Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Ni kweli kabisa mkuu Leo arsenal walikua wameingia kwenye mfumo, saivi timu inacheza na unaona kabisa kuwa kocha. Ruben ana ibadilisha timu taratibu, lakini watu wana taka yale yale ya shaolin monk 10hag. Leo unashinda kwa timu kubwa alafu kesho na kesho na keshokutwa unashenyentwa mfululizo mpaka upate tena bahati ya kushinda huku mfumo unaocheza haueleweki na hauna kikosi cha kwanza 1 chenye wachezaji wanaoelewana vizuri kwenye pitch.
 
Ndio Mshagongwa Sasa
 
Kwa kutumia akili ya kawaida kabisa leo hatukuwa tunaingia uwanjani kushindana na arsenal bali wengi wetu tulitaka kuona positivity kwenye kikosi chetu ukilinganisha na msimu jana. Mambo chnya leo uwanjani yalikuwa mengi sana kuliko hasi.
Kama uchezaji utakuwa huu mechi hadi mechi, basi ni suala la muda tu timu itashika momentum na wapinzani hawatakuja kizembe tena dhidi yetu.
Ugarte sijui Uruguayan wa wapi huyu jamaa, ni heri auzwe yeye tubaki na casemiro kama squad player.

Nmauombea Shaw uimara wa mwili walau acheze mechi 25 za msimu, huyu anajua sana kuzuia ujinga wa akina Saka.
Yoro kama naanza kumuelewa vile, ila Mbeumo na Cunha ni tracker wazuri sana upande wa mapana ya uwanja.

Mechi inayofuata tutaona zaidi kama timu imeamka au ni wenge la arteta boys limetuweka kwenye ramani.
 
Shaw ni mchezaji smart sana ana utulivu sana akiwa na mpira hana pala pala ila Yoro naona changamoto yake kubwa akiwa na mpira hasa kwenye maeneo ambaye kuna pressure anakua kama ana hofu ivi
 
Sesko alisajiliwa lini mpaka kashindwa kufunga pre season?
Sesko kaingia na Amad lakini Diallo, Ugarte kakiwasha kuliko huyu Tapeli Sesko

Yote kwa Yote Cunha ni Mtu, Kapiga on Target nyingi sana, Mbeumo na kilo zake 200 sidhani kama tutafika nalo mbali na tumbo lake kama Mfuko wa Dangote Cement.

Dorgu Ni mtu na Nusu fundi sana kwenye Upande wake,

Bruno Mnamsifia tu ila huyu kenge hajafanya lolote la maana

Yoro nae ni kama Chollo Mpemba tu , Shaw nae astaafu sasa Toka 2017 yupo tu na hakuna la maana analofanya.

Case angalau kapunguza mieleka kama Houjlund na kadi zisizo za Muhimu

Raya Ni Kipa na nusu, Moja ya karata nimeikubali ni Amorim kutomshoboke Grykokoze kwenye usajili kumbe alikua anamjua vizuri ni galasa Halijafanya Maajabu yoyote Aisee nawaza ndo wangemsajili Man U sijui ingekuaje bora hawa kina Cunha wanafika na kutisha golini

Yote kwa yote Game nzuri Timu ime Improve sana bado huyo Baleba tu tuondoke pale kati
 
Mashabiki wa Man U mlianza kunenepa

Sasa mateso yamerudi palepale ni muda wakukata wese mwilini🤣🤣🤣🤣
 
Nyie takataka mnakamia mechi ili mfungwe moja bila mfurahi ?
Arsenal miaka yote akishinda old Trafford anashindaga moja bila kwa hiyo nyinyi bado ni takataka tu msijifariji hapo nilikuwa napiga show za mkwezi
Njooni geto niwapige mridhike
Manjesta ni mwali wa kizaramo ukimpiga kimoja anatangaza mtaa mzima mwanaume hana nguvu za kiume
 
Ukweli mchungu huu.
 
Majirani, hongereni kwa mchezo mzuri wa jana. Ushabiki nikiweka pembeni jana mlikua vizuri kwenye kila eneo, ata goli tulilopata ni lapapatu papatu tu

Timu mnayo, amorim ashindwe yeye tu. Unapokua na watu like cunha, mbeumo, sesko moja kwa moja watu watataka matokeo

Usajiri wenu umeonesha impact for 90%, mazee timu mnayo

Jambo ambalo arsenal ashukuru ni kumalizana na nyumbu OT kabla gari halijawaka vizuri

Cunha sesko mbeumo mkienda vizuri na hii front line bila majerui, itakua hatari sana msimu huu

Ukiona kipa ndio man of the match, ujue hali haikuwa shwari
 
Tupate Darasa kidogo kutoka kwa Geoffrey lea

Kwenye mpira mfumo lazima uwape wachezaji wa kila nafasi faida kulingana na kile wanachoweza kukifanya kwa ubora katika majukumu yao, lakini pia mfumo unatakiwa kuwarahisishia wachezaji wanachofanya uwanjani na sio kufanya kazi yao kuwa ngumu zaidi!!!

Kwa sababu Amorim anaanza mechi na 6 defensive minded players tena bila point of play kwenye attack (jinsi alivyoanza bila mshambuliaji asilia) maana yake timu inawatesa sana wachezaji kama Matheus Cunha na Bruno kwa jinsi ambavyo anaanzia chini sana kama mmoja wa wachezaji wawili wa kiungo

Hizi picha 3 hapo chini zinaonyesha jinsi Cunha alivyolazimika kuanzia safari yake mbali bila Teammate Karibu ambaye wangesaidiana either pasi au kuwaoccupy mabeki na kutengeneza njia nyepesi ya kupita lakini angalia amezungukwa na wapinzani wangapi,

Matokeo yake Cunha na Mbeumo walilazimika kutumia sana uwezo binafsi kushambulia kwa sababu mfumo haujawasaidia,

Katika mfumo kama wa 4-3-3 au 4-2-3-1 mbeumo cunha na Bruno watakuwa wanaanzia karibu na goli na kuspend muda mwingi wa mechi karibu na final third, Changamoto kubwa ya Amorim ni hii hata zile nafasi za kipindi cha kwanza zilikuja kutokana na uwezo binafsi zaidi kuliko mfumo.
Tofautisha na Arsenal ambao walikuwa wakishambulia wana options mbili au tatu kwa jinsi timu ilivyopangwa, System ya Amorim haiwezi kufanya kazi kwenye EPL tena especially dhidi ya Timu ndogo ndogo ambazo zinajua kucheza kwenye low block na kushambulia kwa counter.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…