Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Tatizo sio Pogba, tatizo ni Rooney na Fellaini.

Rooney anamzuia Pogba kutawala sehemu ya kiungo kwa kurudirudi nyuma na Fellaini amenuiziwa na David Moyes.

Hakuna sababu ya kuwapanga Rooney na Pogba kwenye first X1

Pogba hayuko huru.
Tatizo Mou analazimisha timu iwe ya kiingereza kwa kuwaridhisha waingereza kumchezeaha Rooney, hiyo ni namba ya Pogba anayomlazimisha Rooney acheze, Rooney ni striker na bahati mbaya Ibracadabra is far better than Rooney, which means Rooney anatakiwa awe bench, hili ni tatizo mojawapo litaloingarimu Manu.
 
Fellain ndio mchezaji bora kwenye viungo wa United,Tatizo kubwa leo lillikuwa Rooney na Pogba

Nnafahamu hilo ila Fellaini ana tatizo ka nidhamu.

Baada ya Juan Zuniga kufunga goli la pili akaenda kumkwatua.

Baadae amesababisha penalty.

Nimekuwa nikimwangalia Fellaini tangu akiwa Everton na hata timu ya nchi yake ya Belgium.

Mwaka 2014 Fellaini alitajwa kuwa ni mmoja wa worst signings of the season in England.

Fuatilia idadi ya kadi alizo nazo na namba ya suspensions ndiyo utaelewa.

Msimu wake wa kwanza England akichezea Everton Fellaini alipewa kadi mara 10 katika mechi 17 na ikabidi akutane na meneja wa waamuzi kuzungumzia hali hiyo na akaapa kujirekebisha ingawa baada ya mkutano huo alipewa kadi zingine 3 katika mechi 16 alizocheza hivyo kuonyesha improvement.
 
Khe kheee kheeeeee kheeeeeeeeee poleni sana humu. You have been POGBA again by Watford.
 
1474205460781.png
 
Fellain ndio mchezaji bora kwenye viungo wa United,Tatizo kubwa leo lillikuwa Rooney na Pogba
hata mie nakubaliana na wewe kuhusu Fellaini watu wanamchukia ila jamaa ndio anayeweka kidogo matumaini hasa ndani ya Box Cross yeye na Ibra, Herera angekuwa mkabaji then Pogba asogee mbele, Fellaini hasa ikifika dk za mashambulio ya Cross beki wengi wanapata tabu. Rooney ndio tatizo na Rashford si wa kucheza kulia ni kutoka kushoto japo leo alipiga cross nzuri upande wa kulia.
 
Timu inapiga pasi za nyuma sana hakuna killer passes inawalazimu washambuliaji kurudi nyuma kutafuta mipira ila bado mapema sana nafikiri kocha bado anatafuta Muunganiko mzuri wa timu.

Kwa gemu ambazo hazina Tempo kubwa nafikiri ni muhimu CARRICK awe anaanza kwani ni mzuri kwa kusukuma mipira mbele na yuko sharp na kwa gemu za Kukaba Fellaini awe anaanza shida ya Fellani apeleke timu mbele na ivyo husababisha timu kushambuliwa sana...

Bado mapema mapambano yanaendelea.
 
Back
Top Bottom