Zitto Kabwe: Rais Samia aondoe hati ya dharura kwenye Muswada wa Sheria ya Usalama wa Taifa, pia TISS ikaguliwe matumizi yake ya fedha

JanguKamaJangu

JF-Expert Member
Feb 7, 2022
2,308
5,458


Kiongozi wa ACT Wazalendo, Zitto Kabwe akizungumza katika mkutano wa hadhara Ktavi, amesema;

"Tulivyopata taarifa kuwa muswada wa sheria ya usalama wa Taifa umefichwa - fichwa tukasema, wametusikia na sasa wameuweka wazi kwamba sasa wataujadili.Hii ndiyo faida ya vyama vingi kwamba tunasema,wanasikia,wanaona kuwa wamekosea na baadae wanasahihisha.

"Muswada wa sheria ya usalama wa Taifa una baadhi ya maeneo mazuri sana ambapo kwa asilimia 60 unaboresha idara ya usalama, inarasimisha idara, inaboresha maeneo ambayo ni ya kizamani na sasa yanaenda kuwa ya kisasa.

"Asilimia 40 ya Muswada wa sheria ya usalama wa Taifa ina matatizo,ambapo kuna masuala ya haki za watu yanaenda kukandamizwa na sisi ACT wito wetu ni kutaka mabovu yaboreshwe na hakuna haja ya kuharakisha sheria hii.

"Muswada huu wa sheria ya usalama wa Taifa kama utapita hivi ulivyo, unaenda kutoa kinga ya kijinai kwa Maafisa wa usalama kwamba akifanya makosa ya kijinai kwenye majukumu yake ya kikazi haitowezekana kumshtaki."


"Maafisa usalama wa Taifa (TISS) ndiyo wanalaumiwa kwa utekaji wa watu, ndiyo wanaovuruga uchaguzi, ndiyo wanaotishia watu mtaani. Ukiwaruhusu hawa watu wateke halafu ikibainika wameteka sheria inazuia kumpeleka mahakamani, watateka zaidi.

"Kipindi ambacho sheria haiwapi kinga wameteka! vipi wakiwa na kinga? Sasa hivi tuna Rais Samia ndiyo ila atamaliza muda wake. Nani kasema CCM haina Magufuli mwingine? Wanao, wanawatoa tu kabatini baada ya kusoma upepo wa kisiasa unavyoenda.

Sheria ya usalama wa taifa ya Marekani imewapa kinga CIA, Uingereza imewapa kinga maafisa wao wa idara za MI5 na MI6.Wenzetu wanachokifanya kwa maafisa wao ni kwamba ukiitumia kinga yako vibaya inaweza kuondolewa na ukafikishwa mahakamani.

"Kwenye muswada wa sheria yetu lazima tuwe na kifungu kitakacholazimisha uwepo wa kamati ya kibunge ya kusimamia idara ya usalama wa Taifa ambayo inaweza kuondoa kinga kwa afisa wa TISS, ili kuruhusu kuchunguzwa pale wanapovunja haki za binadamu kwenye majukumu yao.

"Wakati wa mjadala Bunge likiridhia kuundwa kwa Kamati ya kuisimamia idara ya TISS kwenye muswada huu, kamati itakayoundwa ijumuishe pia wabunge wa upinzani. Bunge kamili linakuja baada ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2025,sio bunge hili la sasa.

"Lazima pia mabadiliko haya ya sheria ya usalama wa taifa yaweke udhibiti wa matumizi mabaya ya ofisi kwa maafisa wa usalama wa Taifa (TISS), bila kufanya hivyo na wakafanikiwa kuwa na kinga ya kutoshtakiwa wataua na kutesa sana wananchi."

"Kamati itakayoundwa kuisimamia idara ya usalama wa Taifa (TISS) ifuatilie pia matumizi ya fedha ya idara ya usalama wa Taifa kupitia fungu la 20 ndani ya mafungu ya serikali. Fungu hili huwa halikaguliwi na CAG ilihali JWTZ wenyewe hukaguliwa matumizi yao ya fedha.

