KERO Malipo ya Likizo ya Watumishi wa Umma Liwale - Lindi, Idara ya Elimu hayatoki kwa wakati, kuna muda yanachukua hadi miaka miwili

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua
A

Anonymous

Guest
Watumishi wa Umma, Idara ya Elimu hasa Sekondari Wilaya ya Liwale Mkoani Lindi hawalipwi fedha zao za likizo kwa wakati, wakati mwingine inaweza kuchukua hata miaka miwili ndio wanakuja kupata malipo.

Hata wakiomba kiwango fulani cha nauli, wahusika wanaolipa na malipo wanachofanya ni kukadiria tu na sio uhalisia wa ulichoomba, mbaya zaidi na kinachotia mashaka ni kiwango kinachoombwa kwenye mfumo wao (ESS, Elimu Sekondari), wanalazimisha waombe kwa kuandika kwa mkono wakati kila kitu siku hizi kinafanyika kidigitali.

Mwaka 2025 mwezi December walimu waliomba likizo zao za malipo kwenye mfumo wa ESS lakini zilipofika idarani zilikuwa "rolled back" (walirejesha nyuma) na wakasema ni sababu za kimtandao, hivyo walimu waombe likizo zao kwa kuandika kwa mkono.

Hili linatia mashaka na kuleta usumbufu pia na linashusha morali kwa walimu.
 
Pole mwalimu mwenzangu,Mimi Niko mpigamiti SM,wewe uko wapi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…