Unakumbuka kuna siku niliweka masharti kadhaa tulijadili jambo la Uwepo wa Mola muumba,ukapita wima ?
Wewe una mamlaka gani wa kuweka masharti? Masharti gani? yana mantiki gani? Yako wapi? Kwa niniunayatajasasa?
Halafu nina kudai maswali mengi sana.
Hujamalizia kuelezea ya masharti usharukia maswali mengi sana?
Una matatizo ya akili wewe?
Mimi kuna muda huwa nakuuliza maswali sio kwamba natarajia unijibu la hasha,sababu najua huwezi kunijibu. Ila lengo langu ni kuwafikishia habari wale wasemaji mengine waone madhaifu yenu.
Mimi nikishindwa kukujibu swalilolote hilo si la ajabu.
Unanielewa?
Katika ulimwengu ambao haujaumbwa na Mungu mjuzi wa yote, mwenye uwezo wote na upendo wote, watu wengi tu tutakuwa hatujui majibu ya maswali mengi tu.
Hivyo, nikikwambia sijui jibu la swal lolote, si kitu cha ajabu.
Cha ajabu ni pale, wewe unayesema ulimwengu huu umeumbwa na Mungu mjuzi wa yote, mwenye uwezo wote na upendo wote, halafu ukashindwa kujibu swali lolote.
Hapo utakuwa unatupacontradiction, ulimwengu ulioumbwa na Mungu huyo unatakiwakuwa na watu wenye ukamilifu wa elimu kw amaswali yote wanayoweza kuulizana.
Kutokuwa na majibu kwa baadhi ya maswali ni ushahidi kwamba Mungu mjuzi wa yote, mwenye uwezo wote na upendo wote hayupo.
Hili swali la kuhusu MUDA ulianza lini najua huna huwezo wa kulijibu hata wakubwa zako ukiwapa swali hawawezi kulijibu.
Nikishindwa kulijibu swalihili, huo ni ushahidi Mungu mjuzi wa yote, mwenye uwezo wote na upendo wote hayupo.
Angekuwepo asingekuwa mchoyo hivyo kuninyimajibu, kwa sababu uwezo wa kunipa jibu anao, upendo wa kunipa jibu anao, ujuziwa kunipa jibu anao, kwa nini aninyime jibu?
Mungu wako mchoyo?
Mtu yeyote kuwa na swali lolote asilo na jibu lake ni ishara kwamba huyo Mungu hayupo. Inabidi tutafute majibu wenyewe.
Nafanya hivi kuwaonyesha wasomaji ya kuwa nyinyi ni waongo na mnakariri hoja ndio maana maswali na hoja zenu ni hizi hizi,yaani mkitegwa kidogo mnapoteana mazima.
Unaweza kuthibitisha Mungu yupo?
Sasa swali la kuhusu MUDA nimekuuliza zaidi ya masaa matatu nyuma mpaka muda huu hujalijibu.
Nikikwambia sijui jibu, hilo halithibitishi Mungu yupo.
Linathibitisha Mungu hayupo.
Unaweza kuthibitisha Mungu yupo?