Hapo kwenye back three ndipo kwenye utamu wenyewe, pia katikati Kuna utamu wake. 3-4-2-1 hivi ndivyo anavyo set mpango wake, kwahiyo Lisandro Martinez na Shaw watakuwa ni watu muhimu sana LCB (wasiwasi wangu ni majeraha, tunaweza kuingia sokoni hapa, utajikuta timu nzima ipo wodini na ndo kutukanana kutaanza hapa). Yoro nae atakuwa ni muhimu kama RCB kama tu akijaribiwa na kucheza na kuhimili EPL, namuona de light akiwa CB kiongozi (huyu anakuzubaa Fulani japo ni beki mzuri pia).
Najua tutalia na hizi winga, maana kwenye kuzuia lazima tusipungue wanne nyuma na tutakuwa watano tunazuia, majanga ni pale uko na ambush tena na timu zinazopenda kukimbia the likes of Madrid, Liverpool haha, halafu winga zako hazirudi zinatembea lazima utamtukana kocha.
Namuona dalot na mazroui au luke shaw wakiwa pembeni, kati najua ugarte anaweza kufit kwenye mfumo Kwa maana mfumo uko na favour kwake, mainoo anaweza akafit vizuri tu.
Watu watatu kule mbele wanamaliza, rasmus anaweza kuwa forward na akafit Kwa mfumo huo, kule CP Kuna yule mswideni amefit vizuri na huyu jamaa, wanafanana Kwa kiasi Fulani. Rashford au garnacho lazima mmoja atacheza na Bruno. Amad anaweza kucheza pia. Nategemea Kuna nyakati nyingi tu Bruno atakuwa deep sana.
Kwa 3-4-2-1 ndiyo mara nyingi huyu amorim hutumia (If akitua, japo chance ni kubwa), hutumia pia 3-4-3 na 3-5-2.
Binafsi nategemea watu watakimbia sana Kwa hii mifumo ya jamaa na nature ya ligi ya uingereza ilivyo. Uzuri ni kwamba Kuna msingi Fulani upo UTD unafanana na amorim. Sidhani kama wachezaji wavivu au wasiotekeleza majukumu Yao vizuri wataweza maana Kwa hizo back three kutobolewa magoli ni kunusa chap, ndio maana Kuna timu zilitaka kumchukua amorim Kwa sharti tu la kutokuanza na back three lakini alikataa na wakaachana nae. Lazima tuwe na watu wanaoeleweka la sivyo unatoboka mechi kibao Imagine goli walizotufunga spurs, liverpool na kama mnakatika Kwa mifumo ya back three unakula chuma zaidi ya zile.