Mambo matano ya awali niliyoyaona kwa Rais Samia

Mambo matano ya awali niliyoyaona kwa Rais Samia

Taarifa zinavuja endapo wanaotakiwa kuzitunza mioyo yao inavuja damu na macho kutoa machozi
Hapo watavujisha wakihisi ahueni itapatikana
Watu hawalijui hilo. Ni kwamba mkiwa mmepewa mikate miwili na nyie mpo watano halafu mmeambiwa mgawane vipande sawa kwa haki halafu watatu kati yenu wakala vipande vingi kukuzidi nyie wawili..

Mnaweza kuvumilia ila ikiletwa mikate mingine hali ikaendelea kuwa vilevile basi tambua kwamba mtaanza kugeukana ninyi kwa ninyi na mambo yenu ya ndani yataanza kuvuja tu
 
Na Thadei Ole Mushi.

1. Mpaka saa Hakuna Mvujo wa Taarifa za Serikali. Hakuna anayeweza kunusa kabisa nini kinaweza kutokea. Zimebaki kuwa confidential kwa asilimia 💯.

2. Viongozi waliopo kwenye Utumishi wa Umma wawe makini Sana. Kwa muda mfupi niliomsoma Mama anataka viongozi wenye Discipline ya kutosha. Kwa kumuangalia Usoni haogopeshi Ila maamuzi yake yanaogopesha Sana.

3. Kuondolewa kwa Gelasius Gasper Byakanwa Mkuu wa Mkoa wa Mtwara ni muendelezo wa kuelekea kwenye Political reconciliation. Huyu mkuu wa Mkoa ni yule aliyevunja Green House ya Mbowe kule Hai na kupewa promotion toka kuwa mkuu wa Wilaya hadi Mkuu wa Mkoa. Kuna kitu watu hawajakielewa, Mama anataka kuyaleta makundi yote Pamoja. Kuna watu bado wapo kwenye Enzi za matumizi ya Nguvu badala ya akili. Kwa walioteuliwa Mpaka sasa kumbukeni Hili zama zimebadilika.

4. Jambo Lingine naloliona kwa sasa Mama anasikiliza Sana anaowaongoza. Hapo nyuma Kidogo watu wangeweza kupiga kelele kuhusu uadilifu wa Mtu flan lakini mamlaka ikamuacha tu as long as wanaolalamika ni wapinzani. Kwa sasa viongozi wanaoteuliwa pona yao ipo kwa wananchi... Yaani wananchi wakikuchukia utatolewa. Niwahusie wote walioteuliwa Mpaka sasa kuwa mtaji wao upo kwa wananchi. Kiwango Cha kukubalika na wananchi kitaamua umri wako kwenye nafasi uliyopewa.

5. Vipengele Muhimu katika uongozi vimeshaonekana (Power & Authority). Power uwezo wa Ku influence wengine kufanya au kutokufanya jambo flani. Cha pili ni Authority, huu ni uwezo wa kumshurutisha mtu kuacha au kufanya jambo flan "Mamlaka" ambayo kutokana na kazi yako na nafasi yako kazini unakuwa na mamlaka ya kumwamrisha wa chini yako au unaowaongoza.

Kauli Moja tu ya "Kudemka" ilitosha kunyamazisha wabunge na mijadala yao ya kumfananisha na Hayati Dkt. John Magufuli.

Ole Mushi
0712702602

View attachment 1786654
People will always want to test new things to see if they have what it takes own such qualities, As bonus character, a good leader must be unpredictable, and SHE IS.
 
Ugomvi mkubwa sana wa Kigogo ulikuwa ni kati yake na jiwe.
Siku hizi kigogo ni kama sisi
Taarifa za kesho zimeminywa
Huyu mama nahisi majina anatembea nayo kwenye mkoba wake.
 
Na Thadei Ole Mushi.

1. Mpaka saa Hakuna Mvujo wa Taarifa za Serikali. Hakuna anayeweza kunusa kabisa nini kinaweza kutokea. Zimebaki kuwa confidential kwa asilimia 💯.

2. Viongozi waliopo kwenye Utumishi wa Umma wawe makini Sana. Kwa muda mfupi niliomsoma Mama anataka viongozi wenye Discipline ya kutosha. Kwa kumuangalia Usoni haogopeshi Ila maamuzi yake yanaogopesha Sana.

3. Kuondolewa kwa Gelasius Gasper Byakanwa Mkuu wa Mkoa wa Mtwara ni muendelezo wa kuelekea kwenye Political reconciliation. Huyu mkuu wa Mkoa ni yule aliyevunja Green House ya Mbowe kule Hai na kupewa promotion toka kuwa mkuu wa Wilaya hadi Mkuu wa Mkoa. Kuna kitu watu hawajakielewa, Mama anataka kuyaleta makundi yote Pamoja. Kuna watu bado wapo kwenye Enzi za matumizi ya Nguvu badala ya akili. Kwa walioteuliwa Mpaka sasa kumbukeni Hili zama zimebadilika.

