Mkuu
Path Creator hutakiwi kurudia kila comment yako habari ya mama wa kambo,mwandiko wako unanionyesha kuwa unajificha kwenye mwavuli wa mama wa kambo sana.
1.mam yako wa kambo aliwezaje kujimilikisha mali bila kikao cha familia au hata wazee wa ukoo
2. Unasema baba yako aliwekeza kwenye elimu sana,sio,ni elimu ipi aliyoiwekeza
3. Wewe ni mtoto halali wa marehemu huyo baba
4. Unasema kuwa mama yako alianza kukubadilikia baada ya kuanza kuhangaikia mirathi sio!uliangaikia kwa namna ipi
5.kuna mkuu fulani hapo juu amejaribu kukuvuta akusaidie lakini kulingana na unavyocomment

huonyeshi ushirikiano ipasavyo kwanini
6. Mpka umefikia hatua ya kwenda chuo maana umeshavuka umri wa kuwa mtoto,kwanini baba yako hakukupatia japo urithi ikiwa wewe ni mwanae?
7. Kama baba aliwekeza kwenye elimu,kwenye Bank ac kuna shilingi ngapi ya kuweza kukuendeleza kielimu
8. Ina maana kwenye ukoo wenu marehemu alikuwa hapatani na ukoo mzima kisa kupenda kwake elimu
9.kwahiyo nyie mlikuwa hamna japo ndugu mmoja ambae alikuwa anawatembelea na nyie mnamtembelea
Natamani kutichape bakora kidogo kustua akili yako itoke huko ilipo


maana unatoa majibu mepesi kwenye maswali magumu.
JF ni kubwa hii na inawatu wakubwa wengi ila huwezi kuwajua wengine kwa ajili ya fake idz.ondoa ukakasi katika mwandiko wako upate msaada kijana.sentensi zako zinapwaya sana.
Pole kama mwandiko wangu hauonyeshi yale uyategemeayo.jibu maswali niliyokuuliza tafadhali.
Poleni kwa gazeti na kutokupangilia vizuri maswali