Bado majibu na mifano yako ni mepesi kiasi hata hayajajibu hoja ya mtoa mada
Mpaka leo naamini hivi tajiri anaeponda kila aina ya raha na yeye nitachomwa nae moto if wote tumetenda dhambi duniani
Kama mungu yupo kwanini akawa mwenye upendeleo hivi huku duniani
Yaani mimi nizaliwe na masikini alafu mwingine azaliwe na tajiri
Tusome wote tufaulu sawa lakini mimi nitafute kazi bila mafanikio alafu wewe upate kirahisi
Nikiwaza hapa ndo naona kabisa kama kweli mungu yupo basi hakuna moto wa jehanamu na kama moto upo
Basi mungu si mwenye huruma, upendo na, mtenda haki.
Mwenzako alizungumzia juu ya taabu na majanga yanayowapata watu na akahitimisha kuwa Mungu hayupo kama angalikuwepo basi angalizuia hayo majanga na taabu ili WOTE tuishi kwa raha na starehe.
MImi nilimjibu kuwa hiyo hoja yake ni "self contradictory" kwa sababu kama Mungu hayupo kutokana na majanga na taabu zetu, je duniani pia hakuna raha na starehe??utasema nini juu hizo starehe na raha??.
Halafu, majanga yako ya aina mbili, kwanza yapo yale ya kujitakia mfano inapotokea ugonjwa wa kuambukiza kama kipindupindu, mtu ukipata huo ugonjwa maana yake umekula kinyesi kibichi kilichokuwa na vimelea vya kipindupindu, sasa ukiugua kipindupindu unamlaumu Mungu??, Yeye hajakupa AKILI ya kujua tahadhari ya kujikinga??.
Pili kuna majanga ya asili (natural), majanga ya aina hii huwa ni adhabu au mitihani ya Mungu kwa watu, ni adhabu pale watu wanapozama katika kumusi Mungu kwa kufanya madhambi, ni mtihani ili Mungu aone mnapopata shida mtamtegemea nani na hii ni baada ya watu kumuacha Mungu na kushika njia ya USHIRIKINA ambapo wankuwa na majivuno na jeuri na moja kwa moja wana msahau Mungu.
Unahoji juu ya utofauti wa maisha katika jamii kwamba wengine wamezaliwa katika familia za kimasikini na wengine katika familia za kitajiri.
👆🏻Ni ajabu kuleta hiyo hoja kwamba ndiyo utetezi wako kuwa Mungu hayupo!!?😁😁 Sasa ulitaka dunia yote tuwe sawa katika suala hilo??, kama ni hivyo kila mtu angetaka awe rais, au awe kama Billy Gate au mwingine angelaumu kwanini kawa na jinsia aliyonayo nk, kifupi kama hiyo ichukuliwe ni hoja basi dunia ingalikuwa ni uwanja wa fujo na kusingekuwa na maendeleo yoyote kwa sababu watu wote tungekuwa UNIFORM hakuna yeyote angemfanyia mwingine kazi na DUNIA INGESIMAMA NA WATU WOTE KUFUTIKA. ni hoja too illogic, nadhani hapa atheist wenzako watakusaidia.
Umezungumzia juu ya moto jehanam, ni kwamba watu wengi hawajui falsafa (hekima) ya moto wa jehanamu kiasi kwamba wanamlaumu Mungu bure au kumkanusha kuwa hayupo, Jehanamu ni kama hospitali inayotibu roho kutokana madhambi, madhambi ni kama ugonjwa na moto ni kama dawa chungu sana (nasty medicine) ya kuondoa hayo madhambi. Hivyo unaposema adhabu ya moto mfano wake ni ukali wa dawa ya kutibu roho na baada ya mtu kupona (kutolewa madhambi yake) basi ataingizwa peponi na kuanza na moja, lakini kule motoni watu watakaa muda mrefu sana (abadan) kulingana na wingi wa madhambi yake. Hapo ndipo unapoona huruma ya Mungu mtukufu keamba anataka sisi sote twende peponi tukiwa safi na peponi ndiyo makazi aliyotuandalia baada sisi kuwa safi.