Makomandoo wa Bongo

Makomandoo wa Bongo

Mimi nimeshuhudia komandoo wa kiisrael alizunguukwa na Makomandoo wa Hizbullah, alijigeuza kuku ili akwepe ! Hata hivyo walimkamata na kumfanya kitoweo!

Daaaah!!!mkuu..hapo sasaaa.....ni kufurahisha wana jf.😀😀😀
 
unaposkia komando haijalishi nchi anayotoka.., uwezo wake ni wa hali ya juu sana,, sasa kwny huo uwezo wa juu wanapishana huko kutokana na task na specialization..., kwa mfano navy seal team 6, ni wataalam wa counter-terrorism, lakn hapo hapo kwny navy seal commandos wapo specialised kwa tactics nyingine...,

Hapa tz, zamani commandos alikua for general purpose, lakn ikaonekana kuna haja ya specialization ndo maana saivi kuna marine commandos pale navy,, wanasomea china

Pia kuna airborne, hawa wanakua na bawa moja lakn wanafanya mafunzo mengi kama infantry commandos na haja ya kufanya hivyo ni kwa sbb wanakua deployed behind enemy lines, wanafundishwa kufanya kazi kwa vikundi vidogo lakn kwa ufanisi mkubwa

Kuna programme ilioneshwa tbc last year, ungeamini kua jamaa wako fiti..., watu wanavunja tofali kwa vichwa, watu wana uwezo wa kuruka gari.., in short wapo fiti....

Na unapolinganisha na wa nje, makomando wetu wengi wanapata mazoezi nje ya nchi...., katika kikosi maalumu kinachosafirisha sana wanakikosi basi ni 92kj(sangasanga)...,

Commandos wetu wanavaa maroon beret au kwa kiswahili rangi ya damu..., wako tayari kutoa damu yao kwa taifa,

Mm binafsi nimeshashuhudia wanalala wima wanaegemea ukuta!!!

Hawa watu wako fit kweli, they are pushed to the boundary na hapo 92 mazoezi ya vikwazo au ya kimapigano ni live fire, ukifanya masihara unarudi maiti

Kwa kifupi umempa jibu japo si kiundani kabisa lakini wengi wataelewa Hongera sana
 
Jua tu mafunzo yote ya kijeshi ni ya aina moja, nikimaanisha mvitabu vinavyoyumika hapa ndivyo wantumia USA, RUSIA , GERMANY, FRANCE na kwingineko. Majeshi huzidiana ktk vifaa,mazoezi, molali, utayari wa mapambano na matunzo. Mafunzo ya komandoo wa tz ni bora hata kuliko hao wa nchi za magharibi ila vifaa ndivyo hatuna. Angalia hata bunduki wanazotumia makomandoo wetu SMG, hii si bunduki bora kw komandoo anayefanya kazi ya askari wa kawaida 9.

Ushauri nenda JKT ukapate walau hints za kijeshi.
Napingana na wewe Mkuu makomandoo wa tanzania wanatumia AK 47 and above...see the picture below....
jwtz2.jpg
 
Nakubaliana na wewe lakini wakati mwingine pamoja na uchumi kuna vitu vya ziada kwani Somali kumzidi Marekani ni kwa sababu ya uchumi? Na habari ya top ten ya majeshi siwezi kuiamini sana kwa sababu mambo ya ulinzi wa nchi huwa ni siri hivyo tathmini inaweza isiwe rahisi ki hivyo! maoni tuu mkubwa

hata kuwa skilled inategemeana katika nyanja gani, hata kutembea kwa miguu kunahitaji uchumi?

tuache kupigana kamba.
kulingana na uchumi tulionao tz si rahisi kuwa na watu ambao ni skilled compare to those owned by NATO kama wanajamvi wengine wanavyonadi.
juzjuz kuna mtu alipost thread moja inayoelezea majeshi imara top ten africa tz hatupo.
tuache stori za magenge ya kahawa za kupoteza muda.
weak economy = weak army.
najua kuna wenye akili za kuvukia barabara watabisha 2
fakenology wacha kutudanganya TZ ni ya sita Africa kwa kuwa na jeshi bora gonga link below....
https://www.jamiiforums.com/interna...ntries-with-the-strongest-army-in-africa.html
 
Last edited by a moderator:
macomando wote duniani wanakaa kwa komando kipensi, just kidding!
 
Jamani mnafananishaje waagizaji na wahusika halisi? Au sijawaelewa? Wale wa kwenye movie sio askari ni waigizaji tu. Hawa wa kwetu mnaowaona kukiwa na maaadhimisho ya kitaifa ndiyo wa ukweli yaani real. Ukimuleta Rambo hapo ukamuonesha wa kwetu na kusema wapambane. Rambo atakuuliza what crime have I committed to deserve death sentence?
 
