Yani hakuna la kujifunza kwa hawa jamaa,muda wote katika majadiliano nao wao ni watu wa kupinga,kuuliza maswali(kwa nia ushindwe kujibu) na kukana.
Halafu kwa kuyafanya hayo ndio hutaka kukuamisha kuwa hakuna Mungu,yani hukutengezea mazingira ya kuamini kuwa hakuna Mungu na sio kueleza hasa ni vp hakuna Mungu? Ni sawa na mtu wa imani A aishambulie imani B,halafu kwa kufanya hivyo ndio afikiri inatosha kufanya imani A kuwa sahihi.
Sijawahi kuona hoja za huu msimamo wa kuwa hakuna Mungu,yani huu msimamo umekuwa kama shimo ambalo watu wakianguka hudondokea humo na si kwamba kuna sababu za msingi zilizofanya waingie kwenye hilo shimo.
Ndio maana unakuta mtu msimamo wake hakuna Mungu ila kakazana kubishania masuala ya contradictions kwenye vitabu vya dini,na anataka kwa mabishano hayo hayo ya contradictions kwenye vitabu vya dini ndio iwe hitimisho la kuwa hakuna Mungu!!!