Habari zenu wana Jf, naomba msaada wenu kunijulisha ni mambo gani ya msingi ya kisheria kuyafanya unapotaka kununua gari kwa mtu binafsi yaani gari lake analolitumia au unapoenda showroom hasa jinsi ya kulipana pesa, mashahidi wa kuwatumia, uthibitisho kama gari si ya wizi (hasa unaponunua kwa mtu binafsi), jinsi ya kumbana kama gari litakusumbua baada ya siku chache, jinsi ya kubadirisha jina la umiliki, kujua blue kadi feki au original na mengineyo ambayo mnaona yatanisaidai maana ni mgeni ktk ulingo huu wa kumiliki hivi vitu nisije nikaingia kichwakichwa
Kazi njema
Kazi njema