Mimi ninachojua kuhusu makomandoo ni kimoja tu. They don't make themselves known to public! Because if the enemy knows u r a commando atajiandaa vilivyo kukukabili. So element of surprise is crusial to them. Hii philosophy ni world wide ndo maana seal team six hawajulikani kwa public. Labda kama kwa Tanzania hichi kitu haki apply tuambiane mapema.
 
mi naongelea hasa maujanja ya kwenye shughuli, kama vile kupita kwenye moto, kushusha kipondo cha kiteknikali kabisa, kucheza na vyombo vya kivita,,mfano kumpiga kabali piloti na yeye kuongoza ndege,,kubembea kwenye mkia wa ndege afu anasavive mpaka anaenda kumteka rubani.

uliza kongo kwa m23!!!
 
Wakuu naomba kujua kama hawa makomandoo ni kama wale ambao huwa nawaona kwenye video.

Kuna mmoja nilipanda nae daladala la posta G/mboto na pale begani pameandikwa kabisa komandoo ,,, ,,,, ,,,.

Sasa napenda kujua mafunzo yao ni kama yale yenyewe kabisa? yani yani yani kabisa yani .....wanauwezo ule wa ukweli kabisa yani kama komando john zile yani?
Makomando wetu wana mafunzo mazuri na wapo fiti sana,kenya kama wangeomba msaada tanzania kwenye tukio la westgate kazi ingeisha siku ileile jeshi la kenya wanavifaa vingi lakini dhaifu sana.M23 ya congo,vita ya liberia,comoro nk. wote wamesambaratishwa na makomando wetu. Mara kadhaa wanajeshi wa marekani,uingereza,italy,france,china wamekuja kufanya mazoezi na wanajeshi(makomando) wetu hii ni kuonyesha wanakubalika nje ya afrika kwa umahiri wa kupambana kwenye vita
 
Tunategemea tutawaona kesho wakiruka kwa miamvuli inshallah
 
Teh,jamani eeh,kila binadamu ni komandoo kiasili,hii ni kwa misingi ya uvumilivu,ujasiri,nguvu na utumizi wa akili kulingana na mazingira na uhitaji...nani anabisha? Chunguza maisha yako utagundua kama wewe ni komando au sungusungu.
 
Teh,jamani eeh,kila binadamu ni komandoo kiasili,hii ni kwa misingi ya uvumilivu,ujasiri,nguvu na utumizi wa akili kulingana na mazingira na uhitaji...nani anabisha? Chunguza maisha yako utagundua kama wewe ni komando au sungusungu.

Nimeamini kwamba sisi binadamu si wa kawaida Juzi!
Usiku wa kuamkia juzi Sikulala kabisa, nilijipumzisha kitandani naangalia TV, ilipofika saa 9:50 usiku nikaanza safari kwenda Sengerema Mwanza kutokea hapa Dar! Saa 10 nilikuwa nakatiza Ubungo mataa! Nimeendesha kutwa nzima nilisimama Dodoma tu si zaidi ya dakika 10! Taarifa ya habari ya saa 2 usiku nimeangalia Sengerema! Na sikuwahi kuendesha umbali mrefu zaidi ya Chalinze! Sikuchoka wala kusinzia njiani! Sijui Ujasiri na uvumilivu huo ulitoka wapi!
 
Nimeamini kwamba sisi binadamu si wa kawaida Juzi!
Usiku wa kuamkia juzi Sikulala kabisa, nilijipumzisha kitandani naangalia TV, ilipofika saa 9:50 usiku nikaanza safari kwenda Sengerema Mwanza kutokea hapa Dar! Saa 10 nilikuwa nakatiza Ubungo mataa! Nimeendesha kutwa nzima nilisimama Dodoma tu si zaidi ya dakika 10! Taarifa ya habari ya saa 2 usiku nimeangalia Sengerema! Na sikuwahi kuendesha umbali mrefu zaidi ya Chalinze! Sikuchoka wala kusinzia njiani! Sijui Ujasiri na uvumilivu huo ulitoka wapi!

Afu yakitokea tunasema kazi ya Mungu haina makosa,.haya mkuu wewe ni jasiri kweli
 
Wanahitajika kuwakamata wale matapeli wa Escrow account,maana mpaka sasa jeshi la polisi sioni kama litakuwa lina ujasiri wa kuwakamata..
 
afu kwa mambo kama haya sio rahisi kujua ufanisi wao hadi ufahamu wanatumikaje na wapi., na walitumikaje huko nyuma.., kuna thread hapa nimesahau heading nilichangia kuhusu co-ops(covert operations) ambazo tanzania imewahi kuzifanya bila wananchi wengi kufahamu...,

sasa kwny hz co-ops makomando ndo their specialty.., we have done a lot of co-ops kukomboa nchi za kusini mwa afrika including kufundisha sabotage(kuharibu miundo mbinu kwa milipuko).., assasinations of key members of the colonial powers, organizing movements covertly, etc

hyo field ni ya makomandoo chini ya makamanda

Naomba link ya huo uzi
 
Back
Top Bottom