au skills
Team error au skill
Communication error au skills

Kufunga goli kuta taka mfungaji awe na skills , kufungwa goli kuta taka mfungwaji afanye error. Sasa kuna time error % ina zidi skill % au vice versa, kazi kwako ni kuchambua kipi kili zidi kipi. ukitaka nitafute nikupe kitabu hiki usome.
'44 Secrets for Great Soccer Goal Scoring Skills' kimeandikwa na Mirsad Harsic. Huta pata tatizo la ku mpa credit mfungaji au mfungwaji wa goli.

2. Basti na Schneiderln, sija sema waanze au wacheze dakika zote tisini, kama uliona mchezo wa jana utajua wali hitajika wao kuliko Fellaini. So jana tu mechi ya stoke na Arsenal pia mtu kama Basti ali hitajika.

3. Yeye ndio kocha, yeye ndio kiongozi, hivo lawama ata pewa yeye kuliko wachezaji, ahakikishaje morali ni jambo ambalo hata kocha wa level 1 hufundishwa, kuna kitu kinaitwa sports psychology mkuu ni moja ya foundation course za ukocha. Kwa nini Mou aliondoka Madrid next year Anceloti akaja kubeba UEFA? Kwa nini Mou aliiacha pabaya Chelsea lakini Conte na Hiddink walijitahidi!? Tena wakicheza na vikosi almost hivo hivo alivo viacha Morinho!? Tatizo Siyo teknik tuu, hata suala la saikolojia ya wachezj lina husika.
Kama Mou hajui afanye nini ili morali iongezeke bas ndio ana stahili kufukuzwa.

5. Ukiweka hicho kitu kinacho itwa exceptional treatment bas ukifanye kwa exceptional player ambaye ni kweli some tyme single handedly ana ibeba timu, ila si Ibra na Pogba, they are just equal with other players kwa viwango wanavo onesha sasa, haina haja ya special treatment kwao. Part of being good coach is being fair kwa sasa pale man u ili kuwa fair lazima awa treat wote kama equals. Umesema kila timu lazima kuwa na superstar anaye treatiwa tofauti
Messi kwa Barca Yes
Ozil kwa Arsenl yes
Ronaldo kwa Madrid yes
Man u hatuna hata mmoja wa aina hiyo tunajidanganya hapo. Na Mou ana fanya kosa la kuwaza kama wewe unavo waza.

5. Nakubali kuwa alikiwa majeruhi lakini alisha pona mechi 3 au 4 kabla ya jana, yet alikiwa hapangwi, nakubali kuwa at leat mechi mbili za mwisho kapangwa aendelee hivo hivo.

Wewe huwezi kunielewa kama unaingiza mitazamo yako ya ki personal, mfano mimi i have never seen a fan who think knows man utd in the sense of being arrogant as you! Uwa unajiskia kama wewe ndio shabiki bora hivi, unaijua timu vzuri unaujua utamaduni wa utd vizuri, wakat uko Tandale tu kama sisi wengine. Unajihisi ni shabiki mzuri mpaka unataka wengine tuwe kama wewe. Lakini sija wahi ingiza bias zangu kwenye comments zako, nyingine huwa nzuri tuu na huwa na kubali unapokuwa upo sahihi. Ukitaka kuwa ratianal pungiza kujiona wewe ndio kilanja wa mashabiki wa utd, sikiliza maoni ya kila mtu na usitake kila mtu awe kama wewe, halafu nakushauri soma majarida mbali.mbali ya soka, nenda hata you tube uangalie tekniks mbali mbali we mpira unajua ila kuna ki ji elim flan hivi unakikosa.

Am not bitter, natoa na data zangu, tungekuwa wa Pili kwenye ligi, data zingekiwa vizuri si ajabu ningekuwa namsifia hapa Kocha, lakini hali yetu si nzuri na haitii matumaini so lazima niseme. Na expect hatutaingiza mitazamo binafsi juu yetu ili mazungumzo yetu yawe na maelewano.
 
Tutaongea sana lakini United ina matatizo makubwa mawili. Kwanza Kocha. Pili wachezaji. Tatizo la kocha hajui ni wakati gani mchezaji gani anafaa acheze kwa nafasi ipi na kwa lengo lipi. Kila siku anabadili. Wanaokaa bench unashangaa kwanini hawapati minutes?? Tatizo la wachezaji ni uwezo mfano Zlatan ni mzigo hakuna lolote. Not skillful not fast not possessive. Wachezaji walio wengi uwezo binafsi uko low. With exception to Carrick, De Gea , Hererra na Mata. Wings hazipenetrate na overall ball possession is poor. Fellaini anatakiwa atoke kabisa United. Useless.
 
Unajua kwa nini SAF alikuwa kocha bora alikuwa na less talent na aliweza ku utilize.
Talent wise Ibra na pogba, Mikhi na Baily wame add depth kubwa kuliko aiyo kuwa nayo LvG, ambayo ingebidi mou ajue namna ya kuitumia ili ilete matokeo.
Kina RvP walikuwa ndio wako kwenye viwango vibovu kweli kwa wakat wao kipindi cha LvG. So bado LvG alikuwa na less talent heck hakufanya vibaya sana
Jf mi nimeingia mwaka huu huu lakin mpira nimeanza kuangalia kitambo
 
Mkubwa Fella alichokifanya jana amenikumbusha Phil Nevill alipokuwa anakipiga Everton game ngumu km zile matukio km ya yale yalikuwa ya kawaida ndani ya box ya everton na kutupatia Gift inshort Fella jana amewepa offer masela wake wa everton inaweza kuwa makusud au bahati mbaya
 
nimependa maelezo yako.mimi huwa kila siku najiuliza kitatokea kitu gani kama kocha atamtumia mata pamoja na mkhityaran kwa pamoja.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…