Makonda aahidi kuwasaka mashoga mahotelini

Makonda aahidi kuwasaka mashoga mahotelini

Mkuu wa mkoa wa dsm kasema kuwa atapambana na mashoga popote walipo ataenda hadi mahotelini.. Source Magazetini
My take: kuwafuata mashoga mahotelini ni hatari. Ila nampa support yangu. Hii hulka ya ushoga ni mbaya sana

=======

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda ametangaza operesheni ya kuwasaka mashoga jijini humo.

Makonda amesema vitendo hivyo vimeanza kuongezeka jijini humo na lengo lake ni kuwaokoa watoto wasiige mambo hayo yanayoonekana kukua kwa kasi.

Bosi huyo wa mkoa amesema, “hili ni tatizo linalokua kwa kasi sitaruhusu liendelee katika mkoa wangu, nitawasaka popote walipo”.

“Hata hapa bandari wanaweza kuwapo mashoga wafichueni, mkiona mtu ana tabia za ajabu ajabu mfichueni, tutashughulika nao”.


Chanzo: Mwananchi
Safi sana,eti huyo ndio mkuu wa mkoa,hii ni laana tena ya kiwango kikubwa kabisa,au laana imempata baada ya KUMPIGA MAKOFI Mzee WARIOBA,kazi ya mkuu wa mkoa sio kupambana na MASHOGA,hiyo haipo kabisa katika utendaji wake,anatakiwa kufanya jitihada katika majukumu nyeti ambayo yamedorora tangia awamu nne zilizopita ili kuhakikisha hadhi na maendeleo ya mkoa wa Dar yanakuwepo kwa kiwango kinachotakiwa sio kufuatilia mashoga mahotelini,huo ndio uongozi wa kukurupuka.
 
Kimsingi katika nchi ambayo tunaambiwa kila dakika mama anayejifungua anapoteza maisha yake, ni aibu kwa kiongozi yoyote kutangaza kuwa priority yake ni kukimbizana na mashoga hotelini. Mkuu wa mkoa Makonda kaa chini utafakari usije ukajikuta unapoteza relevance katika jamii. Hivi kweli utampa ripoti ya mwezi Rais Magufuli kuwa mwezi Julai ulikuwa unakimbizana na mashoga hotelini?
 
Kuna kero Mingi sana hio ya ushoga hata akipoteza nguvu haitaleta impact pawekwe sheria kali na tu mtu akibainika ila sio kuwatafuta mahotel hio ni privancy na mtu
 
Kwa hii kazi ya kuDeal na Mashoga Makonda ataharibu ndoa yake bila kutarajia! Hao jamaa wanaweza kuandamana na mabango yaliyoandikwa MAKONDA ALIKUA NI MTEJA WETU!
 
Hadi sasa hajui kiki gani itamtoa jamaa,sukari imebuma,kufufua magari,madawati sasa mashoga
 
Labda angeshughulika na ajira kwa vijana wenzie na akina mama hawa jamaa wawe wa mwisho sababu wanafanya kwa hiyari yao na hataweza kumaliza.

Afanye yanayowezekana na yaliyo ndani ya uwezo wake wengine wanawaingilia kinyume wake zao na mademu zao atawapataje.

Manake kama sako la nyani ngedere wataponaje maba.sha wao wako wapi.
 
Mkuu wa mkoa wa dsm kasema kuwa atapambana na mashoga popote walipo ataenda hadi mahotelini.. Source Magazetini
My take: kuwafuata mashoga mahotelini ni hatari. Ila nampa support yangu. Hii hulka ya ushoga ni mbaya sana

=======

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda ametangaza operesheni ya kuwasaka mashoga jijini humo.

Makonda amesema vitendo hivyo vimeanza kuongezeka jijini humo na lengo lake ni kuwaokoa watoto wasiige mambo hayo yanayoonekana kukua kwa kasi.

Bosi huyo wa mkoa amesema, “hili ni tatizo linalokua kwa kasi sitaruhusu liendelee katika mkoa wangu, nitawasaka popote walipo”.

“Hata hapa bandari wanaweza kuwapo mashoga wafichueni, mkiona mtu ana tabia za ajabu ajabu mfichueni, tutashughulika nao”.


Chanzo: Mwananchi

Wananchi wa Dsm wana shida nyingi sana za kijamii na za kiuchumi kuliko kadhia ya uwepo wa mashoga! Nini vipaumbele vyetu? Pia yeye hawezi kukamata, hivyo atahitaji polisi ambao kwa sasa hawatoshi wala kulinda watu wa Dsm na mali zao! Kwenda kuwatumia polisi hao kwenye operation zake sio matumizi mabaya ya nguvu kazi ya Taifa? Pia operation hizo zitahitaji bajeti ya utekelezaji, hapo sio matumizi mabaya ya kodi za wananchi?
 
Wananchi wa Dsm wana shida nyingi sana za kijamii na za kiuchumi kuliko kadhia ya uwepo wa mashoga! Nini vipaumbele vyetu? Pia yeye hawezi kukamata, hivyo atahitaji polisi ambao kwa sasa hawatoshi wala kulinda watu wa Dsm na mali zao! Kwenda kuwatumia polisi hao kwenye operation zake sio matumizi mabaya ya nguvu kazi ya Taifa? Pia operation hizo zitahitaji bajeti ya utekelezaji, hapo sio matumizi mabaya ya kodi za wananchi?

Ukitaka kuchota akili za Waafrika wengi ili kuficha madhaifu yako ya kiuongozi we tangaza vita tu na mashoga!

Fanya vita dhidi ya ushoga kuwa ndo kipaumbele chako.

Uhakika wa kutawala milele kama Mugabe unao!

Hata kama wanashinda kwa kula mavii ya nguruwe watakuunga mkono tu kisa unapinga ushoga.
 
H
Marekani wameruhusu ushoga hadi jeshini... Makonda hajui anachotaka kukifanya.. Kwenye hili marekani watakuwa very serious na harshy.. Msishangae misaada yote kufutwa
Hivi ni States zote Marekani zinaruhusu ushoga?
 
Achana nao huo mfupa umemshinda fisi ( mama mzazi/mlezi ) hautauweza wewe
Kama vipi awatafute drugs lord ambao ni maarufu uko kino na magomeni awashtaki na kuwafunga
 
Mimi sijaelewa kiundani hii issue, kwani kuna sheria yoyote juu ya ushoga?

Na hao mashoga wanawasumbuaje watu kiasi kwamba waendesha nchi wawasake mjini dar, huku wezi na majambazi wanaosumbua wananchi wapo wamekaa mkao bila kusumbuliwa na wengi wanajulikana na hao wengine?

Sasa tunasubiri kusikia kavamia nyumba za majambazi na wezi waliokubuu wa jijini kwake maana hata kutembelea Dar, tunaogopa siku hizi. Bora zaidi mkoani kwangu.
1467479712776.jpg
 
Vipi yule aliyekuwa anahojiwa Clouds TV ameshamkamata?!
 
Back
Top Bottom