Kaka naona umechagua kutokuelewa.
Kaka unakubali kama huwezi kuthibitisha kama Allah mlezi hayupo ?
Wewe ukiniambia kuwa hakuna mzazi mwenye umri wa miaka 30 ambae ana mtoto mwenye umri wa miaka 50,
Hapohapo nikakwambia thibitisha kama hayupo kweli,
Huyo mzazi unaweza mtoa wapi ili mimi nimuone na kusema kweli hayupo?
Ukishamleta ndiyo utakuwa umenithibitishia kwamba hayupo?
Kisichokuwepo wala hakihitaji kuthibitishwa hakipo,nje ya sifa za uwepo wake.
Wewe unayesema yupo ndiyo unapaswa kuthibitsha yupo.
Allah mwenye uwezo wote,ujuzi wote na upendo wote hayupo kwa sababu dhana ama sifa za uwepo wake zinajipinga zenyewe.
Ni kama isivyowezekana kuwepo kwa mtu mwenye miaka 30 halafu mwanae wa kumzaa akawa na miaka 50.
Na kuthibitishwa kwake kuwa hayupo ni kutazama sifa za kwamba haiwezekani mzazi kuwa na umri pungufu ya mwanae wa kumzaa.
Na mimi nasema Mungu hayupo kwa sababu ya sifa lukuki alizonazo na ambazo zinajipinga na hivyo kumfanya asiwekane kuwepo.
Tafakuri fupi ni hii,
Kwa uwezo wote alio nao Allah, anaweza kuumba jiwe zito ambalo hawezi kulibeba?