"Marekani ukishakuwa mgombea Urais unalindwa na idara ya Secret Service ambayo ni idara inayojitegemea ikiwa tofauti na shirika la Ujasusi (CIA). Kama nasi tunataka Viongozi na Wagombea urais walindwe na usalama wa Taifa basi tuwe na idara maalum itakayokuwa huru.

"Sisi mambo yote ya usalama tumeyaweka ndani ya idara moja kiasi kwamba TISS inatumika sana kisiasa na CCM. TISS wanasahau kushughulika na mambo makubwa ya kiuchumi, ufisadi na uwekezaji wa nje na ndani, wanaanza kuhangaika na wanasiasa - wameenda wapi, wanafanya nini.

"Mapendekezo yetu ACT tuwe na idara inayojitegemea kufuatilia maslahi ya nchi na uwekezaji wa nchi. Iundwe idara maalum ya Tiss kufuatilia mambo ya nje ya nchi na kujua wenzetu wanafanya nini huko vyenye athari kwenye mipango na mikakati yetu ya ndani.

"Tunamuomba sana Mh. Rais Samia Suluhu aondoe hati ya dharura kwenye muswada wa sheria ya usalama wa Taifa, muswada uingie kwa utaratibu wa kawaida ili tupate sheria iliyo bora kwa wananchi na sheria bora kwa maafisa wa usalama wa Taifa."
 
 
Zitto aache zake bana. Watu hatulali ili yeye na mke wake wawe salama. Kwanza budget yenyewe haitutoshi inabidi tuongezewe.

Ngoja tumsummon makao makuu atueleze vizuri.
 


Kiongozi wa ACT Wazalendo, Zitto Kabwe akizungumza katika mkutano wa hadhara Ktavi, amesema;

ACT wanajiona ni chama tawala! Inaamini dhamira ya serikali kuleta mswada huu ni njema na kwa hiyo wamejielekeza katika kuuboresha! Kwa mtazamo wao wanaamini kama ilivyo Marekani na Uingereza hii idara yetu ya Usalama nao wanaweza kupewa kinga dhidi ya makosa ya jinai ilimradi tu kutakuwa na kamati ya Bunge ya kuisimamia! Kwa mabadiliko yanayopendekezwa, kimuundo TISS yenyewe itakuwa chini ya Rais moja kwa moja na mabadiliko yanakusudia kuondoa kabisa vyombo vingind vya serikali vilivyokuwa na dhamana ya kushiriki katika usimamizi wake! Je, hapo bado kuna dhamira njema? Haya yanafanyika wakati huu nchi ikiwa katika vuguguvu la kutaka mabadiliko ya kikatiba ikiwa ni pamoja na kutawanya madaraka katika taasisi na vyombo mbalimbali. Ndiyo kusema dhamira njema haipo.

Usalama wameshutumiwa sana kwa matendo mabaya ya utekaji wa raia, mauaji na watu kupotea. Kwa muda huu wote ni kitu gani kimezuia lisichunguze hayo malalamiko ya raia? Sababu hiyo iliyofanya Bunge kushindwa hata kukemea "watu wasiojulikana" licha ya kuchunguza ndiyo hiyo hiyo itakayofanya hiyo kamati ya Bunge kuwa "toothless". Na sababu yenyewe ni mamlaka makubwa ya rais ya kuwa juu ya katiba, sheria na hata Bunge.

Kuna mambo hatuwezi hata kidogo kujifananisha na nchi za wenzetu zilizokomaa katika "check and balances"! Hivi kweli katika hali halisi kiutendeji TISS inafanana na CIA na MI5? Nao wanateka wanaharakati na wakosoaji wa serikali? Wanafuatlia mienendo ya wanasiasa wa vyama shindani? Wanajihusisha na kulinda maslahi ya chama kilichoko madarakani? Wanapoteza raia wanaokosoa vyeti vya viongozi wa serikali? Wanashiriki kuvuruga uchaguzi?

