Mama ni mgonjwa

Mama ni mgonjwa

Mungu mkubwa kuwa naimani mama atapona kumbuka kwakugusa vazi tu mtu alipona nawe kwaimani tu mama yumzima pole best
 
Pole miss Strong, just be strong kama avatar yako na kama alivyoshauri mmoja wetu hapa mpeleke akapime blood sugar! Kipimo hicho si lazima kwenda mbali hata massana anaweza kupimwa, ila akibainika kuwa na diabetic (yaani ana kisukari) ndo umpeleke sasa kwa wataalam wa magonjwa hayo kama huyo Abassy, n.k.
 
Last edited by a moderator:
Pole sana mamy.
Mama mkwe wangu naye ilianza kama hivyo wakagundua ni sukari ila alikuja kukatwa mguu.
Mjaribu kupima sukari kama hajafanya hivyo.
Pole.
 
Kwa jina la Yesu apokee uponyaji
Samwel alisema Eben-ezer.......
 
Habar wa MMU.......aiseee nahitaji mnikumbuke katika maombi,mama yangu ni mgonjwa na hatujui tufanye nini maana hospital ugonjwa hauonekani.

Alichomwa na kitu mguuni wiki 5 zilizopita ikaota kama kipele then lengelenge na baadae mguu wote ukawa umepata vidonda.

Kapimwa magonjwa mengi lakini hamna kitu......leo roho imeniuma sababu mguu umeanza kutoa harufu na tena ukijan umeanza.

Naumia sana....nahitaji maombi yenu anaitwa Vicky

Kuna baadhi ya miti mingine ina sumu kali alichotakiwa siku ya kwanza ange safishwa kidonda na kupatiwa ant biotic mf cloxiacillin kuzuia bakteria wasizaliane na kama kidonda kimeingia ndani ni raisi kupata bakteria wanaosababisha tetenus kutokana na bakteria hao kupenda kuzaliana sehemu yenye joto na sindano ya kinga tetenus ni muhimu sana pole sana ndugu mungu atawatangulia atapona
 
Thanks nimecheck vyeti alivyotoka navyo kwa dada yake na hv vya lugalo.....amepimwa sukari hana.Labda mniambie ni hospital gani nzur zaid kwa ajil ya kupima sukari
 
Pole sana tuko pamoja nawe katika wakati huu mgumu
 
Muwe na amani na vunjeni laana zote ambazo zinawanyelea ktk maombezi Damu Takatifu ya Yesu ifunike kidonda chake kipone haraka. Jina la Bwana lihimidiwe milele na milele Amina.
 
pole saana Madam, Mungu yu pamoja nawe na yeye ndo kimbilio letu sote!

Naamini kwa Neema za mwenyezi Mungu atapona soon tena ndani ya wiki hii!

In name of JESUS !!

trust Me!!
 
endeleeni na juhudi za hospital ila pia kwa imani mliyonayo apatiwe maombi.
 
Huu ugonjwa uliwahi kumpata ndugu yangu mmoja, yeye nae kalikuwa ni kaupele mguuni, akakakuna kilichotokea baada ya kukakuna ni kama unavyosema mguu wa mama yako jinsi ulivyo, walimuwahisha hospital bahati mbaya sana nimesahau jina la huo ugonjwa, ila alifanyiwa oparation tatu, na madaktari walisema ni kwa sababu ugonjwa haujafika kwenye mfupa, ungefika kwenye mfupa kungekuwa hakuna jinsi zaidi ya kuukata mguu hadi kwenye goti, ila coz waliwahi walikwangua tu zile nyama na ata the end walikata nyama kwenye paja na kurudishia pale walipokwangua. Kiukweli hali ilikuwa mbaya hata sisi tulidhani ni kisukari but haikuwa kisukari, now anaendelea vizuri sana tu. so Mpelekeni hospital pengine ana huo ugonjwa, kama uko mwanza huyo ndg yangu alitibiwa hapo hospital ya CF, NSSF ya zamani
 
Pole miss strong and be strong. I can imagine how u feel right now ila jitahidi kuwa jasiri mbele ya mama na fata ushauri wa wana Jf wa hosptal na maombi na mama atapona Inshallah
 
Last edited by a moderator:
Pima sukari lakini cha muhimu kama umesema wali mchoma power cef inj na hajapona mnaweza mpatia gentamycin inj ila achanganye na metronidazole tabs kwa vile bakteria wa namna hyo flagly ndio nzuri kuwatibu pamoja na ant biotic strong na pia anaweza changanya na fluconazole kwa kuwa sehemu kama hizo fangus huwa wanapenda kunyemelea na aendelee na dressing ujitahidi kufanya culture ya hicho kidonda itajulikana ni bacteria wa aina gani waliopo na kingine mgonjwa anapokuwa na kidonda kikubwa cha muda anaweza akapata sukari kutokana na lile jeraha alilokuwa nalo kidonda kikipona sukari inakuwa normal kabisa usife moyo atapona.
 
Miss Strong,

Poleni kwa kuuguza. May the Almighty guide you to the right medication and grant her the healing, so we pray!

PP
 
Pole sana miss strong Mungu awaangazie madaktari wajua hasa kinachomsumbua
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom