Habari za humu wa JF,
Mimi ni kijana umri 24 naishi Dar es salaam. Nilikua na baba ambaye alikua yupo katika mahusiano na mama mwingine (wakambo), kwa muda alianza sumbuliwa na cancer mpaka badae ini likawa infected na mwaka jana kwa bahati mbaya baba akanitoka nikiwa bado nasoma chuo, nakumbuka nilipigiwa simu nakupewa taarifa yakua kanitoka.
Nilipigwa na buutwa nakuchukua masalia yangu ya pesa nakukata ticket ili niwahi kumuona baba hata kwa mara ya mwisho. Nilifanikiwa kufika salama na mambo yote yakaenda salama japo moyoni nikiwaza baba kaniacha nani atakua msaada na chuo sijamaliza nikiangalia kodi pia nadaiwa mawazo mengi sana kichwani!!!
Familia yangu ilikua tofauti na za ndugu zangu kidogo kwakua Late baba aliwekeza sana katika elimu na ukiangalia ba mdogo na ndugu wakaribu walikua hawana support yoyote ile.
Baada ya mambo yote kuisha kuna baadhi ya mali ziliingia katika mkono wa mama wa kambo na alivokutana namimi akaona kama nafatilia akawa mkali na kuacha kabisa kunisaidia hata pesa za matumizi ambayo alikua awali ananisaidia, nimerudi nikitegemea ataweza nisaidia au ndugu jamaa na marafiki ila mambo yamegeuka na amesema hawezi japo uwezo anao wakufanya ivo.
Nipo katika kipindi ambacho sijui nini lakufanya vyuo vimefunguliwa ada sina pakukaa sina kodi iliisha yaani naona mambo yameniharibikia kabisa na ndugu ndio walishanitenga sijui nifanye nini kwakweli nilichokua naweza nikua smart katika masomo yangu nanilipanga mambo mengi sana.
Naandika haya sipo sawa nimekaa namachozi yananilenga mtoto wa kiume sijui nifanye nini naona hakuna msaada I wish ningepata mtu wa karibu ambaye ange act kama baba, ndugu zangu hii hali inaumiza sana i wish ningepata msaada wowote.