Una uhakika gani kama Zakia sio muadilifu, kuna ushahidi wo wote? Usilete ya Kagoda maana she was not involved.
Sasa Makamba is gone does that mean kwamba Tambwe Hizza ndiyo mwisho wake pia au inakuwaje ?
alifanya madudu pale wizara ya afya alipoondoka walifurahi waulizeni watu wa wizarani ikabidi aletwe mama Nyoni kuweka mambo sawa hadi sasa mama Nyoni anahangaika na madudu yake ,Je CCM ataiweza ? pia ni mshikaji sana wa JK kama kawaida yake ushikaji mbele
Huyu pinda aliokotwa wapi na ni zao la nani? kapewa rungu la kuulia kabla ya kuua analia kwanza asaidiwe kuua anajiliza kinafki.. pia mie simuamini tena kwani ni Muongo anadanganya hadi Bunge..nakubaliana kiasi flani na ndugu fairplayer. Lowasa pamoja na ujambazi, unyang'au ni mtu anaediriki.ana uthubutu wa kimaamuzi,kama alikosea ktk mambo kadhaa ni ubinadamu tu. hakuna mtu aliekamili. jamaa mwizi lkn mtu wa kazi sana na anawezesha vtu kwenda. watumishi wengi tu wa serikali walikuwa wanamwogopa enzi zake sio leo wakati wa pinda ambae akikuta uozo anaanza kulia badala ya kuchukua hatua firm. to me lowasa hata akiwa presidaaa 2015 sawa tu!!
Hapo bado sura ni zile zile tu, nyoka hajalivua gamba bali amelipaka majivu tu ili lionekane kubadilika mwonekano wake.halafu mbona naona gamba la nyoka halijavuliwa ..........au wadau mnasemaje
- Mukama a great man and good leader, one of CCM's long time behind the scene propangandists, loongtime Chuo cha Kivukoni, my very close loongtime friend, and with Kinana it means only one thing, the end of Mafisadi.
- Alikuwa ni Mukama, aliyegundua ubadhirifu wa ajabu sana uliofanywa Jiji na kumuarifu Rais no wonder aliyetoka huko mlo ukaisha! This is great change for CCM, isipokuwa ni mapema sana kutabiri what it means to Taifa, lakini with Kinana ninaamini this to be the end of Mafisadi.
FMeS!
CCM imepata a political technocrat.Kama haya ni ya kweli, basi CCM haina shukrani. Makamba kawapigania siku zote! Alikubali kupakwa matope ya chama akabaki nayo ili chama kinusurike! Eti kaondoka kirahisi hivyo? Makamba usijali Mungu atakulipia!
niliwahi pata nyepesi kwamba wakati huyu bwana mukubwa akiwa katibu mkuu afya, aliwahi kwaruzana na 'nguli' moja pale wizarani ambaye aliaminika kuwa mtu wa system... Kilichotokea ni kwamba mmoja alimwaga mboga na mwingine akamwaga ugali, wote wakang'oka; mukama akapelekwa jiji mwingine sikumbuki alitupwa wapi...
Huyu jamaa alikuwa na Keenja Jiji la DSM,baada ya hapo nkumbuka kama alikuwa katibu mkuu wizara moja wapo ya awamu ya nne.
Viongozi wasio kwenye makundi yeyote, wachapa kazi na wenye uchungu wa nchi ndio wanaweza kutufaa mwaka 2015 kutuongoza.
Kiongozi kama Lazaro Nyalandu- naibu waziri wa viwanda na biashara anasifa na anafaa kuongoza nchi akigombea kwa chama chochote atapeta na hana mpizani...!
Wilson Mkama kaukwaa ukatibu mkuu wa CCM, Makamba nje!
Ni kama ilivyotabiriwa na mwana JF mmoja January 12, 2011 hapa ~ https://www.jamiiforums.com/jukwaa-...lson-mukama-anaandaliwa-kumpokea-makamba.html
CCM imepata a political technocrat.
Mtu anayeweza kuendesha chama kwa misingi ya kiitikadi na kukubalika kwa wananchi.Kwa kumteua Mukama CCM haijakosea, huyu ni mtu ambaye aana uzoefu wa kucheza chess ya kisiasa.
Niliwahi kusema huko nyuma kuwa masikini Makamba, he is neither a political analyst. nor a thinker or a strategist!!!
Na aliteua watu uozo kama Tambwe Hizza-Hadija Kopa wa kisiasa-watu wa mipasho badala kupata ya watu wenye uwezo wa kufikiri na kupanga.
Ukimlinganisha na aliyemuachia ofisi , Philip Mangula, ni wazi kuwa alikuwa akipwaya katika idara zote, funga kazi ni madudu ya uchaguzi wa 2010.
JK hajafanya kosa kumwomba Makamba akae pembeni kwani hata yeye(JK) nafasi yake ilianza kupwaya vibaya kutokana na madudu ya chama-yeye akiwa mweyekiti.
Wana CCM-maslahi wamemtumia vilivyo Mzee Makamba, hili liko wazi.
Kiitikadi kuondoka kwa Makamba ni upepo na harufu nzuri kwa uhai wa Chama.
Si wengi watakao mlilia Makamba. ila wale waliofaidika kimaslahi kwa yeye kuwepo pale kama katibu mkuu.