Watu kulala hovyo kwenye madaldala ni dalili ya njaa kali!

WhoWeBe

JF-Expert Member
Dec 18, 2022
2,301
4,243
Watu wanasinzia tu sasa hovyohovyo kwenye daladala; ile mtu amekalia tu siti na gari kujitikisa kidogo tayari usingizi na mara kadhaa udenda pia.

Panda daladala za routes zote sasa hapa Dar hali ni hiyo. Mtu anapanda buguruni sheli anashuka sokota lakini hafiki bila kusinzia. Nenda nje ya Dar, Pwani, Dodoma, Lindi, Mtwara hali ni hiyohiyo. Kesi za watu kupitishwa, sorry, kujipitisha vituo zimekuwa nyingi sasa. Mtu anazinduka usingizini tayari kapita kituo.

Haya ni matokeo ya uchunguzi wangu wa miezi mitano sasa katika maeneo niliyoyataja kwani nipo humo karibu kila siku. Dar ndipo uchunguzi wangu kwa kiasi kikubwa umefanyika (nimeichunguza dar kuhusu hili kwa 98%). Siku za nyuma hali haikuwa hivi kabisa.....

Rais Samia, hali hii imenipatia majibu kuwa ni kutokana na ugumu wa maisha mama; hali ngumu mtaani si mchezo. Vyakula haviliki, kwani wengi hawana uwezo wa kununua mchele kilo tshs. 4,000/= wala kununua maharage 3000/=.

Ada hakuna lakini mfumuko wa hivyo vifaa vya shule si mchezo, wazazi hoooi.

Hali imekuwa tafrani kiasi watu wanaumwa lakini hata hawajui kama wanaumwa, wanatembea tu na kuhangaika.

Si mkulima, si asiye mkulima; wote hoooi.

Mama mswalie mtume, fikiria namna ya kutukwamua......kama vipi mazao yazuiwe tu kutoka nje kama zamani kwani kwa sasa hata wakulima wenyewe (nazungumzia hawa wadogo wadogo ambao ndo 99%) hawana hela wala chakula; kumbe wanaofaidika na ruhusa hii ni wafanyabiashara wa mazao ya chakula na wakulima wakubwa (ambao ni 1% tu).

Nawasilisha.
 
Hiyo hali ni uchovu, unaosababisha hali ya hewa, joto, kipindi hiki ni kali sana, hivyo watu wengi hulala wakipepewa na feni, ambalo husababisha mtu kuchoka.

Hivyo ukitulia tu kidogo usingizi unakuja tu, hakuna zaidi hilo.
 
Nyie subirini tu mkue, mtaelewa.
Labda nife, niko mwishoni mwa wastani miaka ya kuishi mtanzania, miaka 54, nikue niende wapi.

Unakumbuka methari za wahenga, Shibe mwana malevya, na njaa mwana malegeza, unadhani walimaanisha nini.

Alafu jiulize kwanini, madereva wengi hukwepa kula sana, wakati wa mchana.
 
Wewe ukiwa na njaa ndo unalala hovyo au ukishiba ndio unalala hovyo?
 
Mkuu umeweka percent tena 98% ambapo huo ni utafiti wako, mbona kama umefanya observation tu? Kwenye utafiti observation pekee hautoshi kukupa conclusion ya utafiti, labda ungeuliza watu kwanini wanalala?
 
Wakati mwingine mtuwekee basi na picha ili tuwaone hao wasinziaji. Maana sisi wengine tuko vijijini huku, ambako hizo daladala hakuna.
 
Kuna mmoja jana alitakiwa kushuka itv ,kutokana na kusinzia akashtuka gari likiwa mataa yakuingiaa makumbusho stend aisee alimtukana kondaa utafikirii konda ndio alimwambia alale
 
Dogo nakukumbusha tu kua mvua sasa zinanyesha uende ukalime na wewe sio kulia lia hapa eti mama afunge mipaka ili mchele na maharage vishuke bei

Kama mji umekushinda rudi bush kalime uje uuze hizo bei unazotaka wewe.
 
Aisee!Nilikua sijui kuwa kulala kwenye daladala ni ishara ya njaa.
Kulala au kupata usingizi ni majaliwa ya ulevi wa SHIBE.
Kuwa na njaa uone kama utasinzia.
N. B, Mama lishe na wapishi mbalimbali acheni kuweka hamira kwenye ubwabwa mnasababisha haya.
 
Back
Top Bottom