4. Jambo Lingine naloliona kwa sasa Mama anasikiliza Sana anaowaongoza. Hapo nyuma Kidogo watu wangeweza kupiga kelele kuhusu uadilifu wa Mtu flan lakini mamlaka ikamuacha tu as long as wanaolalamika ni wapinzani. Kwa sasa viongozi wanaoteuliwa pona yao ipo kwa wananchi... Yaani wananchi wakikuchukia utatolewa. Niwahusie wote walioteuliwa Mpaka sasa kuwa mtaji wao upo kwa wananchi. Kiwango Cha kukubalika na wananchi kitaamua umri wako kwenye nafasi uliyopewa.

5. Vipengele Muhimu katika uongozi vimeshaonekana (Power & Authority). Power uwezo wa Ku influence wengine kufanya au kutokufanya jambo flani. Cha pili ni Authority, huu ni uwezo wa kumshurutisha mtu kuacha au kufanya jambo flan "Mamlaka" ambayo kutokana na kazi yako na nafasi yako kazini unakuwa na mamlaka ya kumwamrisha wa chini yako au unaowaongoza.

Kauli Moja tu ya "Kudemka" ilitosha kunyamazisha wabunge na mijadala yao ya kumfananisha na Hayati Dkt. John Magufuli.

Ole Mushi
0712702602

View attachment 1786654
Punguza mahaba mkuu.... Hakuna jipya..
 
Matumizi ya mabavu ,kujipendekeza hofu na kutumia media kusifia MTU vimepotea.Asante Mungu Baba kwa zawadi ya Mama.
 
Siku hizi kigogo ni kama sisi
Taarifa za kesho zimeminywa
Huyu mama nahisi majina anatembea nayo kwenye mkoba wake.
Shujaa taarifa zilivuja kwa kuwa watu wa karibu yake hawakumpenda pia, walikuwa wanafanya HUJUMA kuonyesha madhaifu ya mfumo. Mama kaanza vizuri, akiboronga utaona yale yale ya taarifa kuanza kuvuja....
 
Uhuru wa vyombo vya habari pia umechangia kutovuja siri za serikali. All in all wanawake kwa kutunza siri ndo mahari pao.
 
Ikulu kwa sasa imemilikishwa kwa wa Znz, hawa jamaa wana siri hatare sana

Nakumbuka 2003 kwny uchaguzi wa marudio wa Majimbo 16 kule Znz…Jamaa kisiwa kizima kumbe waliambiana wakapige kura za Maruhani huwezi amini na uwepo wetu kule hawakuwahi kumwambia Mbara yeyote kuwa kesho tunaenda kupiga kura ya Maruhan, hadi watoto wa Madrasa walikuwa na siri hiyo kisiwa kizima lakin sie 'Machogo' hatukujulishwa hadi tunastukia aibu kwmy Masanduku ya kura

Sasa hivi Kigogo amekuwa mchambuzi wa Siasa sio tena mtu wa Breaking newz


Ila pia nmejifunza Wasukuma 'hawana vifua', wakati wao Ikulu kila kitu kipo open

Kuhusu taarifa na usiri wake naunga mkono.

Serikali ilitumia nguvu Sana kupambana na kigogo badala ya kudhibiti utokaji wa taarifa hovyo..
 
Mahawara wa kike wenye 'mikia' na rangi ya 'mtume' ndio lilikuwa 'tobo'

Ukishikwa shikwa kifua unaeleza hata usiyopaswa kueleza

Mbinu hii imetumika sana kwny vilabu vyetu vya Simba na Yanga kwa kina Morrison na Okwi na wachezaji wengine kadhaa

Wahuni wa Jiji japo wamestaafu lakin akili hazijastaafu
Nasikia walibadilishwa sana still hakufanikiwa kuziba leakages, labda kuna kitu walimuwekea bila yeye kujua kikawa kinaiba taarifa
 
Ikulu kwa sasa imemilikishwa kwa wa Znz, hawa jamaa wana siri hatare sana

Nakumbuka 2003 kwny uchaguzi wa marudio wa Majimbo 16 kule Znz…Jamaa kisiwa kizima kumbe waliambiana wakapige kura za Maruhani huwezi amini na uwepo wetu kule hawakuwahi kumwambia Mbara yeyote kuwa kesho tunaenda kupiga kura ya Maruhan, hadi watoto wa Madrasa walikuwa na siri hiyo kisiwa kizima lakin sie 'Machogo' hatukujulishwa hadi tunastukia aibu kwmy Masanduku ya kura

Sasa hivi Kigogo amekuwa mchambuzi wa Siasa sio tena mtu wa Breaking newz


Ila pia nmejifunza Wasukuma 'hawana vifua', wakati wao Ikulu kila kitu kipo open
Kura za maruhan ndio kura gani Mkuu?
 
baada ya wajinga fulani kumtaka amtoe happi na chalamila,mama akawashtukia.

kifupi mama anataka kuonyesha watu,kwamba hapendo shobo na kukadiriwa kadiriwa.
 
Taarifa zinavuja endapo wanaotakiwa kuzitunza mioyo yao inavuja damu na macho kutoa machozi
Hapo watavujisha wakihisi ahueni itapatikana
hakuna sababu ya msingi ya taarifa kutokuvuja mpaka sasa,zaidi ya usaliti kwa mwendazake.

mama anajua kabisa kwamba adui wa mtu mwingine sio wa kumwamini atakubadirikia na wewe muda wowote usipomnufaisha tu,hao ni wanafiki tu.
kwa misingi hiyo anaandika majina kwenye kioo asubuhi akiwa anapiga mswaki.
 
Back
Top Bottom