Malengo hasa ya kuzaa watoto wengi ni nini?

Jogoo mbegu

JF-Expert Member
Jun 28, 2023
824
3,406
Kwa maisha ya sasa sioni kama kuna tija ya kuzaa watoto wengi ni bora watoto wachache ambao utaweza kuwapatia mahitaji yao ya msingi, chakula, malazi, mavazi, furaha na elimu bora.

Mbaya zaidi unakuta mtu ana watoto wengi ambapo yeye anateseka na watoto pia wanateseka kwa kukosa mahitaji yao msingi.

Unakuta mstaafu ana watoto watu wazima na familia zao ila bado yeye anaendelea kuzaa tu.

Ushauri zaa kiasi upate muda na fedha za wewe kujinafasi na mkeo.
 
Dini Dini Dini....

'mtoto ni baraka' 'kila mtoto anakuja na sahani yake' 'zaeni mkaijaze dunia' ni sawa tu, ila watu hawazingatii uchumi kama unatosheleza

angalia nchi zilizoendelea ambazo hazina sana dini, watu wanazaa kwa mpangilio, tena kuna wengine wako serious kabisa kuliko wazae wanaamua kufuga kambwa kamoja
 
Kwa maisha ya sasa sioni kama kuna tija ya kuzaa watoto wengi ni bora watoto wachache ambao utaweza kuwapatia mahitaji yao ya msingi, chakula, malazi, mavazi, furaha na elimu bora.

Mbaya zaidi unakuta mtu ana watoto wengi ambapo yeye anateseka na watoto pia wanateseka kwa kukosa mahitaji yao msingi.

Unakuta mstaafu ana watoto watu wazima na familia zao ila bado yeye anaendelea kuzaa tu.

Ushauri zaa kiasi upate muda na fedha za wewe kujinafasi na mkeo.
Huku Afrika wanasema watoto waje kuwalea wakizeeka
 
Zaa kadili ya uwezo wako nikimaanisha kama unauwezo wa kuwatunza watoto 20(kuwapa mahitaji yao ipasavyo) zaa tu hamna namna..

Kwa sasa mwenye karata nyingi ndiye mwenye nafasi ya kushinda

Ukiwa na watoto wengi hutokosa wa kukustill kwa namna yoyote ile.
Na piga uwa garagaza wa kutoboa wapo..
 
Dini Dini Dini....

'mtoto ni baraka' 'kila mtoto anakuja na sahani yake' 'zaeni mkaijaze dunia' ni sawa tu, ila watu hawazingatii uchumi kama unatosheleza

angalia nchi zilizoendelea ambazo hazina sana dini, watu wanazaa kwa mpangilio, tena kuna wengine wako serious kabisa kuliko wazae wanaamua kufuga kambwa kamoja
Matajiri pesa zisizohesabika ila unakuta ana mtoto mmoja au wawili tu
 
Ndugu elewa kwamba jamii zetu nyingi zimetokea Mashambani kwa wakulima na wafungaji hivyo ili uwe na mali hauna budi ujikite kwenye kilimo sana na ufungaji kipindi msimu wa kilimo ukifika hivyo unaitaji nguvu kazi ya kulima na kuchunga mifugo

Hapo ndio dhana ya kuzaa watoto wengi ilikuja ili wazazi wapate vijana wa kuchunga ng'ombe na kufanya kazi za mashambani kwa gharama ndogo sana

Tujiulize wewe upo mjini unazaa watoto wengi wanakupa faida ipi mjini hakuna mashamba hakuna mapori yakuchungia

Kijijini mtoto wa miaka kumi na mbili ana tija kwenye familia ila mjini ni mzigo kwenye familia maana atachunga mifugo, au kufanya kazi za mashambani kama parizi nk
 
Mimi nataka nifikishe watoto kumi kila mtu namamaake ndo nioe na hasaivi nipo kwenye wa tano sema kuna uyu mwanamke alienizalia mapacha keshatibua kaongeza idadi kwaspidi mno na watoto wote wawe mikoa tofauti na hawa nilozaa nao maskini ana grocery staki habari zakupelekana ustawi wa jamii
 
Back
Top Bottom