Mgeni wa Jiji
JF-Expert Member
- Jul 27, 2017
- 8,120
- 13,956
Mkuu bado hujazeeka alafu mwanao yule jembe kabisa akakataa chochote kutoka kwako. Utafadhaika sana Mkuu. Sahivi unaweza ukachukulia poa ila sio poa kabisa.Duuh Kweli tunatofautiana, mimi binafsi mali ya urithi nilishaiondoa kwenye akili zangu, Baba yangu wa kambo aliniweka kwenye urithi wa moja kati ya mali zake lakini nilikataa, sio kwamba tuna migogoro ya kifamilia au matatizo yoyote ila nilikataa tu, kwa sababu huwa naamini urithi pekee nilio nao ni akili yangu tu, na inanitosha kupata nachohitaji maishani.
Unajua kwenye urithi wa mali huwa kuna dhamira inafatana na hiyo mali. Unaweza rithi mali ila ikawa n mfano tu wa baraka ulizorithishwa na huyo marehemu. Kwa hiyo tambua urithi wa mali unakuja na baraka/heri kutoka kwa mgawa urithi
Kukataa urithi ni sawa na kukataa baraka na heri utakiwazo na marehemu. Ikiwa wewe unambariki mwanao alafu mwanao anakuamba sitaki hizo baraka na heri zako aise, usipomlaani basi utakufa na kinyongo kibaya.
Watu wengi wanafikiri ukirithi mali basi umerithi hiyo mali tu, jibu ni hapana ukirithi mali unarithi na baraka, heri na hata laana zake pia kama zipo.
Kuna mdau leoleo-tu amesema urithi unaaeza ukawa mzigo ni kweli na hiyo inatokana na mambo mengi sana