Yericko Nyerere
JF-Expert Member
- Dec 22, 2010
- 16,987
- 20,271
MAKOSA MAKUBWA YA MSWADA WA TISS
Sehemu ya 1.
Moja ya makosa ya mswada wa sheria ya Usalama wa Taifa, kipengele cha 5 cha mswada huo kinampa mamlaka Afisa usalama kukamata na kupekua viongozi, hapa Kifungu hicho kina kinakinzana na Katiba ya Jamhuri ya Muungano inayosema kila mtu sawa mbele ya sheria, Kifungu kinaweka tabaka kwamba viongozi wa kitaifa hawatawajibika mbele ya sheria ya makosa ya jinai inayosimamiwa na jeshi la polisi, Viongozi wote watakuwa na sheria yao na chombo chao cha kuwakamata, kuwapekua na pengine wanaweza kuwa na mahakama zao.
Duniani kote Afisa usalama hafanyi kazi ambazo ni za wazi. Ukishamruhusu akamate na kupekuwa ni automatically umeamrisha afisa usalama huyo afike mbele ya mahakama kutoa ushahidi wa mtuhumiwa kama mkamataji na mpekuzi. Kazi hii iliwekwa kwa Idara ya upelelezi pekee na sio TISS.
Ajabu katika mswada huohuo, unajipinga katika kifungu cha 16 ambapo umeweka katazo la Afisa usalama kutotajwa wala kutojulikana popote yeye binafsi na kazi zake. Unajiuliza hivi hawa walipoweka kifungu cha Afisa usalama kukamata na kufanya upekuzi walijua hata onekana na kujulikana? Wanafahamu taratibu za ukamataji na upekuzi huanzia kwa Mwenyekiti/mjumbe wa mtaa/kitongoji na kisha mashahidi wa mtuhumiwa ndipo mtu apekuliwe? Je hapo afisa huyo atakuwa kafichwa utambulisho wake, sura yake au?
Mswada huu ni wa hovyo na haufai kabisa kupitishwa kuwa Sheria. Ukipitishwa kama ulivyo ni automatically hatutakuwa na Usalama wa Taifa, bali tutakuwa na Jeshi jipya lililochukua nafasi ya Idara ya Polisi ya upelelezi tu.
Dunia inapambana kufanya mageuzi Mashiriks ya Ujasusi yawe na mrengo wa kuhami uchumi, Lakini Serikali ya CCM imeleta mswada unaoirudisha TISS nyuma kuwa genge la kisiasa kulinda madaraka rasmi kutoka awali kuwa TISS ilifanya shughuli za kisiasa/kichama kinyemera, Sasa Rais Samia anairasmisha kuwa kikundi cha kulinda na kutetea madaraka ya kisiasa. Very sad!
Napendekeza kifungu hiki cha 5A kirekebishwe, TISS isihusike na ukamataji wala Upekuzi wa mtu yoyote katika nchi, isipokuwa ipewe idhini ya "kudhibiti" kwa mtindo wa elimination ama equity/excute katika eneo muhimu tu. Ukamataji na upekuzi ubakie kwa Idara ya upelelezi ambayo ndio itahusika na mambo ya Mahakamani pia. Kifungu cha 16 kirekebishwe, kimeweka mkazo sana katika kuficha utambulisho, dunia ya Teknolojia ni vigumu sana kwa maafisa kuficha utambulisho wake, badala yake kazi/Oparesheni ndio ziwekwe kwenye sheria ya kuzuia utambuzi wake.
Leo naomba niongelee juu ya contradiction ya vifungu hivi viwili cha 5A na 16 vya mswada huu, kati ya vifungu 27 vya marekebisho ya sheria ya Usalama wa taifa.
Na Yericko Nyerere
Sehemu ya 1.
Moja ya makosa ya mswada wa sheria ya Usalama wa Taifa, kipengele cha 5 cha mswada huo kinampa mamlaka Afisa usalama kukamata na kupekua viongozi, hapa Kifungu hicho kina kinakinzana na Katiba ya Jamhuri ya Muungano inayosema kila mtu sawa mbele ya sheria, Kifungu kinaweka tabaka kwamba viongozi wa kitaifa hawatawajibika mbele ya sheria ya makosa ya jinai inayosimamiwa na jeshi la polisi, Viongozi wote watakuwa na sheria yao na chombo chao cha kuwakamata, kuwapekua na pengine wanaweza kuwa na mahakama zao.
Duniani kote Afisa usalama hafanyi kazi ambazo ni za wazi. Ukishamruhusu akamate na kupekuwa ni automatically umeamrisha afisa usalama huyo afike mbele ya mahakama kutoa ushahidi wa mtuhumiwa kama mkamataji na mpekuzi. Kazi hii iliwekwa kwa Idara ya upelelezi pekee na sio TISS.
Ajabu katika mswada huohuo, unajipinga katika kifungu cha 16 ambapo umeweka katazo la Afisa usalama kutotajwa wala kutojulikana popote yeye binafsi na kazi zake. Unajiuliza hivi hawa walipoweka kifungu cha Afisa usalama kukamata na kufanya upekuzi walijua hata onekana na kujulikana? Wanafahamu taratibu za ukamataji na upekuzi huanzia kwa Mwenyekiti/mjumbe wa mtaa/kitongoji na kisha mashahidi wa mtuhumiwa ndipo mtu apekuliwe? Je hapo afisa huyo atakuwa kafichwa utambulisho wake, sura yake au?
Mswada huu ni wa hovyo na haufai kabisa kupitishwa kuwa Sheria. Ukipitishwa kama ulivyo ni automatically hatutakuwa na Usalama wa Taifa, bali tutakuwa na Jeshi jipya lililochukua nafasi ya Idara ya Polisi ya upelelezi tu.
Dunia inapambana kufanya mageuzi Mashiriks ya Ujasusi yawe na mrengo wa kuhami uchumi, Lakini Serikali ya CCM imeleta mswada unaoirudisha TISS nyuma kuwa genge la kisiasa kulinda madaraka rasmi kutoka awali kuwa TISS ilifanya shughuli za kisiasa/kichama kinyemera, Sasa Rais Samia anairasmisha kuwa kikundi cha kulinda na kutetea madaraka ya kisiasa. Very sad!
Napendekeza kifungu hiki cha 5A kirekebishwe, TISS isihusike na ukamataji wala Upekuzi wa mtu yoyote katika nchi, isipokuwa ipewe idhini ya "kudhibiti" kwa mtindo wa elimination ama equity/excute katika eneo muhimu tu. Ukamataji na upekuzi ubakie kwa Idara ya upelelezi ambayo ndio itahusika na mambo ya Mahakamani pia. Kifungu cha 16 kirekebishwe, kimeweka mkazo sana katika kuficha utambulisho, dunia ya Teknolojia ni vigumu sana kwa maafisa kuficha utambulisho wake, badala yake kazi/Oparesheni ndio ziwekwe kwenye sheria ya kuzuia utambuzi wake.
Leo naomba niongelee juu ya contradiction ya vifungu hivi viwili cha 5A na 16 vya mswada huu, kati ya vifungu 27 vya marekebisho ya sheria ya Usalama wa taifa.
Na Yericko Nyerere