Hofu kubwa ya raia wa nchi hii kwamba mswada wa marekebisho ya sheria ya usalama ni mwendelezo wa ule mpango wa serikali ya awamu ya tano wa kuigeuza hii nchi kuwa mali binafsi ya watawala (fiefdom)! Mpango huo umekuwa ukitekelezwa kwa kutunga na kupitisha haraka haraka sheria kandamizi ikiwa ni pamoja na kutoa madaraka yaliyopitiliza kwa wateule wa rais na watu wengine walioko katika nafasi ya ya kuwezesha ubinafsishwaji huo wa nchi kama Bunge na Mahakama. Kama raia wa nchi hii tutakuwa tunakosea sana kama leo tutageuka kuwa vipofu wasioweza kuona mambo tuliyokuwa tukiyaona jana na kuyapigia kelele kwa sababu tu kuna mtu mmoja katika uongozi wa kisiasa ameondoka hata kama dhamira ya waliobaki na matendo yao ni ni yale yale.
 
ACT wanajiona ni chama tawala! Inaamini dhamira ya serikali kuleta mswada huu ni njema na kwa hiyo wamejielekeza katika kuuboresha! Kwa mtazamo wao wanaamini kama ilivyo Marekani na Uingereza hii idara yetu ya Usalama nao wanaweza kupewa kinga dhidi ya makosa ya jinai ilimradi tu kutakuwa na kamati ya Bunge ya kuisimamia! Kwa
Ubarikiwe sana.... yaani nchi hii binafs naona bora TISS sheria iseme kuwa ni idara ya kuilinda ccm na viongozi wake...TISS wamekosa sifa kbs kulinganisha na hzo idara za nchi za walioendelea... Kila ovu la nchi hii wao wako yake... ufisadi wao, utekaji wao, kuvuruga chaguzi za nchi wao...daaah
 
ACT wanajiona ni chama tawala! Inaamini dhamira ya serikali kuleta mswada huu ni njema na kwa hiyo wamejielekeza katika kuuboresha! Kwa mtazamo wao wanaamini kama ilivyo Marekani na Uingereza hii idara yetu ya Usalama nao
Pengine hawa tuwapongeze japo kwa hiki kimchango kidogo!! Kuna wengine wanatembea tu angani na Buyu la asali, wapo kimyaaa
 
Unataka kujua nini?????
Je, unataka kujua kwamba bajeti ya mpango mzima uliosukwa wa "kumuua Tundu Lissu" uligharimu shiilingi ngapi?????Je, unatakakujua hili kweli????
Definitely unaonekana ni mtu mwenye u dictator na roho mbaya, Nina wasiwasi kuhusu malezi yako yalikua ya kikatili na bila upendo, matumizi ya tiss ni kodi yangu, I have a right to know na issue ya Mh. Lissu hii ni police case, ni wajibu wa police kuelezea what's happened kwa MP kupigwa risasi na sio kwa kesi hii pia kuna kesi za Akwilina, Azory, CoCo beach etc etc, ndio maana ipo siku nitalivunja jeshi la police love,nitaajiri young graduates na kuwapeleka nje kwa mafunzo ,definitely traffic officer's nitawapeleka Botswana ili waone wenzao wanavyofanya kazi with zero corruption, and all cops above 40yrs nitawastaafisha kwa manufaa ya umma,Tanzania it belongs to all tanzanians sio kwa ccm au royal families
 
Definitely unaonekana ni mtu mwenye u dictator na roho mbaya, Nina wasiwasi kuhusu malezi yako yalikua ya kikatili na bila upendo, matumizi ya tiss ni kodi yangu, I have a right to know na issue ya Mh. Lissu hii ni police case, ni wajibu wa police kuelezea what's happened kwa MP kupigwa risasi na sio kwa kesi hii pia kuna kesi za Akwilina, Azory, CoCo beach etc etc, ndio maana ipo siku nitalivunja jeshi la police love,nitaajiri young graduates na kuwapeleka nje kwa mafunzo ,definitely traffic officer's nitawapeleka Botswana ili waone wenzao wanavyofanya kazi with zero corruption, and all cops above 40yrs nitawastaafisha kwa manufaa ya umma,Tanzania it belongs to all tanzanians sio kwa ccm au royal families
Tiss ni kichaka cha Wanasiasa watawala kwa ajili ya kuficha diri zao, sasa wewe na wenzako mnataka kukifyeka kwa Ukaguzi wa CAG ili Siri zao zibaki uchi, unaona hili litawezekana kweli???
 
Back
Top Bottom